KIKOSI CHA KISASI

KIDOKEZO

Ni nani hasa anayewaua viongozi wa wapigania uhuru? Kwa nini viongozi hawa wameuawa wengi zaidi Kinshasa kuliko mahali pengine popote katika Afrika? Je, hatua gani zichukuliwe ili kupambana na kukomesha uhalifu huu usiokuwa na kifani?.

Naam. Umoja wa Nchi Huru za Afrika umepata jibu la masuala yote hayo na mengine. Ni Willy Gamba tena. Nyota ya Afrika na mpelelezi maarufu asiyekubali kushindwa - katika mapambano ya kutisha na kumwaga damu.

Safari hii Willy hakupambana na vikundi vya wanafunzi wa ujasusi bali ni miamba kamambe iliyojidhatiti kutenda uovu bila kujulikana. Ni mapambano ya mafahali, maana Willy naye si mchezo, na vurumai iliyotokea iliukumba mji wa Kishasa katika wimbi la misukosuko ambayo kamwe haitasahaulika.

Usalama wa viongozi wa wapigania uhuru Kusini mwa Afrika ulikuwa umetishiwa, kwani kulikuwa kumetokea mauaji ya viongozi hawa katika nchi mbalimbali za Afrika. Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) haukuweza kuvumilia hali hii, hivyo ulikata kauli kuwasaka wapinga mapinduzi hawa na kuwafagilia mbali ili kukomesha vitendo hivi vya kijahili.

Willy Gamba mpelelezi maarufu wa Afrika alijikuta amechaguliwa na OAU kuongoza kikundi cha wapelelezi wa Kiafrika cha kuwasaka na kuwatokomeza majahili hawa.

Kinsasa mji mkuu wa Zaire na mji unaosifika kwa starehe zake katika Afrika ulijikuta ni uwanja wa mapambano kati ya vijana wapiganaji shupavu wa Kiafrika wakiongozwa na Willy Gamba na wapinga mapinduzi wa Afrika wakiongozwa na Kaburu Pierre Simonard. Ndipo patashika ambalo halijawahi kutokea katika Afrika liliwaka moto katika mji huu ambalo halijatokea lisahaulike katika historia ya mapambano dhidi ya wapinga mapinduzi wa Afrika

ITAANZA RASMI 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU