MTEJA WA BENKI AFRIKA TANZANIA (BOA) ASHINDA GARI LA KISASA



Meneja Uendeshaji Biashara wa Benki ya Afrika Tanzania (BOA), Bw. Wasia Mushi (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu droo ya mwisho ya Pormosheni ya ya Deposit and Win iliyoanza Oktoba mwaka jana. Kulia ni Meneja wa Benki hiyo Tawi la Kijitonyama, Bw. Emanuel Moya na Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Bw. Mirisho Millao.

.................................................................................................................................
DAR ES SALAAM LEO
Mteja wa Benki ya Afrika Tanzania (BANK OF AFRIKA TANZANIA BOA), Bw. Ismail Said Mohamed, kutoka Tawi la Benki hiyo Mtwara, ametangazwa leo kuwa mshindi wa gari mpya aina ya TOYOTA BREVIS, wakati wa droo ya mwisho ya Promosheni ya Deposit and Win iliyoanza Oktoba mwaka jana.

Wakati Bw. Mohamaed akishinda gari hilo mpya kabisa, mteja menzake Thureiya Zabron Mgamba naye ameibuka mshindi wa pili katika Promosheni hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya tawi la Benki hiyo Kijitonyama, Jijini Dar es Salaam baada ya kushinda Pikipiki mpya aina ya TOYO.

Katika mchezo huo wa Bahati Nasibu uliosimamiwa na Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha nchini, Bw. Mrisho Millao, washindi wengine watatu pia walishinda zawadi mbalimbali zikiwemo Tshirt, Simu za kisasa na vocha za manunuzi.

Awali akizungumza na waanndishi wa habari, kabla ya Promosheni hiyo, Meneja Uendeshaji Biashara wa BOA, Bw. Wasia Mushi, amesema, lengo la Poromosheni hiyo ni kuongeza hamasa kwa watanzania ili wakumbuke kujiwekea akiba, huku akisisitiza kuwa kujiwekea akiba ndio utamaduni halisi wa kuelekea katika mafanikio.

Bw. Mushi amesema wakati wote wa Promosheni hiyo iliyofanyika nchi nzima, wateja zaidi ya 2000 wa Benki hiyo walishiriki na kushinda zawadi mbalimbali. “Tumefurahishwa sana jinsi Promosheni hii ilivyopokelewa na wateja wetu, tumeongeza idadi ya wateja pia kukuza amana kwa wateja wetu”, anasema Bw. Wasia.

Amesema pamoja na Promosheni hiyo kufikia tamati, Benki ya Afrika bado inaendelea kuwahimiza wateja kuweka akiba kwa ajili ya manufaa ya jamii na kuahidi kuwa wamejipanga kutoa huduma za kisasa kwa wateja.

Bw. Wasia amesema Benki ya Afrika Tanzania imejiikuwa ikijimalisha kwa kuwa na mtandao wa matawi 20 nchi nzima, ambapo matawi kumi yako Jijini Dar es Salaam, wakati matawi mengine yakiwa Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Morogoro, Mtibwa, Kahama, Mbeya, Mtwara na Tunduma.


Meneja Uendeshaji Biashara wa Benki ya Afrika Tanzania (BOA), Bw. Wasia Mushi akiwaonyesha waandishi wa habari gari mpya aina ya Toyota BREVIS lililotolewa na Benki hiyo kwa ajili ya Droo ya mwisho ya Promosheni ya Deposit and Win iliyoanza Oktoba mwaka jana. Wengine ni Meneja wa Benki hiyo Tawi la Kijitonyama, Bw. Emanuel Moya (kulia) na Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Bw. Mirisho Millao. 
Meneja Uendeshaji Biashara wa Benki ya Afrika Tanzania (BOA), Bw. Wasia Mushi akionyesha gari mpya aina ya Toyota BREVIS lililotolewa na Benki hiyo kwa ajili ya Droo ya mwisho ya Promosheni ya Deposit and Win iliyoanza Oktoba mwaka jana. Wengine ni Meneja wa Benki hiyo Tawi la Kijitonyama, Bw. Emanuel Moya (kulia) na Afisa kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Bw. Mirisho Millao. 
Gari aina ya Toyota Brevis lililotolewa na Benki hiyo kwa ajili ya Droo ya mwisho ya Promosheni ya Deposit and Win iliyoanza Oktoba mwaka jana.
Wapigapicha kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini.wakati wa Droo ya Promosheni ya BOA.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU