MCHEZO wa Nani Mtani Jembe, unaozikutanisha timu mbili kongwe zenye
upinzani wa jadi nchini, Yanga na Simba imegeuka kuwa machinjio kwa makocha wa Yanga baada ya Kocha Mkuu wake Mbrazil Marcio Maximo kutimuliwa rasmi jana kufuatia kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Simba.
Huu ni msimu wa pili mfululizo, kwa Yanga kuwafukuza makocha wake baada ya kufungwa na Simba, kwa kupoteza mchezo wa nani mtani jembe. Mchezo wa kwanza uliofanyika mwaka jana, 2013, Yanga
ilifungwa 3-1 na kusababisha aliyekuwa kocha wake Ernie Brandts kutimuliwa
pamoja na benchi lake la ufundi.
MARCIO MAXIMO
Mwaka huu Kocha Marcio Maximo nae amefungashiwa
virago baada ya timu yake kungwa mabao 2-0 Jumamosi iliyopita Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ukiwa
mchezo wa nane wa ushindani baada ya michezo saba ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania
Bara.
Maximo aliyepokelewa Jangwani na mashabiki wa Yanga kwa vifijo na
nderemo Juni mwaka huu baada ya kutangazwa kuwa Kocha mpya wa timu hiyo,
amewaaga rasmi wachezaji wake wakati wa mazoezi uwanja wa Sekondari ya Loyola Dar es
Salaam jana.
Mazoezi hayo ya Jumanne asubuhi yaligeuka simanzi baada ya
Maximo kuwakusanya wachezaji wake na kuwatakia maisha mema ndani ya Klabu hiyo
ya Jangwani huku akionekana mwenye shauku ya kutaka kuendelea na kibarua chake.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wachezaji walielezea
kutoridhishwa na uamuzi wa uongozi wa kumuacha kocha wao akiwemo mshambuliaji Hamis
Kiiza kutoka Uganda. Mmoja wa wachezaji ambaye hakupenda kutajwa jina alisema "Ni kweli kocha
ametuaga, lakini angepewa muda!
Comments
Post a Comment