SURA YA KUMI
NA MOJA
KAMPALA
II
Ilikuwa
yapata saa moja asubuhi Willy aliposhituka kutoka usingizini baada ya kuota ndoto mbaya ya vita
ambayo aliota Bibiane akipigwa risasi sita kifuani na kupoteza maisha, alipotaka kupiga kelele alishituka kutoka usingizini, akamwona Bibiane amemlalia kifuani wakiwa
kitandani akakumbuka kuwa kumbe walikuwa Hoteli ya Sheraton, iliyoko mjini
Kampala, baada ya kuletwa hapa jana jioni kwa ndege ya serikali ya Rwanda baada ya kuchukuliwa na helikopita ya jeshi ya akina Col. Rwivanga kutoka kule
porini Kibumba walikolala baada ya usiku wa kasheshe walipofanikiwa kuiteketeza ngome ya
Akazu. Taratibu Willy alimwondoa Bibiane kwenye kifua chake na kumlaza kwenye mto.
Alichukua chombo cha kuwashia televisheni ili kusikia taarifa ya habari ya saa
moja.
Baada ya kuwasha
televisheni mtangazaji alisoma taarifa ifuatayo.
"Zaire.
Vikosi vya wapinzani wa serikali ya Zaire, vikiongozwa na mpinzani mkuu Bwana
Mpinda vimeanzisha mapigano makali dhidi ya serikali hiyo vikisaidiwa na vikosi
vya waasi wa kabila la Banyamulenge vikiongozwa na Meja Tom Kabalisa
Mubanyamulenge, aliyeasi kutoka jeshi la Zaire. Bwana Mpinda amekaririwa na
vyombo vya habari kuwa nia yao ni kuuondoa utawala wa kidikteta wa serikali
iliyoko madarakani Kinshansa. Wamejigamba wakisema usiku wa kuamkia jana
walishambulia kambi kubwa ya kivita iliyoko Kibumba, karibu na Goma na
kuteketeza silaha nyingi, vikiwemo vifaru, ndege za kivita, mizinga mkibwa na
midogo na kuua askari wapatao elfu kumi".
"Pamoja
na kwamba habari hizi hazijathibitishwa na vyombo vingine vya habari vya ndani
na nje, raia wa sehemu hiyo wamethibitisha kutokea kwa milipuko mkubwa ya ajabu
ambayo hawajawahi kuisikia katika kambi hiyo. Na wanasema wanajeshi karibu wote
na silaha zilizokuwa kwenye kambi hiyo zimeteketezwa kwa milipuko hiyo
iliyosikika mpaka Gisenyi na Goma".
"Habari
zilizotufikia hivi punde katika chumba chetu cha habari zinasema waasi tayari
wamekamata miji wa Goma na Bukavu na bado wanasonga mbele kuchukua maeneo
mengine. Vilevile, kuna habari ambazo hazijathibitishwa kuwa vikosi hivyo vya
wapinzani vinasaidiwa na vikosi vya jeshi la RPF la Rwanda".
"Hii
ina maana kuwa wapinzani wamekusudia kuung'oa utawala wa sasa ambao umedumu
madarakani kwa zaidi ya miaka thelethini sasa ambao wameupachika jina kuwa
utawala wa mabavu, unyanyasaji uliojaa rushwa na udikteta. Bado hakuna taarifa
yoyote ya kukanusha habari hizo kutoka kwa serikali ya Zaire, mji
Kinshansa".
"Na
huko Jijini Dar es Salaam, Tanzania kuna habari kuwa waziri wa ngazi ya juu
nchini humo kwa jina maarufu la JKS amefariki dunia akiwa katika benki moja
huko Geneva, Uswisi baada ya kupatwa na shinikizo la damu. Kiongozi huyo
aliondoka nchini Tanzania siku mbili zilizopita na kuelekea London kwa ajili ya
matibabu ya moyo, bado haijabainika kwa nini alikwenda Geneva, na alifuata nini
kwenye benki hiyo. Waziri huyo ndiye aliyekuwa akitegemewa kuwania urais wa
Tanzania baada ya rais wa sasa kumaliza muda wake".
Willy
alitabasamu baada ya taarifa hii iliyonoga. Kisha, akachukua simu na kumpigia
Mzee Musoke na kumwomba waonane mchana kama walivyokuwa wamepanga wakati akiwa
mjini Kigali ili ampatie ripoti ya kazi yake aliyoifanya kwa mafanikio.
"Nimefarijika
kusikia kazi yako kwenye taarifa ya habari ya asubuhi hii, wewe ni mwanaume wa
shoka", Musoke alimsifu Willy.
"Asante
mzee, tutaonana hiyo saa nane", Willy alimjibu Musoke na kukata simu.
Kisha akapiga simu nyingine.
"Pepe
mpenzi".
"Uko
wapi", Pepe aliuliza.
""Niko
Kampala narudi kesho".
"Ooh
Mungu wangu, toka umeondoka sijapata usingizi. Njoo mume wangu nina hamu sana
na wewe, nakupenda sana".
"Na
mimi zaidi, kesho mama, kwaheri", Willy akakata simu.
Bibiane
alikuwa akisikia lakini alijifanya kama hamsikii alimgeukia Willy na kusema.
"Uko wapi Willy?, njoo ulale, najua siku yangu ni leo tu, hivyo lazima
niitumie siku hii kikamilifu".
"Katika
nafsi yangu hupenda mtu anayeelewa mambo kama wewe", Willy alijibu huku
akirudi ndani ya shuka na kumkumbatia Bibiane.
MWISHO wa
HADITHI YA UCHU
WAPENDDWA
WASOMAJI, MNARUHUSIWA KUTUMA MSG KUCHAGUA HADITHI GANI YA KUSISIMUA NIWALETEE KUPITIA
BLOG YETU YA MPIGANAJI. KARIBUNI 0784296253
Comments
Post a Comment