Wachezaji wa
Mwananchi Communication, Iman Makongoro (kulia) na Luth Liana wakiutamani mpira
unaolindwa na Jesca Claud wa Tumaini
Media, wakati mchezo wa awali wa netiboli wa NSSF MEDIA CUP 2015 kwenye viwanja vya TCC Chang’ombe Dar es
Salaam. Tumaini Media walishinda 14 -12.
Luth Liana
(kulia) wa Mwananchi Communication na Jesca Claud wa Tumaini Media wakichuana
vikali kuwania mpira wakati wa mchezo wa awali wa netiboli wa NSSF Media Cup
2015, uliochezwa kwenye viwanja vya TCC Chang’ombe. Tumaini
Media walishinda 14-12.
Kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam, wachezaji wa netiboli walilazimika kuogelea kwenye madimbwi ya maji wakati wakiziwakilisha timu zao kusaka kombe la NSSF Media Cup 2015.
Lilian Timbuka wa Mwananchi akionyesha ishara ya kuomba ruhusa ya mwamuzi ili aweze kurusha mpira huku wachezaji wenzake wakimsubiri wakati wa mchezo wa awali wa netiboli kuwania kombe la NSSF Media Cup 2015
Lilian Timbuka wa Mwananchi Communication akiwa hoi uwanjani haamini macho yake baada ya timu yake kubugizwa na Tumaini Media mabao 14 -12
Iman Makongoro wa Mwananchi akijiandaa kupokea mpira kutoka kwa Lilian Timbuka huku mchezaji wa Tumain Media Rose Michael akiwaangalia kwa makini.
Comments
Post a Comment