KIKOSI CHA KISASI

SURA TA TISA 

USIKU WA KAZI

II

Yule mlinzi aliyetoroka kutoka ndani ya ile gereji, alikimbia mpaka kwenye kibanda cha simu kilichokuwa karibu. Alipiga simu kwenye nambari ya simu waliyokuwa wamepewa kupiga kama jambo lolote litatokea.

"Hallo," aliita.

"Hallo unasemaje?" Sauti ilijibu.

"G.A.D." alijibu.

"WP", alijibiwa.

"Aha, G.A.D imeshambuliwa tafadhali tumeni msaada upesi sana kama kikosi kizima kinatushambulia," alieleza huku akitetemeka.

"Sawa," alijibiwa na simu ikakatwa. Pierre na wenzake walikuwa wamemaliza mkutano wao uliokuwa umeitishwa usiku ule wakati simu wakati simu ilipolia. Pierre aliinua simu, "Hallo", aliita.

"Patron?" aliulizwa.

"Ndito", alijibu. 'G.A.D. inashambuliwa sasa hivi. Mapambano bado yanaendelea, nimetuma watu wengine kwenda kusaidia kutoka Papadimitriou," alielezwa.

"Vizuri tunakuja," alijibu na kukata simu. "G.A.D. inashambuliwa twendeni", aliwaeleza wenzake kwa kifupi.

"Hapana Patron, wewe baki sisi tutaenda kule hatuwezi kwenda wote", Jean alishauri.

"Ndiyo sisi tutakwenda wewe baki", Papa alikubaliana na Jean

"Mkiwakuta watu hawa tafadhali wauweni kabisa, sina haja ya kuwahoji, wameishafanya ubaya mwingi kiasi cha kuonana nao. Mimi nitawapa muda wa kutangulia halafu nitampigia afisa mmoja wa polisi rafiki yangu kuwa wezi wanashambulia gereji 'G.A.D.", alieleza Pierre. Kisha aliingia ndani ya stoo akatoa bunduki na mabomu ya mikono akawapa hawa wenzake na wakaondoka wakiwa tayari kwa mapambano huko G.A.D.     

Ni wakati walipokuwa wanaingia barabara ya Bokasa waliposikia mlipuko mkubwa uliotingisha sehemu nzima ya Gombe. Waliongeza mwendo na walipofika kwenye kona ya barabara ya 30 Juin na T.S.F. ndipo walipotambua kilichokuwa kimetokea kwani, watu wote waliokuwa wanakaa sehemu hiyo walikuwa wanakimbia ovyo kwa hofu. Walipofika sehemu ya 'Gereji G.A.D' ilipokuwa imesimama hawakukuta kitu. Tokea majengo, magari na kila kitu kilichokuwemo ndani ya sehemu ile kiliteketezwa. Nyumba zilizokuwa jirani nazo ziliharibika ingawaje si sana, maana ngome ya gereji ilizisaidia kustahimili mlipuko huu, kwani ngome yote nayo ilianguka. 

"Hakika hawa watu ni wanaharamu sana," alisema Jean kwa chuki. Mara wakasikia milio ya magari ya polisi na zimamoto unaelekea sehemu hii.

Walinzi waliokuwa wametokea Gereji Papadimitriou walifika nao wamechelewa.

"Rudini sehemu zenu", Papa alimwelezea kiongozi wa watu hawa. Papa, Muteba na Jean waliingia ndani ya gari lao na kuelekea gereji ya Papadimitriou katika uchunguzi mwingine.

ITAENDELEA 0784296253

Comments

Post a Comment

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU