Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya
Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhani Dau akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa kuwapata
wanafunzi wa michezo (Sports Academy)
kitakachoanzishwa eneo la Kigamboni Dar es Salaam kwa
ushirikiano wa NSSF na Klabu ya Real Madrid ya
Hispania. Kushoto ni Meneja Usalama wa NSSF, Ramadhani Nassib,
Mtaalamu wa Uongozi na Menejimenti ya michezo, Henry Tandau na
Afisa Uwekezaji Mkuu wa NSSF, Tajudin Kamugisha (kulia).
...........................................................................................................
Hivi karibuni Shirika la Taifa la
Hifadhi ya Jamii (NSSF) lilisaini mkataba na timu ya Real Madrid ya Hispania
kuanzisha na kuendesha kituo cha michezo (NSSF- REAL MADRID Sports Academy) kwa
lengo la kuibua, kuendeleza na kukuza vipaji vyaa mpira wa miguu. Kituo hiki kitajengwa
katika eneo la Mwasonga Kigamboni, Dar es Salaam na wataalamu kutoka Real
Madrid watatoa mafunzo kwa vijana wa umri wa miaka13 na 19 ili
kukuza mchezo wa soka, kupata wachezaji bora wanaouzika nje na ndani
ya nchi pamoja na kulipatia mapato shirika na nchi kwa ujumla.
Akizungumza na Waandishi Habari,
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt. Ramadhani K. Dau alisema mradi huo utakuwa sehemu
ya uwekezaji wa shirika hilo ulioanza baada ya kusaini mkataba. ambapo
NSSF imeanza utaratibu wa kuwabaini vijana walengwa ambapo utafutaji wa vipaji
vya mpira wa miguu utaanzia mkoa wa Dar es Salaam kwa vijana wenye umri wa
chini ya miaka 14. Utafutaji wa vipaji utafanyika kila wilaya kwa Wilaya za
mkoa wa Dar es salaam na utafanyika kwenye viwanja vya Karume.
Dkt. Dau amesema zoezi hilo litakuwa
linafanyika kati ya saa moja asubuhi hadi saa 9 alasiri kwa tarehe
zilizoainishwa. Amesema andikishaji washiriki utakuwa unafanyika siku za
mwisho wa wiki ili kutoathiri wanafunzi watakaopenda kushiriki na utaanza rasmi
Februari 14 na 15, 22 na 23 mwaka huu na kufuatiwa na michezo ya
majaribio Februari 28 na Machi moja, 2015 kwa wilaya zote za Dar es
salaam, ambapo kituo kitakuwa viwanja vya Karume.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF amesema, zoezi
la uandikishaji halitafanywa kwa gharama na uandikishaji wa washiriki
utafanyika kwa kujaza fomu maalum na kupewa namba ya ushiriki na kila mshiriki
atapata fursa ya kucheza katika awamu mbili za dakika 30, kuanzia washiriki
watatakiwa kuja na vifaa vyao vya michezo.
Amesema Vijana 500 kati watakaofanyiwa
majaribio wataingia katika awamu ya pili ya majaribio na watadahiliwa na
wataalamu kutoka Klabu ya Real Madrid na hatimaye kupatikana vijana 30 ambao
ndio wataingia katika shule maalum ya mafunzo kwa awamu ya kwanza.
Dkt. Dau amebainisha kuwa wakati wa
uandikishwaji washiriki watatakiwa kuja na wazazi au walezi wao wakiwa na
vitambulisho vyao, na kijana husika awe na Cheti halisi cha kuzaliwa na
kopi yake pamoja na picha mbili za pasport za rangi ya blue. Muda wa uandikishaji
na majaribio unaweza kuongezwa kulinagana na mahitaji.
Shirika la NSSF linatoa wito kwa
vijana kujitokeza kwani ni fursa kwao ya kuweza kujiendeleza kimichezo na
kujiajiri katika tasnia hiyo.
Comments
Post a Comment