UCHU

NGUVU YA RUSHWA

Nkubana, huku damu zikimtoka, alikimbia moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Col. Gatabazi. Alipolisukuma lango la mbele alikuta likiwa wazi. Akaingia ndani, moja kwa moja kwenye mlango wa mbele ambao ulikuwa umefungwa. Aligonga kwa nguvu mpaka Col. Gatabazi aliyekuwa anaoga, alitoka haraka huku akiwa amejifunga taulo na bastola mkononi. "Nini", aliuliza kwa shauku baada ya kuona hali aliyokuwanayo Nkubana.

"Vaa tuondoke hapa, mambo yameharibika.

"Nini?", Col. Gatabazi aliuliza tena.

"Nakwambia vaa twende, mambo yameharibika", Nkubana alimjibu huku akielekea sebuleni, akafungua friji akatoa maji baridi na kunywa huku Col. Gatabazi akimwangalia kwa mshangao.

"Huyu mtu wako ni mchawi. Kawaua vijana wangu wote na sasa yuko na Bibiane. Kwa kuwa ilikuwa tumuue Bibiane, sasa atakuwa upande wa Willy Gamba. Hivyo, lazima tayari mambo yako yataelezwa, na Jeshi la RPF litakuwa hapa sasa hivi. Lililopo tuondoke hapa tufuate majeshi yetu Kihumba".

"Hebu nieleze vizuri imekuwaje, maana siamini kabisa mtu mmoja kufanya kazi kubwa namna hiyo, tena kwa watu wenye uwezo mkubwa kama wewe?", Col. Gatabazi aliuliza kwa hofu huku akielekea chumbani kujitayarisha kwa ajili ya kuondoka eneo hilo. Nkubana alimweleza kila jambo lilivyotokea kwa Bibiane na jinsi alivyopoteza vijana wake.


ITAENDELEA 0784296253

Comments

  1. ntajitahidi kusoma riwaya zote za Willy Gamba utakazoweka humu,hakika umenikumbusha mbali sana. R.I.P Musiba

    ReplyDelete

Post a Comment

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU