WANAHABARI WAJITOKEZA KUMUAGA MPOKI BUKUKU

Baadhi ya Waandishi wa Habari na Wapigapicha kutoka Vyombo mbalimbali wakiupeleka Mwiili wa Marehemu Mpoki Bukuku kwenye Viwanja Kimanga kwa ajili ya kuuaga rasmi, Dar es Salaam leo.
 Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku.
 Baadhi ya waandishi wa Habari waliofanya kazi karibu zaidi na Marehemu Mpoki Bukuku, kutoka kushoto, Juma Abbas Pinto, Benny Kissaka, Angetile Osiah na Mobare Matinyi.
 Mke wa Marehemu Mpoki Bukuku, Lilian (katikati), akiwa na watoto wake wawili, wakisubiri kuuaga mwili wa mpendwa wao.
 Mwenyekiti wa Chama Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akizungumza wakati wa kuuaga mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku.
 Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea, akizungumza wakati wa kuuaga mwili wa Mpoki.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, Wasanii na Vijana, Nape Nnauye akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, wakisubiri kuuaga mwili wa Mpoki.

 Mpigapicha Mkuu wa The Guardian Limited, Seleman Mpochi, akizungumza na waombolezaji wakati akieleza sifa za Marehemu Mpoki Bukuku aliyefariki hivi karibuni kwa ajali ya barabarani
 Mwakilishi wa wamiliki wa Blog Tanzania (TBN), Richard Mwaikenda, akieleza sifa alizokuwa nazo Marehemu Mpoki Bukuku wakati wa uhai wake.
 Steven Nyerere, akiwakilisha wasanii wa filamu Tanzania.
 Baadhi ya waandishi wa Habari waliofika kwenye Viwanja vya KImanga.
 Mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku ukiwa ndani ya jeneza
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, Wasanii na Vijana, Nape Nnauye, akitoa heshima zake za mwisho kwenye jeneza lenye mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku, Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa Chama Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoka kuuaga mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku.
 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo, Juma Pinto (mbele) na Peter Ambilikile wakiuaga mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku.
 Benny Kissaka.
 Angetile Osiah
 Muhidin Issa Michuzi
 Jamal Rwambow
 Aliyekuwa Mpigapicha wa Daily News, Athuman Hamis, aliyepata ulemavu kwa ajali ya gari.
 Mke wa Marehemu, Lilian (picha ya juu na chini) akiuaga mwili wa mumewe Marehemu Mpoki Bukuku.

Wapigapicha wakiusindikiza Mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku kuupeleka kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea mkoani Dodoma, ambako utahifadhiwa milele.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU