UCHU

SURA YA PILI

KAZI KWAKO

"Umesikia George Foreman amerudi ulingoni na kutwaa ubingwa", Chifu aliuliza.

"Sikusikia tu, nimeona kwenye televisheni".

"Basi na wewe nataka urudi ulingoni", Chifu anasema kwa tabasamu huku akiupaka mkate wake siagi.

"Mimi! mimi nimeoa na mke wangu ana mimba. Mchezo huo sifanyi, sifanyi ng'o".

Chifu anaangua kicheko kiasi cha kuwafanya watu wote ndani ya chumba cha mkutano wamwangalie.

"Kwani mimi sijui umeoa! Kwani mimi sijui mke wako ana mimba! Najua, lakini nakutaka ulingoni tena. Kwani George Foreman hana mke, hana watoto, mbona karudi ulingoni", Chifu aliendelea kusema kwa kebehi.

"Huenda alikuwa anataka pesa, huenda alikuwa anatafuta sifa, mimi sitaki vitu vyote hivyo, sirudi ng'o", Chifu alielezwa kwa busara.

"Sikiliza nikueleze kwanza. Mimi ndiye niliyekuruhusu uache kazi na kukushauri uoe na nisingependa uharibu ndoa yako. Najua unampenda sana mkeo, sasa nasema nisikilize kwa makini nikueleze, kama utakataa itanibidi niingie mimi mwenyewe ulingoni", Chifu alijibu kwa masikitiko kiasi cha kumfanya mwenzake apoe hasira zake.

"Chifu, hebu nieleze kuna nini? Kitu cha maana namna hiyo, kiasi cha kusema utafanya kazi hiyo mimi nisipokubali? Unajua mimi siwezi kukuruhusu wewe kufanya hivyo.

"Basi sikiliza".

Ilimchukua Chifu saa nzima kumweleza suala la Rwanda na jinsi msimamo wa PAM ulivyohusiana pamoja na vipengele vingine vingi ambavyo hata akina Musoke wasingeweza kumweleza maana hawavijui.

"Unafikiri Serikali ya sasa ya huko haiwezi kufanya kazi hiyo", Chifu aliulizwa.

"Haiwezi. Inahitaji ujuzi wa hali ya juu kufanya kazi hiyo, katika hali ya machafuko namna ile, maana hata wao hawajui nani ni nani katika nchi yao. Hawamwamini mtu yeyote na wao hawaaminiki vilevile na kuweza kupata habari za kina kama zinavyotakiwa, unahitajika ujuzi wa juu sana. Na katika Afrika nzima kama si wewe basi itanibidi mimi mwalimu wako nikaifanye.

"Umenipa mtihani mkubwa sana. Unafikiri kazi kama hii inaweza kuchukua muda gani?".

Chifu alipoulizwa swali hili, moyo wake ilitulia akijuwa kazi itafanywa.

"Inategemea na wewe mwenywe, wiki moja au mbili, mwezi yote yategemea wewe. Kwani Pepe atajifungua lini?".

"Bado ana miezi miwili".

"Nakutakia heri. Nafikiri utamaliza kazi kabla ya hapo. Tafadhali, hafadhari iwe kitu cha kwanza kwako maana huko kuna hatari nyingi, usifanye mchezo kama unataka kumwona mtoto wako", Chifu sasa alikuwa amebadilika na kumwasa mwenzake.

"Nikifa utamlea wewe", Alijibu.

"Sasa nina miaka sabini, nitamlea miaka mingapi mie", Chifu alijibu.

"Wewe ndiye uliyetaka, shauri yako, damu yangu itakuwa juu ya kichwa chako".

"Pole sana. Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania inaondoka saa tano na nusu kwenda Kilimanjaro. Tiketi hii hapa, umepatiwa nafasi kwenye ndage hiyo. Musoke mtaonana uwanja wa ndege, atakuja kukupokea, si unamfahamu?".

"Ndio, namfahamu".

"Haya kwa heri. Ukirudi toka Arusha, kabla ya kwenda Kigali, njoo unione nitakuwa tayari na taarifa za kukusaidia kule".

"Asante, nitafanya hivyo.

Chifu alilipa wakaondoka.

ITAENDELEA 0784296253


Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU