TAFUTA UKWELI
III
Ilikuwa saa
kumi na mbili alfajiri simu ya JKS ilipolia na kumwamsha usingizini.
"Hallo,
nani?", JKS aliuliza huku amebanwa na usingizi.
"Phillipe".
"Ehe,
sema", alijibu kwa shauku.
"Matanga
hayatakuwepo, mtu wetu hakulala pale, na hata hajulikani kalala wapi,
alionekana akiingia lakini hakuna aliyemuona wakati akitoka. Funguo za chumba
kaziacha chumbani, Kavurugavuruga kitanda lakini hakukilalia. Tumefanya utafiti
katika hoteli na nyumba zote za kulala wageni Arusha nzima,hayupo. Mtu wako ni
mjuzi, naamini maneno yako", Phillipe alimalizia.
"Haya
asante, kazi imeanza". JKS alikata simu baada ya kusema.
IV
Baada ya
kutelemka Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, akitokea Arusha
alikwenda kwenye ofisi za Tanzaniar za pale uwanjani na kwa bahati alimkuta
meneja hajaondoka, hivyo akafanya mipango ya kukodi ndege yao kesho yake
alfajiri ili impeleke Kigali. Ingawa ndege zao zilikuwa na kazi nyingi kesho
yake, lakini kwa vile ile biashara ya kwenda Kigali ilikuwa nzuri, meneja
alimkubalia ila akaomba Willy asaidie kupata ruhusa ya kutuwa kwenye uwanja wa
ndege wa Kavihanda wa mjini Kigali. Willy alilipa na kuahidi kuwa angejitahidi
kupata hiyo ruhusa. Alipewa kila kitu ambacho kingehitajika kule Kigali ili
kibali kipatikane.
Willy
alifika nyumbani yapata saa mbili usiku baada ya kupokelewa uwanja wa ndege na
kuletwa moja kwa moja nyumbani na Ismail, dereva wa AVIS. Alitoa shilingi elfu
tano akampa Ismail kama bakshishi.
"Asante
sana mzee, gharama zitawekwa kwenye akaunti yako", Ismail alijibu.
"Kama
kawaida. Asante kwa kuja kunipokea na kwa heri", Willy alijibu na
kutelemka kwenye gari.
"Kwa
heri mzee", Ismail alimwaga.
Pepe alikuwa
jikoni akipika wakati Willy alipoingia ndani. Mara alipomwona alitoka jikoni
akamkimbilia sebuleni huku akiwa ameshikilia kipande cha nyama.
"Karibu
nyumbani bwana wee", kabla Willy hajajibu, Pepe alimkumbatia na kumbusu.
Tumbo la Pepe lilipoligusa la Willy, akahisi mtoto akicheza tumboni.
Kitu ambacho
kilimwongeza furaha. Willy, bila kujua akadondosha mkoba wake, na kuendelea
kumbusu Pepe. Mara Pepe akamsukuma kidogo na kuangalia jikoni asije akaunguza,
na kumwekea Willy kile kipande cha nyama alichokuwa ameshikilia mdomoni, kisha
alitabasamu na kukimbilia tena jikoni ambako Willy naye alimfuata.
"Siku
nyingine utafanya moyo wangu usimame kwa raha unazonipa", Willy alisema
akiwa amemshikilia Pepe begani, huku Pepe akikaangiza nyama kwenye chungu.
"Sasa
nimpe nani raha kama si wewe mume wangu", Pepe alijibu.
"Kuoa
kutamu", Willy alijibu.
"Kutamu
sana, kama ukioa ama kuolewa na akupendaye ki-kwelikweli", Pepe alijibu
huku akimtupia jicho la mahaba.
Willy
alimgeuza na kuanza kumbusu tena.
"Inatosha
kwa sasa. Ngoja kwanza nikakuwekee maji uoge, halafu utakuta chakula tayari
ndipo unieleze kwanini umechelewa kuja nyumbani", Pepe alieleza.
"Nakwambia
kuoa kutamu, najisikia kama mtoto wa miaka mitatu, nilivyokuwa nafanyiwa na
Mama Willy", Willy alijibu kwa dhati kabisa kwani kila aliporudi nyumbani
Pepe alimfanya ajisikie kama mtoto, na hivyo kusikia raha isiyo kifani.
Baada ya
kuoga na kula, huku wakizungumza mambo yao ya kawaida Willy alifikiria jinsi ya
kuanza kumweleza Pepe juu ya safari yake.
Ni mpaka
walipokwenda kulala ndipo Pepe alipotoa wasiwasi wake. Wakiwa wameingia
kitandani na kujifunika shuka, Pepe alijilaza juu ya kifua cha Willy na
kuuliza.
"Chifu
keshanieleza huenda ukasafiri kesho, mbona husemi?".
"Mara
moja Willy alimfikiria Chifu ambavyo alijaribu kumsaidia ili asipate tatizo
lolote kuhusu masuala ya nyumbani.
"Nilikuwa
najishauri nitaanzaje kukueleza".
"Unaenda
kesho lakini", Pepe aliuliza kwa sauti kali kidogo.
"Ndio
alfajiri", Willy alijibu kwa unyonge.
"Sawa",
Pepe alijibu.
"Sawa
ya ukweli au ya hasira?".
"Sawa
ya kikwelikweli, naelewa. Naelewa ya kwamba mpaka umekubali kuondoka uniache,
kweli ni lazima uende, nami yafaa nikubaliane nawe. Willy nataka uelewa kitu
kimoja, najuwa unavyonipenda, na unajuwa ninavyokupenda kwa hiyo uamzi wako
ndio uamzi wangu, najuwa lingekuwa jambo la hivihivi tu usingekubali na Chifu
asingejaribu kama alivyojaribu kunisihi nikueleze. Nimeelewa. Willy, nakupenda
Willy, nakupenda sana", Pepe alisema na kuanza kububujikwa na machozi
ambayo yalianguka kifuani kwa Willy.
Kwa mara ya
kwanza maishani mwake, Willy naye machozi ya mapenzi yalimtoka. Mara mtoto
tumboni kwa Pepe alicheza na mara hii kwa fujo sana, na kwa vile walikuwa
wamekumbatiana ndani ya shuka Willy naye alimhisi.
Kitendo hiki
cha mtoto kiliwatoa kwenye haya mawazo yao ya majonzi ya kuachana kwa muda na
kuwarudisha katika hali yao ya furaha ya kawaida".
"Mtoto
hataki tuwe na majonzi", Willy alimnong'oneza mkewe.
"Haswa",
Pepe alijibu na kumkumbatia kwa kujibana kabisa kwenye mwili wa mumewe na
kuweka mguu wake juu ya mapaja yake.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment