HOFU

SEHAMU YA KUMI

MAMBO BADO

Ilikuwa yapata saa sita kasoro dakika kumi wakati Bon alipobisha hodi kwenye chumba cha Willy, huku akiwa na bastola mkononi tayari. Mike alikwenda kufungua. Akiwa tayari kabisa, aliruka haraka upande.

"Lo! Mungu wangu vipi?", Mike aliuliza baada ya kumwona Bon".

"Willy yuko wapi?", Bon aliuliza kabla ya kujibu.

"Amewafuata", Mike alijibu.

"Kama nusu saa hivi. Nyaso amempeleka na atarudi si muda mrefu. Rocky yuko wapi?", Mike aliuliza.

"Mike. Rocky ameuawa", Bon alijibu.

"Hapana", Mike alisema bila kuamini.

"Ukweli ni kwamba watu hawa ni majasusi wa hali ya juu. Twende tumfuate Willy. Huko njiani nimeona gari likielekea nyumbani kwa F.K. likiwa limejaa watu. Iwapo Willy yuko peke yake, atapata matatizo. Heri tumfuate kwani hatuwezi kumpotenza na Willy pia. Mambo mengine nitakueleza njiani. Kwani hatuna muda. Nyaso akirudi anaweza akatusubiri hapa hapa", Bon alisema.

Bila kusema neno Mike alichukua zana zake na wanaume wakatelemka chini. Mbele ya hoteli walipungia taksi na kupanda.

"Tupeleke Themi Hill", Bon alimwamrisha dereva. wakaondoka.

ITAENDELEA

Comments

Post a Comment

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU