Rais Dkt. John Pombe Magufuli, leo ametengua Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Anne Kilango Malecela (pichani), baada ya kubaini kuwa amemdanganya kuhusu kuwepo kwa watumishi hewa mkoani Shinyanga. Rais amesema amemuondoa Mkuu huyo wa mkoa baada ya kumdanganya.
Taarifa iliyotolewa Dar es Sakaan jana imeeleza kuwa Mkuu huyo wa mkoa, alitoa taarifa zisizo za kweli kwa Rais Magufuli kuwa Shinyanga hakuna wafanyakazi hewa, jambo ambalo limemuudhi rais na kuamua kuchukua hatua ya kumfukuza kazi.
Comments
Post a Comment