HOFU

SEHEMU YA SABA

ARUSHA

Ilikuwa saa moja asubuhi wakati F.K alipoegesha gari lake. Huku nusu akitembea  nusu akikimbia , aliingia nyumbani. Majasusi wote walikuwa wanamsubiri kwa hamu.

"Eh imekuwaje?", George aliuliza.

"Paul na Fouche wameuawa!", F.K alijibu.

"Nini?", Dave aliuliza kwa ghadhabu.

"Wamekufa", F.K alieleza. "Polisi wanasema maiti zao zimekutwa Equator Hotel. Sasa hivi Polisi wanafanya upelelezi kwani watu hawa hawana rekodi kuhusu kuwa kwao nchini. Zaidi ya hayo, hakuna jibu lolote kutoka kwa Peter Gerrit, sijui kumetokea nini!".

"Mungu wangu, maana hata Peter ameuawa?", Dave aliuliza.

"Sijui, lakini hakuna jibu. Hivyo wanahisi kuna kitu kimetokea".

"Oke, sasa kazi imeanza. Katika mchezo huu mambo kama haya sharti yatokee. Hivi Bon na wenzake wametupiku. Sasa ni zamu yetu kufunga kazi; F.K kazi yetu ya usiku wameisha izungumzia? George aliuliza.

"Kati ya wale watu wawili ni ofisa mmoja wa wapigania uhuru ambaye ameuawa. Yule wa sabasaba Hoteli alikuwa mfanyabiashara. Kwa hiyo hicho chumba kimekosewa", F.K alijibu kwa sauti ya uwoga.

"Nafikiri ni lazima uifanye kazi yako vizuri, F.K sharti ulete habari sahihi maana kazi kubwa iko leo usiku. Kusema kweli kama mtafanya mchezo mtateketea nyote. nyinyi wenyewe mmeona jinsi Paul na Fouche walivyoangamia. Inatubidi kujidhatiti na kufunga kazi haraka. Jambo moja lazima niwahakikishie; hakuna kushindwa, sawa?", George alisema kwa ukali.

"Sawa", wote walijibu kwa pamoja.

"Oke, tuendelee na maelezo kuhusu mipango ya mashambulizi ya siku nzima", George alishauri.

Wote walisogea ili kila mmoja wao ajue kazi yake na jinsi ya kuitekeleza.

ITAENDELEA

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU