SIKUJUA, KITABU KIPYA CHA HADITHI KIKO MITAANI


SIKUJUA

Wazazi wake walikuwa wamekata tamaa ya kupata mtoto wakati mimba ilipotungwa bila wao kutarajia. Jitihada za wataalam wa kisasa na wale wa asili zilikuwa zimegonga mwamba.
Kila mmoja alistaajabishwa na ujauzito ule wa ghafla!!

Akazaliwa mtoto wa kike wakamuita SIKUJUA….
Na kweli hawakujua na hakuna aliyejua!!

Mzee Chapakazi haupati wasaa wa kuishi muda mrefu na binti yake wa pekee, katika namna ya ghafla sana anaugua na kuaga dunia! Anamuachia maagizo mazito mkewe juu ya binti yao Sikujua.
Mama Sikujua anayapokea na kuyahifadhi moyoni.

Sikujua akakua kwa hekima na kimo, akautambua ugumu wa maisha na kujidhatiti katika elimu, Akavuka madarasa na hatimaye vidato….

Alijifunza mengi katika elimu ya darasani lakini hakuikumbuka elimu dunia!!
Hatimaye akakutana na upepo wa mapenzi ukaanza kumpeperusha na hatimaye akajikuta anafanya jambo zito bila kujua madhara yake!!

Baada ya miaka kadhaa akiwa anafurahia maisha zimwi lile alilodhani amelizika miaka kadhaa nyuma likamrudia!! Tafsiri ya jina lake ikaja katika uhalisia lakini tayari alikuwa amechelewa sana………

Ni jambo gani lililomtafuna Sikujua na nini hatma yake!
Fungua ndani uburudike na kujifunza kutoka katika mkasa huu ulioegemea katika maisha halisi….

NI HADITHI MPYA KUTOKA KWA MTUNZI MAHIRI ANAYEFAHAMIKA KAMA ‘CHANGAS MWANGALELA’ KITABU HIKI SI CHA KUKOSA, KWANI KINA MENGI YA KUJIFUNZA KATIKA MAISHA TUNAYOYAISHI MIMI NA WEWE.

KIMEINGIA SOKONI JUMATATU MARCH  17, 2014.
JIPATIE NAKALA YAKO KWA BEI POWA KABISA  YA Tsh 7000/=
 KWA MAWASILIANO PIGA NAMBA 0713 193 002 & 0753 172654, ILI UJIPATIE NAKALA YAKO!!!!

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU