BIBIANE
Ilikuwa
yapata saa nne usiku wakati Willy Gamba alipokuwa akielekea nyumbani kwa Col.
Rwivanga, akitokea Centre Christus. Walikuwa wamekubaliana na Col. Rwivanga kuonana baada tu ya
Willy kutoka kwa Mapadri. Wakati anakaribia kukata kona kuingia Barabara inayoingia
sehemu ya Kimihurura ili aelekee nyumbani kwa Col. Rwivanga alipitwa na gari
nyingine aina ya Landrover 110, lililokuwa likienda kasi sana na kama asingekuwa
makini katika uendeshaji wangeweza kumgonga maana pamoja na kuonyesha ishara ya taa kuwa anahitaji kuingia
kushoto lakini gari hilo lilipita kasi bila kujali ishara ya taa.
"Hawa
wanajeshi ndio sababu hupata ajali mara kwa mara, uendeshaji wao ni wa ovyo
sana", Willy alijisemea moyoni na kisha akakata kushoto kuelekea nyumbani
kwa Col. Rwivanga.
"Endesha
kwa tahadhali Felician, tungeweza kumgonga yule mtu ikaleta balaa hata kabla
hatujaanza kazi. Kazi yetu ni kummaliza Willy Gamba na wala si kugonga magari
ya watu ovyo", Xavier Nkubana alikaripia Felician.
Nkubana na
wenzake waliwasili jioni ile mjini Kigali kwa ndege ya serikali ya Tanzania ambayo
iliwasili na ujumbe wa Serikali ya Tanzania uliofika kuchunguza tukio la
kulipuliwa kwa ndege ya Tanzania iliyokuwa inamilikiwa na Kampuni ya ndege ya
Tanzaiar. Ndege hii iliwaleta maafisa kutoka idara ya usalama wa anga, mambo ya
nje, polisi na waandishi wa habari. Nkubana na wenzake walifanyiwa mpango na
kupanda ndege hii kama wafanyabiashara wa kinyarwanda waishio Tanzania walikuwa
wakirudi nyumbani Rwanda kuangalia hali ya nchi ilivyo kwa wakati huu ili kama
ikiwezekana waanzishe biashara tena kati ya Tanzania na Rwanda. Waliingia
Rwanda bila tatizo lolote na kupokelewa vizuri na viongozi wa serikali ya
Rwanda na kupelekwa kwenye Hoteli ya Des Mills Collines. Kwa vile walijulikana
kama wafanyabiashara, baada ya kufikishwa hotelini waliachwa ili waendelee na
mambo yao, na wale maofisa wa serikali ya Tanzania wakaanza kushugulikiwa na
wenzao kuhusu mambo ya hotelina mambo mengine ya kiusalama.
Baada ya
kuchukuwa vyumba na kuoga. Nkubana aliondoka na kuelekea nyumbani kwa Co.
Gatabazi na kuwaacha wenzake wakipumzika, kwani ratiba yao ya kazi ilikuwa
usiku ule ule. Ilikuwa yapata saa moja hivi Nkubana alipowasili nyumbani kwa
Col. Gatabazi aliyekuwa akimsubiri.
"Karibu
sana", Col. Gatabazi alimkumbatia Nkubana kwani walikuwa hawajaonana kwa
muda mrefu.
"Asante,
naona mambo mazuri", Nkubana alijibu.
"Mambo
mazuri gani haya! Mambo yatakuwa mazuri baada ya sisi wenyewe kuchukuwa
madaraka ya nchi hii. Kila siku nasikia uchungu moyoni kuona 'Inyenzi' inazidi
kujiimalisha hapa. Lazima mambo yafanyike haraka kabla hawajajizatiti sawasawa,
karibu ndani", Col. Gatabazi alijibu huku akiwa ameushikilia mkono wa
Nkubana kisha akamwongoza kuelekea sebuleni.
"Utakunywa
nini?", Col. Gatabazi alimuuliza.
"Nipe
chai kama ipo".
"Tena
na mimi sasa hivi nilikuwa nakunywa chai", Col. Gatabazi alijibu na kwenda
kuchukuwa chupa ya chai na vikombe viwili vya chai, wakakaa mezani pale
sebuleni.
"Karibu".
"Asante
sana". Nkubana alichukua kikombe chenye chai na kuanza kunywa.
"Ehee,
hamkupata tatizo lolote?".
"Wewe
unacheza na mipango ya JKS nini?, atakapokuwa Rais wa Tanzania na wewe hapa
mbona tutakula kuku mpaka tuchoke! Tumekuja kwa heshima zote na kupokelewa na
'Inyenzi', na kutupeleka mpaka hotelini. Wangeweza hata kutulipia hoteli lakini
sisi tumekataa maana tumekuja kama wafanyabiashara hivyo ni vizuri
kujitegemea", Nkubana alijibu.
"Vijana
wako katika hali nzuri?".
"Wako
na moto kama nini, maana wanataka kumaliza kazi usiku huuhuu, na baada ya hapa
tunaelekea Bukavu tukasaidie kupanga mapambano dhidi ya 'Inyenzi', JKS
ametueleza mipango yote nasi tumeafiki".
"Hiyo
safi, lakini kwanza mambo ya hapa. Huyu Willy Gamba ni mtu hatari kabisa.
Inabidi tumfanyie mkakati mzuri. Siyo mtu wa kawaida", Col. Gatabazi
alieleza lakini kabla hajajendelea Nkubana alimkata kauli.
"Yaani
huna maana sisi watu watano ambao ni sawa na jeshi zima la askari shupavu, bado
una wasiwasi? Hivi umesahau kuwa sisi ni makomandoo, tupe mipango tujuwe yuko
wapi, kazi ingine tuachie sisi wenyewe", Nkubana alijigamba.
"Imebidi
nikutahadharishe kwanza, msije mkamwendea kwa pupa. Ni lazima tupange mipango
mathubuti. Inabidi kwanza kueleza nyendo zake kutokana na upelelezi niliofanya
toka mambo yaliyotokea juzi usiku", Col. Gatabazi alijibu.
"Sawa
endele", Nkubana alijibu huku akionyesha kuwa Col. Gatabazi alikuwa
anazidi kupoteza muda kwani anaamini hakuna mtu. Hata awe wa uwezo wa aaina
gani asingeweza kutamba mbele ya kikosi chake.
Nkubana
alikuwa kati ya askari waliopatiwa mafunzo ya kijeshi na kijasusi kwa pamoja.
Alikuwa na cheo cha Meja Jeshini lakini aliingia hata katika kambi za RPF huko
Uganda na kuchukuwa habari na ndiye ambaye mara nyingi aliifanya RPF
isifanikiwe katika mashambulizi yake kwani yalijulikana mapema. Inasemekana
mauaji yote yaliyofanywa kwa watu na wanajeshi waliokuwa wakitoa habari kwa RPF
yalifanywa na yeye. Alikuwa jasiri na shupavu lakini uso wake kila siku
utadhani wa padri hata namna yake ya kusema akiwa na watu wa kawaida. Pia
inasemekana kuwa 'Akazu' walimchagua kufuatilia maofisa ambao baadaye waliwafundisha
Intarahamwe, na kuwapa amri kumi ili wazieneze kwa Wahutu. Mhutu yeyote ambaye
asingezifuata na kuzitekeleza basi auawe hapohapo.
Na hizi amri
kumi za Wahutu zilikuwa kama ifuatavyo.
1. Kila
Mhutu ajue kuwa mwanamke wa Kitutsi kokote aliko, yuko kwa manufaa ya watutsi.
Kwa hiyo mtu yeyote atakayeoa,
kufanya urafiki au kumwajiri mwanamke wa Kitutsi kama mfanyakazi wake au mkewe basi Mhutu huyo ni msaliti, lazima auawe.
2. Kila
Mhutu ajue kuwa ni mwanamke wa Kihutu tu anjayefaa kama mke, kama rafiki na
kama mfanyakazi wake ofisini.
3. Wanawake
wote wa Kihutu lazima wewe imara na wawahamasishe waume zao, kaka zao na watoto
wao wa kiume kumchukia Mtutsi.
4. Kila
Mhutu lazima ajue kuwa Mtutsi yeyote si mwaminifu katika biashara. Hivyo, Mhutu
anayefanya biashara na Mtutsi, anayewekeza fedha zake au za serikali katika
kampuni za Kitutsi, anayekopesha ama kukopa kwa Mtutsi, anayewasaidia
wafanyabiashara wa Kitutsi ni msaliti, anatakiwa kuuawa.
5. Kazi zote
za juu katika siasa, utawala, uchumi, jeshi na usalama lazima wapewe Wahutu.
6. Katika
sekta ya elimu (walimu, watoto wa shule na nguo), lazima wengi wawe Wahutu.
7. Jjeshi la
Rwanda liwe kwa Wahutu tu. Na mwanajeshi haruhusiwi kuona Mtutsi.
8. Wahutu
waache kuwaonea huruma Watutsi, unyama unyama tu dhidi ya Watutsi.
9. Wahutu
popote walipo duniani lazima wawe na umoja kwa kila njia na wajaribu kuzima
propaganda za Watutsi na kuungana katika kuwaangamiza Watutsi.
10.
Mapinduzi ya kijani ya mwaka 1959 na itikadi za Kihutu lazima zifundishwe kwa
kila Mhutu. Na Mhutu yeyote anayemwonea Mhutu mwenzake kwa kueneza itikadi hizi
basi huyo Mhutu auawe, maana ni msaliti.
Kwa kutumia
askari wa vikosi alivyovifundisha Nkubana alihakikisha kuwa amri hizi
zinatekelezwa na zinachochea chuki ya Wahutu dhidi ya Watutsi kama alivyoagizwa
na Akazu.
Huyu ndiye
Nkubana, mtu jasiri, aliyehitimu katika shule mbalimbali za kijeshi, kijasusi
na kikomandoo ulimwenguni, lakini mafunzo yake yote yalikuwa ya dhamira moja
tu, ya kuhakikisha kuwa utawala wa Kihutu uliokuwa madarakani unaendelea
kutawala milele na milele kwa njia moja tu kuhakikisha Watutsi wote wanafyekwa
ili wasiwepo tena duniani. Hivyo, kwake mtu yeyote aliyemuunga mkono Mtutsi
lazima afe na yeyote aliyesaidia Mhutu basi yeye Nkubana alimsaidia kwa lolote.
Hivyo ndivyo walivyoweza kuelewana na kundi la Jean kwani lilikuwa upande wa
Akazu. Na habari za Willy Gamba kuwa alikuwa anajaribu kuharibu mipango ya
Wahutu kurudi madarakani, zilimuudhi sana na kusikia hasira isiyo kifani dhidi
ya Willy Gamba.
"Lazima
usiku huu huu afe", Nkubana alijishitukia amesema kwa hasira hata Col.
Gatabazi aliyekuwa ameanza kueleza mipango akashituka. Akashtuka.
"Haya
sasa endelea, huyu mtu ameniudhi sanasana, tayari hukumu yake ya kifo
imeshapita".
Col.
Gatabazi ilibidi aanze upya kumpa mipango ya usiku ule kama walivyokuwa
wamepanga na Jean na JKS.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment