SURA YA KUMI
NA MOJA
KAMPALA
JKS aliamka
mapema asubuhi huku roho yake ikiwa na furaha nyingi sana. Sasa hivi alikuwa
akielekea benki kwa ajili ya kuchukua pesa zake. Hisia za urais wa Tanzania
zilimjia katika mawazo yake, akatamani kuwa kiongozi wa Tanzania ili atimize ndoto
yake ya kuwa mheshimiwa rais wa Tanzania.
Baada ya
kustafutahi kwa chai nzito, alipiga simu kwenye benki yake hapo Geneva na kuuliza mahali ilipo. Baada
ya kupata maelekezo sehemu na mtaa ambao benki ipo, alipiga simu mapokezi na kumuomba mhudumu amletee
teksi saa tatu kamili ili impeleke benki.
Baada ya kujiweka sawa, alitelemka
chini taratibu ilikuwa majira ya saa tatu kamili, akiwa amebeba mkoba wake wa ngozi ya mamba mkononi aliokuwa amepewa kama zawadi na rafiki yake Jean.
Alipofika
chini alikuta teksi inamsubiri mbele ya hoteli. Alifungua mlango wa nyuma kama VIP akaingia, akampa dereva anuani ya benki, baada ya kuthibitisha ni eneo gari
dereva aliondoa gari huku mawazo ya JKS yakiwa juu ya baraza lake la mawaziri
baada ya kuukwaa urais.
Jean alikuwa
amempa jina la meneja wa benki na kumweleza kuwa akifika benki amwone meneja
huyo. Alipofika benki alitelemka na kumwambia mwenye teksi amsubiri akaingia
ndani ya benki na kuelekea mapokezi. alimwonyesha yule msichana wa mapokezi jina
la meneja. Asubuhi ile meneja alikuwa bado hana watu wengi, hivyo akamkaribisha vizuri
sana.
"Karibu
Mheshimiwa, nikusaidie nini?", meneja wa benki aliuliza JKS baada ya kuingia ofisini kwake.
"Asante",
JKS alijibu na kutoa bahasha yenye maelezo yake yote. Meneja aliipokea kwa
tabasmu na kuifungua bahasha na kuanza kusoma. Alivuta Kompyuta yake na kuanza
kushughulika. Meneja, akiwa anatabasamu tena alimgeukia JKS na kumweleza,
"Samahani, hii akaunti imefungwa jana na aliyeifunga ametoa pesa zote na
kusema mtu yeyote akifika hapa kuuliza juu ya akaunti mwenye kitambulisho namba
hii, aelezwe kuwa akaunti hiyo imefungwa maana mkataba umeisha. Samahani sana
mheshimiwa, nina wateja wengine wananisubiri".
JKS alichanganyikiwa.
Aliinuka, mara akamuona yule meneja wa benki anakuwa mkubwa zaidi na yeye JKS anakuwa
mdogo na chumba kinazidi kuwa kidogo, akasikia anakosa pumzi halafu giza nene
likamuingia mara akaanguka chini na kupoteza fahamu.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment