UCHU



KASHESHE

VI

Ilikuwa saa nne na nusu usiku, wakati Jean na kundi lake walipoondoka Kibumba kuelekea Goma.

"Hakika nimeridhika na ari ya wanajeshi wetu na uwezo mkubwa wa vikosi vyetu, pia nimefurahishwa sana na aina ya silaha tulizonazo, hii inaonyesha ni jinsi gani tumedhamilia kufanya kweli", Jean alisema kwa kujiamini.

"Nilikwambia toka mwanzo kuwa ukifika na kuona lazima utaamua tuingie vitani, kwani hakuna sababu wala haja ya kusubiri, vita vianze moja kwa moja, tuchukue madaraka", Col. Gatabazi alitamba huku Jean akitingisha kichwa kukubaliana nae.

"Twendeni Goma tukafanye maamuzi. Sijui kwa upande wa wenzangu, lakini mimi nafikiri tuanze mashambulizi alfajiri na mapema ila kwanza tukamate vikosi vya hapa Gisenyi kabla ya jua kuchomoza, maana adui hajui nguvu zetu, sisi nguvu yake tunaijua", Jean alishauri, wote kwa pamoja wakakubaliana.

"Mimi niko tayari wakati wowote, hata sasa vijana wangu wako tayari, uamuzi wenu tu ndio unasubiliwa", Col. Gatabazi alijibu.

"Haya twendeni Goma tukafanye uamuzi mara moja", Jean alijibu wakaondoka haraka kuelekea Goma.

ITAENDELEA 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU