NGUVU YA
RUSHWA
Nkubana,
huku damu zikimtoka, alikimbia moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Col. Gatabazi.
Alipolisukuma lango la mbele alikuta likiwa wazi. Akaingia ndani, moja kwa moja
kwenye mlango wa mbele ambao ulikuwa umefungwa. Aligonga kwa nguvu mpaka Col.
Gatabazi aliyekuwa anaoga, alitoka haraka huku akiwa amejifunga taulo na
bastola mkononi. "Nini", aliuliza kwa shauku baada ya kuona hali
aliyokuwanayo Nkubana.
"Vaa
tuondoke hapa, mambo yameharibika.
"Nini?",
Col. Gatabazi aliuliza tena.
"Nakwambia
vaa twende, mambo yameharibika", Nkubana alimjibu huku akielekea sebuleni,
akafungua friji akatoa maji baridi na kunywa huku Col. Gatabazi akimwangalia
kwa mshangao.
"Huyu
mtu wako ni mchawi. Kawaua vijana wangu wote na sasa yuko na Bibiane. Kwa kuwa
ilikuwa tumuue Bibiane, sasa atakuwa upande wa Willy Gamba. Hivyo, lazima
tayari mambo yako yataelezwa, na Jeshi la RPF litakuwa hapa sasa hivi. Lililopo
tuondoke hapa tufuate majeshi yetu Kihumba".
"Hebu
nieleze vizuri imekuwaje, maana siamini kabisa mtu mmoja kufanya kazi kubwa
namna hiyo, tena kwa watu wenye uwezo mkubwa kama wewe?", Col. Gatabazi
aliuliza kwa hofu huku akielekea chumbani kujitayarisha kwa ajili ya kuondoka eneo hilo. Nkubana
alimweleza kila jambo lilivyotokea kwa Bibiane na jinsi alivyopoteza vijana wake.
ITAENDELEA
0784296253
ntajitahidi kusoma riwaya zote za Willy Gamba utakazoweka humu,hakika umenikumbusha mbali sana. R.I.P Musiba
ReplyDelete