KIKOSI CHA YANGA
LIGI Kuu ya
Soka Tanzania Bara inaendelea leo, katika mzunguko wa saba, huku Vijana wa
Jangwani chini ya Kocha, Marcio Maximo Yanga wakipania kulipa kisasi kwa Mgambo
JKT ya Handeni Tanga, iliyotia ndimu safari ya Yanga kutwaa Ubingwa msimu
uliopita.
Mchezo wa
leo unatalajiwa kuwa mkali nawenye ushindani wa aina yake hasa baada ya Yanga kufungwa
bao 1-0 mwaka jana na kupoteza mchezo wa raundi ya sita dhidi ya Kagera Sukari,
uliochezwa mkoani Kagera, nao Mgambo wakipata sare dhidi ya Mbeya City mkoani
Tanga.
Katika
mchezo wa leo, Kikosi cha Yanga kitawakosa wachezaji wake nyota, Nahodha Nadir
Haroub Canavaro aliyepewa kadi nyekundu mkoani Kagera wakati Yanga ikilala bao
1-0 na mlinzi kisiki Kelvin Yondan mwenye kadi tatu za njano, ambazo zinamfanya
asicheze mchezo wa leo.
Kutokana na
pengo hilo, Yanga italazimika kuwatumia wachezaji wake kama Zahir na Salim
Telela, ambao wamekuwa benchi kwa muda mrefu, katika safu ya ushambuliaji timu
inatarajiwa kuwapa nafasi akina Jerrison Tegete na Husein Javu walioonyesha
uhai wakati wa mchezo dhidi ya Stand United.
Mbali na
mchezo huo utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam majira ya saa kumi
alasiri. Mabingwa watetezi Azam watakuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani Chamazi
kuwakaribisha ‘Wagosi wa Kaya’ Coastal Union kutoka Tanga, Mtibwa Sukari watawakaribisha
ndugu zao Kagera Sukari, Stand United na Mbeya City.
Comments
Post a Comment