MTABIRI WA NYOTA SHEIKH SHARIFF MATONGO AKIONGEA NA WAANDISHI LEO
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mtabiri wa
nyota Sheikh Shariff Matongo amezungumza na waandishi wa habari Dar es
Salaam leo, akidai kuwa ameoteshwa ndoto na Mwenyezi Mungu na kupata ushauri kutoka kwa
Masheikh mbalimbali Duniani kuwa mambo mazito saba yatatokea likiwemo la
mchakato wa kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete mwaka 2015, ambaye nyota zinaonesha nafasi hiyo itashikwa na mtanzania aliyeishi nje
ya Tanzania kwa muda mrefu.
Sheikh Shariff amewaambia
waandishi wa habari kuwa,mwaka 2015
kitatokea kifo cha kiongozi mzito, aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali
ndani ya Chama tawala (CCM). Amesema pia zitanyesha mvua nyingi na
watu waishio mabondeni watasombwa na mafuriko, vitatokea vifo vingi vya
watoto, baadhi ya wafanyabiashara watapata mafanikio mwaka 2015.
Amewaambia waandishi wa habari kuwa, nyota
zinaonyesha vijana wengi watang'ara na kushinda Ubunge na Udiwani
katika uchaguzi mkuu ujao. Amewataka vijana kujitokeza kwa wingi
kuwania nyadhifa hizo kwani wazee wengi watapoteza nafasi hizo.
"Baada
ya kuota ndoto hii sikukaa kimya, niliuliza na kutafuta ushauri
kwa watu
mbalimbali duniani, mfano nimeongea na Mufti wa Abhudhabi,
Nigeria na
wengine ambao wamenishauri nisikae kimya, ndio maana
nikawaita
kuwafahamisha kuhusu utabiri wangu", amesema Sheikh Shariff
Matongo.
Kuhusu
usafiri na majini, Sheikh Shariff amesema utakuwa na misukosuko
ya hapa na
pale kwani bahari itachafuka na kusababisha mawimbi mazito na
hatimaye
chombo kimoja kitazama kutokana na hali hiyo amewataka watoa
huduma ya
usafiri wa majini kuwa makini.
Sheikh
Shariff amewaasa watanzania kuzingatia maoni na ushauri wake
kutokana na
ndoto hizo. Hata hivyo alipoulizwa kama amewahi kuota ndoto
zenye
mtazamo kama hiyo hakuwa tayari kutoa maelezo isipokuwa
amesisitiza
kuwa ndoto yake isipuuzwe.
Kazi kwenu
mnaotafuta Unyerere wa Tanzania kwa udi na uvumba, mtabiri
anasema
nyota inaonyesha mrithi wa Rais Kikwete lazima awe ameishi nje
ya Tanzania
kwa muda mrefu. Huyo hatufai, kama anaishi nje ya Tanzania
kwa muda
mrefu hatakuwa chaguo halisi la watanzania.
Watanzania
wanahitaji kiongozi wanayemfahamu, awe karibu na wananchi kwa shida na
raha, awe ameishi ndani ya Tanzania akiyajuwa vizuri matatizo
ya
watanzania, mtu aliyeishi nje ya Tanzania kwa muda mrefu ni dhahili
kuwa haujuwi
vizuri utanzania wake, yawezekana akaja na heleni masikioni
ama kidali
mguuni, huyo atakuja kwa ajili ya kuuza nchi.
Ni jambo
lisilotia shaka kuwa watanzania wanasubiri kwa shauku kubwa
kipyenga cha
mbio za urais, Ubunge na udiwani ili wawachague viongozi
wawapendao.
Watanzania wengi wametangaza nia ya kugombea urais. Kila
mmoja akiwa
na siri yake moyoni.
Watanzania
waliotangaza nia ya kuwania nafasi hiyo hadi sasa ni Wawaziri
Mkuu Mizengo
Pinda, ambaye hata hivyo anatajwa kuwa hana sifa kutokana
na kushindwa
kuonyesha uwezo kwenye nafasi aliyonayo sasa. Wengine ni
Mawaziri
Wakuu Wastaafu Edward Lowassa na Fredrick Sumaye, Mawaziri
Benard Membe
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Lazaro
Nyarando wa
Maliasili na Utalii, Mark Mwandosya asiye na Wizara maalum
na Steven
Wassira wa UMahusiano na Uratibu Ikulu.
Wengine
wanaotajwa kuwania nafasi hiyo ni Naibu Waziri wa Sayansi na
Teknolojia,
January Makamba, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Emanuel Nchimbi,
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja na Mwana mama pekee
Asharose Migiro.
Comments
Post a Comment