BIBIANE
III
Baada ya
Col. Gatabazi kumwelezea mipango yote kama walivyokuwa wamepanga na Jean,
Nkubana aliomba gari ili akawachukuwe wenzake na kuanza kazi ya kumsaka Willy.
Col. Gatabazi aliwapa gari aina ya Landrover 110 ya Jeshi ambayo hutumika kwa
ajili ya wageni wa Serikali. Kwa sababu ya kazi maalum iliyokuwa ikiwakabili,
kutokana na unyeti wa kazi hiyo, Col. Gatabazi aliwaachia gari hilo waendeshe
wenyewe. Nkubana alikwenda, moja kwa moja akawaamsha wenzake, baada ya mazoezi
makali, walioga na kupata chakula pale hotelini, kisha wakaanza kazi ya
kupeleleza habari za Willy Gamba.
Kutokana na maelezo waliyokuwa wamepewa na
Col. Gatabazi, mara moja walijua kuwa Willy yuko Meridien Hoteli, mara baada ya
kupata namba ya chumba chake cha kulala waliamua kwanza wakafanye shughuli
nyingine ili wasubiri wakati mzuri wa kupambana na Willy Gamba ambaye pia
walikuwa wakimhofia kwa kiasi fulani.
Baada ya
kupanga vyema mipango yao ya kuhakikisha wanamuua Willy Gamba usiku huo.
Walirudi hotelini wakapata kinywaji kidogo kwa ajili ya kujiweka safi.
Ilipotimia saa nne hivi usiku wakaamua kwenda kwa wote kwa Col. Gatabazi kwa
ajili ya mikakati ya ziada. Ni wakati huo walipokuwa wakielekea kwa Col.
Gatabazi ndipo walipokaribia kuligonga gari la Willy Gamba bila wao kujuwa kuwa
ndiye mtu anayepanga kumuangamiza usiku huo.
Kwa kasi
ileile, gari hilo liliingia nyumbani kwa Col. Gatabazi, aliyekuwa nje ya nyumba
yake akitafakari jinsi Willy alivyokuwa akiwanyima usingizi. alipowaona
akawapokea kwa tabasamu kisha akawaongoza hadi kwenye sebule ya nyumba yake.
"Vipi
mmepata habari zozote kuhusu Willy Gamba?", Col. Gatabazi aliwauliza baada
tu ya kuketi kwenye makochi.
"Habari
za Willy zote tunazo, huyo tutaanza biashara yake, atakuwa marehemu baada ya
saa sita usiku", Nkubana alijibu kwa majidai na kujiamini.
"Nasema
tena lazima muwe makini sana, huyo mtu ni hatari sana, na amri ni kwamba mara
hii isishindikane, akionekana tu ua mara moja", Col. Gatabazi alisisitiza.
"Col.
tafadhali usitutishe na huyo mtu wako, atakuwa hatari gari mbele yetu! Vipi una
matatizo nini Col. Gatabazi?", Nkubana alijibu kwa mshangao huku vijana
wake wote wanne wakicheka kwa dharau.
"Acha
wasiwasi mzee, kazi ya Willy hesabu imeisha, amezoea kucheza na wafanzi leo
atakutana na waalimu wa kazi", Felician alimhakikishia Col. Gatabazi.
"Ehe,
Bibiane umemtaarifu kuwa tutakwenda nyumbani kwake leo?", Nkubana
aliuliza.
"Bibiane
ana taarifa zenu, na wakati ndio huu, twendeni basi mara moja, hiyo gari acheni
hapa maana anakaa ileile nyumba yake", Col. Gatabazi alijibu.
"Ahaa,
kweli gari tuache tu hapa, tutalipitia wakati wa kwenda mjini", Felician
alijibu.
"Haya
twendeni anatusubiri, lakini mjuwe kutokana na mipango ilivyo mimi nitawaacha
pale nyinyi mtaendelea nae", Col. Gatabazi aliwaelza.
"Sawa
hamna tabu", wote walijibu kwa pamoja na kuondoka kuelekea kwa Bibiane.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment