UCHU



GISENYI

V

Mjini Kigali baada ya Willy Gamba na Bibiane kuondoka wakielekea mpakani mwa Zaire, Col. Rwivanga alikwenda moja kwa moja kuonana na Mkuu wa Majeshi mnamo saa mbili, akamweleza yote aliyoyapata kutoka kwa Willy kutokana na maelezo ya msichana mrembo Bibiane.

"Kamanda, hali ni mbaya, tusipofanya haraka tunaweza kuvamiwa," Col. Rwivanga alimuasa Mkuu wa Majeshi.

"Sasa tunafanyaje?" Mkuu wa Majeshi, Jenerali Bunyenyezi, alimuuliza Col. Rwivanga.

"Nafikiri mpigie simu Rais aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri na makamanda wa vikosi vyote haraka ili tuliangalie swala hili kwa undani zaidi, maana tukifanya mchezo hawa Interahamwe wanaweza kutuvamia, wamepania sana kufanya hivyo, wanaweza kutuvamia, silaha wanazo tena kali na za kisasa, mafunzo wanapewa na askari wa kukodi, maana wapiganaji wao hawana njia nyingine ila kupigana tu ili warudi. Wamekataza hata wakimbizi halali wanawake kwa watoto wasirudi Rwanda kwa hiari yao ili wawatumie katika uvamizi huu. Kamanda, hii ni hatari na ni hatari sana lazima uamuzi upatikane leo", Col. Rwivanga alishauri.

Jenerali Bunyenyezi alimpigia simu Mkuu wa nchi, nae aliposikia uzito wa swala lenyewe aliamua kuitisha mkutano saa sita na nusu ili watu wote wanaohusika waweze kuwepo maana swala hili lilikuwa na maana ya kuanzisha vita dhidi ya Interahamwe waliokuwa mpakani mwa Zaire na Rwanda.

Baada ya Col. Rwivanga kuona umuhimu wa mkutano huu aliwasiliana na Col. Tom Kabalisa, Kiongozi wa Banyamulenge, Baada tu ya kuwasiliana na Mkuu wa Majeshi kwa njia ya simu ya Satellite ambayo serikali ya Rwanda ilikuwa imewapa kurahisisha mawasiliano na kumweleza ajitayarishe kuja Kigali kwenye mkutano muhimu na kwamba angemtumia helikopta ya kumchukua awe Gisenyi saa nne na watu wasiozidi watatu wa ngazi za juu katika uongozi wao wanaoweza kufanya maamuzi. Kwa miezi mingi Col. Tom Kabalisa alikuwa anasubiri huo muda hivyo alifurahi sana kupata habari hizi.  

ITAENDELEA 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU