Katika jitihada za kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dar es Salaam, Mlinzi huyu wa Makampuni binafsi amekutwa akisaidia kuongoza magari kwa ustadi mkubwa, katika Barabara ya Zanaki leo
Akiwa ameyazuia magari kutoka upande mmoja wa Barabara ili kuruhusu magari ya upande mwingine yapite
Akionyesha ishara kwa madereva wanaokwenda kulia kufanya hivyo ama wanaokwenda moja kwa moja
Akiangalia kama kuna magari mengine kutoka upande wa pili kabla ya kuruhusu magari yapite.
Akizungumza na dereva aliyeonekana kukaidi amri yake. Hata hivyo Dereva huyo alitii amri na kusimama.
Akifanya manjonjo kama wafanyavyo Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani wanapoongoza magari. Hapati ujira, halipwi chochote, lakini ameguswa kusaidia kupunguza msongamano wa magari, tusimbeze.
Comments
Post a Comment