UCHU



KASHESHE

XVIII

Wakati huo Jean alikuwa ameanza kumvua nguo Bibiane ili atimize ahadi yake kama alivyoahidi kuwa atafanya nae mapenzi kabla ya kumuua, wakati akikaribia kutimiza ahadi yake, ghafla mlipuko mkubwa ulitokea eneo hilo na kuleta hofu, palepale nyumba ile ikasambaratika vipande. Bahati nzuri nyumba hii ilikuwa imetengenezwa kwa mbao tupu ili likitokea tatizo kama hili Kamanda Morris asihatarishe maisha yake.

Kwa vile Bibiane alikuwa akiutegemea mlipuko kama huo, ulipotokea tu hakuzirai kama wengine. Alizitupa mbao zilizomwangukia mwilini mwake, akainuka na kuanza kumsaka Willy ambaye wakati huo alikuwa amefungwa kwenye kiti pale ukumbini. Kumbe mlipuko ulipotokea kile kiti kilirushwa pamoja na Willy Gamba mpaka nje kwenye bustani. Bibiane aliangalia huku na huko kwa tahadhari kubwa, maana watu wote walikuwa wamelala chini kwa hofu. Vilio vilisikika eneo lote la kambi hii mara akamuona Willy Gamba na kiti chake akiwa nusu amezirai.

Milipuko ile iliendelea kuleta hofu na kusababisha mwanga mkubwa katika eneo lote. Milio na mwanga ilionekana na kusikika mpaka Goma, Gisenyi na sehemu nyingine kwani sasa mizinga na makombora nayo nayo yalianza kulipuka bila mpangilio na kusababisha Jean na wenzake kupatwa na taharuki. Bibiane alitoa kisu chake kidogo alichokuwa amekifika kwenye nywele zake, akiwa tayari kabisa kummaliza Jean. Na kwa kutumia hiki kisu alifanikiwa kuzikata kamba alizokuwa amefungwa Willy Gamba kisha akamtingisha hadi Willy akapata fahamu. Baada ya Willy kuzinduka Bibiane akamshika mkono. Willy alisimama wakakimbia kuelekea sehemu ile ya Magharibi ya kambi mahali ambapo kulikuwa na mstu mkubwa.

Walipokimbia kama mita hamsini hivi Bibiane alitoa bomu la kurusha kwa mkono akalitupa kwenye ile nyuma kisha wakajitupa chini. Bomu hilo liliporipuka likasambaratisha eneo hilo halikubakiza mtu wala kitu kilichokuwa ndani ya nyumba hii au mita thelathini kuzunguka nyumba hii. Wakati wanaelekea kwenye ule mstu mabomu, mizinga na makombora yaliyokuwa ndani ya maghala makubwa ya kuhifadhia silaha yaliendelea kuripuka yenyewe.

"Kazi ipo Willy, wamelikoroga acha walinywe sasa", Bibiane alisema kwa kebehi.

"Kazi yenyewe si kidogo, wamelala matajiri wataamka masikini", Willy alijibu wakiwa wemeingia kwenye msitu.

"Naona sasa tumechoka, kazi hii inatosha kabisa kwa siku moja ya leo", Willy alieleza wakiwa wametokeza kwenye sehemu ya majani mazuri chini ya mbaramwezi. "Hapa panafaa kupuzika,  au vipi", Willy aliuliza.

"Hapa tumetafutiwa na Mwenyezi Mungu ili tupumzike baada ya hii kasheshe. Nilikuwa natamani ufike muda nipate mahali ambapo dunia itakuwa mimi na wewe tu. Na mahali hapo ni hapa, yaani mimi, wewe, mbaramwezi, nyota, malaika na Mungu", Bibiane alieleza.

Willy alivua gwanda lake la juu akatandika chini kwenye majani, Bibiane akavua pia na kusema. "Hili tutajifunika".

Willy akamwinua na kumbeba mikononi kisha akambusu na kumlaza juu ya gwanda lake.

ITAENDELEA 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU