KADA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), BW. NJOWOKA NJOWOKA (WA TATU KULIA) AKIWA NA MBUNGE WA MBINGA MAGHARIBI, KAPTENI MSTAAFU JOHN KOMBA (KULIA KWAKE) WAKIANGALIA MASHIMO YA VYOO VINAVYOJENGWA KWA UFADHILI WAKE KATIKA SHULE YA MSINGI MBAMBA-BAY, WILAYA YA NYASA, MKOANI RUVUMA.
VYOO VYA ZAMANI AMBAVYO WANAFUNZI WA SHULE HIYO WALIVITUMIA PAMOJA NA WAALIMU WAO KWA AJILI YA KUJISAIDIA. KUTOKANA NA HALI HIYO NJOWOKA AMEFADHILI UJENZI WA VYOO VYA KISASA.
HEKAYA ZA ABUNUWASI
HEKAYA ZA ABUNUWASI ni kitabu cha hadithi za kusisimua, zinazofurahisha sana kutokana na umahili wa watunzi wa vitabu vya kale. Kutokana na utamu wa hadithi za ABUNUWASI, Blog ya MPIGANAJI itawaletea hadithi hizo ili kuwachangamsha akili............... KISA CHA ABUNUWASI NA MFALME SIKU moja alfajiri, wakati wananchi wa mji wenye wakazi wengi walipokwenda kuchota maji mtoni, walishangazwa kuuona mkono wa mtu ukiwa katikati ya mto. Mkono huo wa ajabu ulikuwa umenyoosha vidole viwili juu, kuonyesha alama ya mbili. Wananchi walistushwa sana na kitendo hicho, wakaogopa hata kuchota maji mtoni, kwani hawakuwahi kuona tukio la kuogopesha kama lile. Wengine waliamini kuwa huo ulikuwa mwili wa mtu aliyetupwa mtoni. Lakini ishara iliyoonyeshwa na mkono huo iliwafanya wananchi waamini kuwa huo ulikuwa mkono wa ajabu. Katika kiza kinene kilichozunguka ndani ya vichwa vya wananchi, habari zikamfikia Mfalme wao, naye akafika haraka eneo la tukio. Mfalme wa nchi hiyo baada ya kujiridhisha k
Comments
Post a Comment