GISENYI
VII
Mpinda
alipofika kwenye nyumba aliyokuwa amefikia, aliteremka haraka kutoka ndani ya gari na kuingia ndani
ya nyumba hii, akawagongea wenzake waliokuwa ndani ya vyumba, akiwataka kwenye mkutano
pale sebuleni.
Alifikiria na kuona kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa ameyajibu
maombi yake. Hii ilikuwa nafasi aliyoisubiri kwa muda mrefu sana. Na yeye
vilevile kama wenzake wa Rwanda aliona nafasi hii ilikuwa inazifaa pande zote
tatu zilizokuwa zinahusika kwenye harakati hizi za mapambano. Kati ya wote
waliokuwa katika sakata hilo, alijiona ndiye mwenye fursa ya kufaidika zaidi
ingawaje Serikali ya Rwanda ndio ingefaidika zaidi kwa kuhakikisha kuwa haina
mgogoro au wasiwasi wa kushambuliwa na Wahutu wenye msimamo mkali chini ya
wanamgambo wa Intarahamwe na Banyamulenge ambao nao wangefaidika kwa kutobuguziwa
tena na Serikali ya Zaire, na wangeendelea na maisha yao raha mstarehe.
Makamanda hawa walipokusanyika pale sebuleni Mpinda aliwaeleza kila kitu jinsi mambo
yalivyokuwa wamejipa.
"Tunachotakiwa
kufanya ni kukishawishi na kukikahakikishia kikao cha Serikali ya Rwanda na
viongozi wa Banyamulenge kuwa tutakapoanzisha vita hii ni kweli uwezo
wa kushinda tunao?. Pande zote zimekubali kuwa sababu tunayo na nia tunayo,
swala hapa ni uwezo, wakiridhika kuwa uwezo upo, basi mambo tayari", Mpanda aliwaeleza
wenzake.
"Mkuu,
wala tusipoteze muda wa kufikiri, sisi tumekuwa hapa tukijaribu kuwashawishi
siku zote, tusingekuwa na uhakika na uwezo wetu kivita tusingekuja kuomba watuunge
mkono, uwezo tunao. Nenda kawaeleze kwa uhakika kama watatoa msaada kidogo tu, basi
nchi yetu tumeikomboa kutoka kwenye mikono ya utawala wa Kidikteta na kifashisti",
Col. Mkengeri, mmoja wa makamanda wa wapinzani wa serikali ya Zaire alijibu.
Wenzake wote walitingisha vichwa kukubali maneno yake.
"Azimio,
tunakwenda wote kushiriki kikao hicho", Mpinda alijibu.
ITAENDELEA 0784296253
Comments
Post a Comment