Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (aliyeshika tama pichani), ametangaza kujiuzulu rasimi
wadhifa huo, Jijini Dar es Salaam leo, kufuatia kashfa nzito ya uchotaji wa Sh. Bilioni 306,
zilizokuwa kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, inayowakabiri yeye na wenzake.
.
Waziri
Muhongo amelazimika kutangaza kujiuzulu leo ikiwa ni siku chache tu kabla ya kuanza kwa vikao
vya Bunge la Jamhuri ya Muungano, Mjini Dodoma. Lakini wachunguzi wa mambo wanasema
Profesa Muhongo amepita uzito wa kashfa hiyo dhidi yake na kulazimika kujiuzulu kukwepa maswali mengi ya Wabunge.
Sakata hilo
ambalo lilimlazimu Rais Jakaya Kikwete kumuondoa aliyekuwa Waziri wa
Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ambaye awali aliwaambia waandishi wa habari kuwa yeye na
Waziri mwenzake Profesa Muhongo, hawawezi kujiuzulu kwa sababu Rais
Kikwete atawashangaa kwani anawategemea sana katika majukumu yake.
Pamoja na
majigambo hayo ya Profesa Tibaijuka, Rais Kikwete alitangaza kumuondoa kwenye Baraza lake la Mawaziri, akidai kuwa maelezo na jinsi alivyopokea mapesa hayo
kupitia kwenye akaunti yake vinatia shaka, Hata hivyo Rais Kikwete alikimweka Waziri Muhongo kiporo.
Kitendo cha Rais Kikwete kutangaza kuwa Waziri Muhongo amewekwa kiporo, kilichukua sura mpya baada ya wana harakati na wapenda demokrasia nchini, walidai kuwa kiporo cha Profesa
Muhongo kilikuwa kimechacha.
Uchunguzi wa
kina uliofanywa na MPIGANAJI, umebaini kuwa Wabunge bila kujali
itikadi ya vyama vyao walikuwa wamejipanga kumshambulia Profesa Muhongona kumshinikiza aachie ngazi. Ni wazi kuwa shinikizo la Wabunge limemsukuma Profesa huyo kuachia ngazi kabla ya
kurudi Bungeni.
Kuahirishwa kwa Bunge mjini Dodoma, mwishoni mwa mwaka jana ni kama kulileta ahuweni
kwa Mawaziri hao, kwani mijadala yote ya nchi ilisimama huku wabunge wengine
wakiwatetea wasiochie ngazi wengine wakisema wezi hao waondoke.
Baada ya kuahirishwa Bunge Mjini Dodoma, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alitangaza kujiondoa mwenyewe na nafasi hiyo kuwa wazi kwa muda kabla ya Rais Kikwete kumteua Mwanasheria Mkuu Mpya.
Hata hivyo,
baada ya Profesa Tibaijuka kuwekwa kando na Rais Kikwete, alirudi kwao, mkoani
Kagera kama shujaa wa vita akisindikizwa na msururu mrefu wa magari zaidi ya mia moja, ambayo
baadhi ya wapenda maendeleo ya nchi yao, walisema mafuta yaliyotumika kwenye msafara huo yangeweza
kujenga Maabara za shule kadhaa mkoani humo.
Sasa watanzania
wanasubiri kuona, nani ataingia kwenye baraza la mawaziri nani atatoka,
kufuatia tetesi na uvumi kuwa Rais Kikwete anapanga kuliwekea viraka baraza hilo.
Profesa Muhongo ni Waziri wa tatu kujiuzulu kutoa Wizara ya Nisati na Madini, wengine ni Ibrahimu Msabaha, aliyejiuzulu kutokana na sakata la RICHMOND na Wiliam Mganga Ngereja.
WATANZANIA KAZI TUNAYO.... IMEANDIKWA NA MPIGANAJI
Profesa Muhongo ni Waziri wa tatu kujiuzulu kutoa Wizara ya Nisati na Madini, wengine ni Ibrahimu Msabaha, aliyejiuzulu kutokana na sakata la RICHMOND na Wiliam Mganga Ngereja.
WATANZANIA KAZI TUNAYO.... IMEANDIKWA NA MPIGANAJI
Comments
Post a Comment