KIKOSI CHA KISASI

MAUAJI YA KISHENZI 

VII

Saa hizi saa tatu za usiku, Pierre alikuwa nyumbani kwake akingojea kwa hamu kupata maelezo kamili, juu ya msako uliokuwa ukiendelea. Alikuwa ameishapata ripoti kutoka kwa Muteba, kuhusu maelezo waliyokuwa wameyapata toka kwa Tete juu ya Willy. Vile vile alimweleza kuwa Kabaya alipokwenda kumwona Mwadi alihisi kuwa Mwadi alikuwa anajua mengi juu ya Willy lakini hakutaka kueleza hivi Kabeya akamuua.

"Ni dhahiri kuwa huyu Willy ni mpelelezi, mmoja wa wale wengine, kwa hivi katika msako wetu na yeye yumo," Muteba alikuwa amemweleza. Akiwa anangojea ripoti wa Pierre alikuwa na wasiwasi sana juu ya wapelelezi hawa. Mara simu ililia akainua haraka haraka.

"Hallo," aliita.

"Patron, Muteba hapa, kumetokea mauaji mengine kwa upande wetu. Kabeya, Charles na Ngoma wameuawa. Bila shaka wameuawa na huyu Willy." KWa sauti ya utaratibu Pierre aliuliza.

"Unazungumzia wapi?|

"Nipo nyumbani kwa Kabeya".

"Wape habari Jean na Papa kuwa wote njooni tuonane hapa," Pierre aliamru na kukata simu.

ITAENDELEA 0784296253

Comments

  1. shukrani sana mkuu,ila ndo kiduchu

    ReplyDelete
  2. Enter your comment...mbona fupii hvo pia 2naomba muwe mnaitoa ata kila baada ya sik tatu

    ReplyDelete

Post a Comment

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU