XII
"Saa
ngapi sasa?" Bibiane alimwuliza Willy Gamba.
"Imefika
saa sita na nusu sasa", Willy aliMjibu.
Walikuwa
tayari wana saa moja ndani ya kambi hii ya kijeshi na bado walikuwa hawajapata
tatizo lolote. Sasa ndio walikuwa wanaanza kutega mabomu kwenye bweni la mwisho
ili baada ya hapo kama itawezekana watafute namna ya kutoka nje, kwani mabomu
waliyokuwa wameyatega na kuyaprogramu kwa saa ya Willy ili kuyalipuwa lazima wawe mbali, maana yalikuwa na uwezo wa kuharibu kambi nzima na vitu vyote
vilivyomo kama yangefanya kazi kama ilivyotarajiwa. Wakati wanafikiri hivi,
ghafla taa za kiwanja cha ndege zikawashwa.
"Aha,
kumbe ule ni uwanja wa ndege!" Willy alinong'ona.
"Ndio,
unafikiri zile ndege za kijeshi zinaruka kutokea wapi!", Bibiane ambaye
naye hapo awali alikuwa hajui uwanja ulikuwa wapi, alijibu.
"Kwanini wanawashwa taa wakati huu?", Willy alijiuliza.
Wakiwa
wameduwazwa na kitendo hiki na wakiwa sasa wameondoka kwenye ukuta wa bweni la
mwisho na kujibanza kwenye kivuli cha lori kubwa la jeshi lililokuwa limeegeshwa pale,
Bibiane alijibu. "Huenda ndege za kivita zinatolewa ili zikashambulie
mahali ama ndege ya Jean inataka kutua".
"Nafikiri
hilo la pili ni sawa. Hii itakuwa raha sana mimi kukutana uso kwa uso na huyu
bwana yako", Willy alikejeli Bibiane akafadhaika.
"Si
bwana yangu tena, bwana yangu ni wewe Willy, maana wewe ndiyo uko na mimi sasa, sema, fanya kila unachotaka nifanye", Bibiane alijibu kwa sauti ya mahaba.
Willy alimwangalia, kisha akamshika na kumbusu.
Mara
wakasikia king'ola na askari wakatoka na kuanza kuelekea kwenye kiwanja cha
ndege.
"Hapa
kuna hatari, nafikiri wametushitukia", Willy alisema huku ile kengere yake
ya hadhari ikilia kichwani mwake. Kisha akaendelea. "Kinachotokea hapa ni
sisi kutoka ndani ya kambi hii. Wataanza kutusaka sasa hivi".
Mara tena
wakasikia mwungurumo wa ndege na magari sita aina ya Landrover ya wazi yakiwa
yamebeba askari yakielekea karibu na uwanja, yalipokaribia yakasimama. Kisha,
yakafika magari mengine mawili aina ya Landcruiser GX nayo yakasimama pale
vilevile kusubiri ile ndege itue. Pale kwenye uwanja mkubwa, vikosi vya
askari vilizidi kujipanga kwa ajili ya mapokezi.
Ile ndege ilipotua watu wanne walitoka ndani ya Landcuiser zilizokuwa zimesimama kando na kusogea karibu ili kuilaki ile
ndege. Wakiwa bado wamefichwa na kivuli cha lile Lori walitumia viona mbali
vyao na kuwaangalia kwa makini wale watu waliotoka kwenye yale magari.
"Yule
aliyetangulia ni Col. Marcel Bazimaziki, huyu ndiye kamanda mkuu wa majeshi
yote ya Akazu. huyo wa kushoto ni Kapten Nkubana aliyekutoroka Kigali, ndiye
aliyetumwa kuniua, kumbe naye keshafika huku. Wa kulia ni kamanda Morris huyu
ni mkuu wa vikosi vya kukodiwa ambavyo vinafundisha majeshi ya Akazu. Huyu wa
nyuma simfahamu".
Ndege
ilisimama na milango ikafunguliwa na watu wakaanza kutoka. Jean ndiye alikuwa
wa kwanza kutoka ndani ya ndege hii.
"Aha
huyu ndiye Jean nafikiri?", Willy aliuliza.
"Bila
shaka huyo ndiye Jean, ambaye ndiye mzizi wa fitina katika Rwanda. na yule
anayemfuatia ni Anatoile Kabuga, huyo ndiye kiongozi wa Akazu, anayefuata ni
Jenerali Kasongo, kamanda wa majeshi ya Rais wa Zaire, rafiki mkubwa wa Jean,
anayetokea sasa pale mlangoni ni Col. Gatabazi na huyo anayetokea mwisho
simfahamu, maana sijawahi kumuona", Bibiane alieleza.
"Asante,
sijui bila wewe ingekuwaje, umefanya kazi yangu iwe rahisi kiasi fulani".
"Ni
kweli, lakini ungetumia njia nyingine, wewe si wa kushindwa jambo".
Baada ya
kutoka ndani ya ndege, kundi la Jean liliingia ndani ya zile Landcruiser
wakaondoka huku wakisindikizwa askari kwa ulinzi mkali.
"Unadhani
watakuwa wanaelekea wapi sasa?", Willy alimuuliza Bibiane.
"Sijui,
nilitegemea huenda wanataka kuzungumza na vikosi vilivyofanya gwaride pale
uwanjani, lakini wameondoka moja kwa moja kuelekea upande ambao ndiko kuna
lango kuu. Huenda wanakwenda kupumzika kwa kamanda Morris, nyumba na ofisi ya
kamanda Morris iko juu ya hicho kilima, huwezi kuona ukiwa hapa kwa vile
kumefichika kwa miti", Bibiane alieleza.
Kati ya
magari yaliyobeba askari moja halikuendelea na msafara isipokuwa lilielekea
kwenye gwaride. Gari hilo lilipofika hapo lilisimama na watu waliotoka ndani
walikuwa Nkubana na askari wengine watano. Kisha Nkubana akaanza kuhutubia hilo
gwarinde na kikosi kimoja wapo kikapiga hatua moja mbele na vingine
vikatawanyika. Willy na Bibiane hawakuelewa nini kilikuwa kinaendelea.
"Lililopo
ni sisi kuondoka hapa kambini haraka iwezekanavyo. Vinginevyo tutakamatwa hata
kabla hatujamaliza kazi iliyotuleta", Willy alieleza.
"Mimi
bila kummaliza huyu Jean siendi kokote ng'o", Bibiane alijibu kwa hasira.
"Lazima
ufahamu kuwa hatuwezi kukabiliana na watu wote hawa, lazima kutumia akili ya
ziada, wewe unajua katika kazi yetu hii swala ni kuendelea kuishi; lazima
uhakikishe unajilinda ili ubaki salama. Hapa tukitaka kuanza mapambano ni sawa
na kujinyonga sisi wenyewe. Pili ili tuweze kulipua mabomu tuliyotega ni lazima
tutoke nje kabisa ya eneo hili, la sivyo sisi pia tutakuwa tumejiteketeza
pamoja na adui", Willy alimuasa Bibiane kisha wakaona wale askari wa
kikosi wanakabidhiwa silaha na kuelekea kwenye seng'enge ya ua wa kambi.
"Ehe,
umeona kazi hiyo, hawa jamaa wanategemea tutakuja hapa, lakini hawajui kama
tumeingia ndani na kazi imefanyika", Willy alieleza.
"Lakini
wakifika pale tulipoingilia lazima watajuwa tuko ndani", Bibiane alijibu.
"Ndio
sababu nikasema tutafute njia tutoke humu ndani", Willy alisisitiza.
Wakati wote
Willy alikuwa akipanga mbinu za kuweza kutoka ndani ya kambi hii wakiwa salama.
"Hebu
nifuate tuangalie hali ikoje upande wa lango kuu", Willy alimwambia
Bibiane.
"Kule
hatuwezi kupita, afadhari tuwahi palepale mahali tulipotumia mwanzo", Bibiane
alisema na Willy akamuunga mkono na kuona alikuwa na mawazo sahihi hivyo,
haraka haraka wakaelekea sehemu waliyokuwa wameingilia, huku askari wa doria
wakizidi kujipanga na kupewa silaha ili kuzidi kujipanga kando ya ua huu wa
seng'enge wakiwa tayari kulinda kambi yao. Ile tembetembea ya hawa askari kiasi
fulani iliwasaidia sana akina Willy na Bibiane kutobainika mapema kwani
walikuwa wamevaa mavazi ya kijeshi kama wale askari. Nkubana na watu wake
waliweka ulinzi mkali upande la lango kuu wakiamini kuwa Willy angeweza
kujaribu kuingia pale kambini kwa kutumia lango kuu.
Hakuna
askari wala kiongozi katka kikosi chicho aliyefikiri kuwa adui wangeweza
kupitia sehemu nyingine yoyote kwani waliamini kwamba hakuna kitu ambacho
kingeweza kupita ua ulioizunguka kambi hii. Hivyo, hata hawakuweka askari
kuzunguka ua ilikuwa ni kwa hadhari tu. Kumbe kitu ambacho hawakujua ni kwamba
teknolojia yotote inaweza kushindwa na teknolojia nyingine yenye maarifa ya juu
zaidi. Willy alikuwa ndani na tayari alikuwa ametega mabomu kila upande.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment