HOFU

SURA YA SITA

MAMBO

II

Siku hiyo ilikuwa sikukuu ya Idd-elftri. Mjini Nairobi mchana ule Mike alikuwa ofisini akipokea ripoti kutoka kwa Mwaura.

"Tangu jana mimi na vijana ulionipa tulikuwa tunachunga nyumba hii kwa zamu", Mwaura alisema. "Hata hivyo, hatujagundua kitu chochote. Hakuna mtu hata mmoja ambaye ametoka nje ya nyumba ile. Ila kuna kitu kimoja kinashangaza. Ni kwamba jioni hatumwona Peter akirudi nyumbani. Na Onyango ameniletea habari kuwa amemwona akirudi sasa hivi tunahisi kwamba Peter hakulala nyumbani".

"Unayo hakika hakurudi na kutoka?", Mike aliuliza.

"Labda hiyo iwe wakati tulipokuwa hatujaanza doria wakati wa mchana".

"Hivyo una maana wale watu bado wako ndani?".

"Bila shaka. Labda tu ule muda ambao nilikuja hapa kuwasiliana nawe. Maana kama nilivyokwambia jana, kwa muda ule wa masaa manne hapakuwa na ulinzi", Mwaura alijibu.

"Mike Maina alifikiri sana na kisha akasema. "Sidhani, lakini lazima tuwe na uhakika mtu anaweza kufanya hivyo kama amehisi kuwa tunamfuata".

"Sidhani kama alikuwa ameniona", Mwaura alieleza, "Mimi naelewa kuwa mtu ambaye huchukua tahadhari na mwenye ujuzi kama Peter hawezi kuwa katika hali ile kama alihisi kufuatwa na watu. Bali Onyango aliniambia alipokuwa anarudi leo mchana alionekana kama mtu mwenye wasiwasi kuwa anafuatwa".

"Ndio. Hapa kuna kitu kinanitia wasiwasi sijui ni nini! Mwaura jiweke tayari mnamo saa sita usiku nipitie nyumbani kwangu. Tutakwenda kwa Peter kwani lazima tuhakikishe kuwa mambo gani yanaendelea ndani ya nyumba yake. Waache wale vijana waendelee kufanya kazi", Mike aliagiza.

"Sawa mzee", Mwaura alijibu.

ITAENDELEA

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU