GISENYI
V
Mjini Kigali
baada ya Willy Gamba na Bibiane kuondoka wakielekea mpakani mwa Zaire, Col. Rwivanga
alikwenda moja kwa moja kuonana na Mkuu wa Majeshi mnamo saa mbili, akamweleza
yote aliyoyapata kutoka kwa Willy kutokana na maelezo ya msichana mrembo
Bibiane.
"Kamanda,
hali ni mbaya, tusipofanya haraka tunaweza kuvamiwa," Col. Rwivanga
alimuasa Mkuu wa Majeshi.
"Sasa
tunafanyaje?" Mkuu wa Majeshi, Jenerali Bunyenyezi, alimuuliza Col.
Rwivanga.
"Nafikiri
mpigie simu Rais aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri na makamanda wa vikosi
vyote haraka ili tuliangalie swala hili kwa undani zaidi, maana tukifanya
mchezo hawa Interahamwe wanaweza kutuvamia, wamepania sana kufanya hivyo,
wanaweza kutuvamia, silaha wanazo tena kali na za kisasa, mafunzo wanapewa na
askari wa kukodi, maana wapiganaji wao hawana njia nyingine ila kupigana tu ili
warudi. Wamekataza hata wakimbizi halali wanawake kwa watoto wasirudi Rwanda
kwa hiari yao ili wawatumie katika uvamizi huu. Kamanda, hii ni hatari na ni
hatari sana lazima uamuzi upatikane leo", Col. Rwivanga alishauri.
Jenerali
Bunyenyezi alimpigia simu Mkuu wa nchi, nae aliposikia uzito wa swala lenyewe
aliamua kuitisha mkutano saa sita na nusu ili watu wote wanaohusika waweze
kuwepo maana swala hili lilikuwa na maana ya kuanzisha vita dhidi ya
Interahamwe waliokuwa mpakani mwa Zaire na Rwanda.
Baada ya
Col. Rwivanga kuona umuhimu wa mkutano huu aliwasiliana na Col. Tom Kabalisa,
Kiongozi wa Banyamulenge, Baada tu ya kuwasiliana na Mkuu wa Majeshi kwa njia
ya simu ya Satellite ambayo serikali ya Rwanda ilikuwa imewapa kurahisisha
mawasiliano na kumweleza ajitayarishe kuja Kigali kwenye mkutano muhimu na
kwamba angemtumia helikopta ya kumchukua awe Gisenyi saa nne na watu wasiozidi
watatu wa ngazi za juu katika uongozi wao wanaoweza kufanya maamuzi. Kwa miezi
mingi Col. Tom Kabalisa alikuwa anasubiri huo muda hivyo alifurahi sana kupata
habari hizi.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment