Kocha Mkuu wa Yanga Marcio Maximo, ambaye uongozi na mashabiki wa Yanga wamemchoka
Nahodha wa Yanga Nadir Haroub 'Canavaro', alifanya kazi kubwa ya kuzuia mashambulizi.
Kpah Sherman alionyesha uwezo mkubwa japo hakupata msaada
Emerson Oliveira, alionyesha kiwango kidogo wakati Yanga ilipocheza na Simba
Nahodha wa Yanga Nadir Haroub 'Canavaro', alifanya kazi kubwa ya kuzuia mashambulizi.
Kpah Sherman alionyesha uwezo mkubwa japo hakupata msaada
Emerson Oliveira, alionyesha kiwango kidogo wakati Yanga ilipocheza na Simba
Winga Mshambuliaji wa Yanga Simon Msuva ambaye uwezo wake haulingani na wachezaji wa Maximo
Kikosi cha Yanga kilicholambishwa subiri na Simba, Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
“Ni ndoto ya mchana Yanga kuwafunga mahasimu wao Simba”, Ndivyo
unaweza kusema, itabaki
kuwa historia kwani wapinzani wao wanajuwa mbinu za kuwafunga, wakati ushindi wa Yanga ni sare. Kasumba
iliyojengwa na viongozi wa Yanga kukimbilia kusajili kila mchezaji anayetakiwa
na Simba itaendelea kuwafanya wafungwe kila watakapokutana, hali hiyo
ikichagizwa pia na Kocha Mkuu wa Klabu hiyo, Mbrazil, Marcio Maxime.
Hivi
karibuni Simba ilitangaza kumsajili mshambuliaji mkongwe wa Polisi Morogoro,
Danny Mrwanda, baada ya Yanga kupata tetesi, viongozi wa Klabi hiyo walifanya
mipango ya haraka kumsajili kana kwamba wanawakomoa Simba, kumbe wanaongeza
mamluki ndani ya klabu.
Hakuna
asiyefahamu kuwa Mrwada ni mchezaji na mwanachama hai wa Simba, na uongozi wa
Simba kutaka kumsajili ni mkakati mojawapo wa kumrejesha kundini kada huyo
aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nje ya Tanzania kwa muda mrefu.
Waswahili
wanasema kikulacho ki nguoni mwako, kwa kiasi Fulani Simba imewekeza wachezaji
wao ndani ya Yanga, wakati Yanga wenyewe hawajawekeza ndani ya Simba, kwa hali hiyo, Yanga isitegemee miujiza
kuwafunga Simba.
Mtoto wa
nyoka ni nyoka, Ndani ya Yanga wapo nyoka kama, makipa Ali Mstafa, Deogratius
Munis na Juma Kaseja (anayeondolewa msimu huu, mlinzi kisiki Kelvin Yondan
aliyesajiliwa Yanga mwaka jana na sasa wamemchukua kada mwingine mwandamizi wa
klabu hiyo ya Msimbazi Danny Mrwanda na Amis Tambwe ambaye Simba wameona kiwango
chake kimeshuka.
Kuhusu Kocha
Maximo, ataendelea kuwaudhi mashabiki wa Yanga kwa kuwaleta wachezaji wenye
uwezo mdogo ili wachezaji wenye wazawa wenye uwezo mkubwa wa kusakata soka
wasipate namba. Kitendo cha Maximo kuwaleta ndugu zake Emerson Oliveira na
Andrey Coutinho na kuwaacha Jerryson Tegete, Hussein Javu, Nizar Khalfan na
Salim Telela wenye uwezo mkubwa ni kuiangamiza Yanga.
Wakati
umefika Yanga watambue kuwa si kila Kocha kutoka Brazil ana uwezo, hebu
tuwapatie kazi makoche wetu wazalendo, wenye mapenzi makubwa na Yanga kama
Boniface Mkwasa, Fred Minziro na Juma Pondamali. Hakika Yanga itafanya vizuri,
poleni wana Yanga wote.
Comments
Post a Comment