KIKOSI CHA KISASI

SURA YA KUMI 

MAPAMBANO BADO YANAENDEKEA

V

Pierre na wenzake walikuwa wamekutana tena mchana huu kama walivyokuwa wameahidi.

"Nilipokwenda kuonana na Mkurugenzi huko Sozidime wakati nilipowaacha hapa nilipata habari nzuri sana kutoka BOSs. Boss imeamua kuwa baada ya kuhakikisha kuwa tumewateketeza wapelelezi hawa wa Afrika tutaruhusiwa kustaafu na kuchangua nchi yoyote tunayotaka kwenda kuishi kazi tuliyoifanya ni nzuri ya kutosha," Pierre aliwaeleza wenzake kwa tabasamu kwa mara ya kwanza tangu wafahamiane. Pierre siku zote alikuwa mtu ambaye hatabasamu wala hacheki. Kisha aliendelea. "Tayari Mkurugenzi ameishatufanyia mipango ya usafiri kiasi kwamba tukimaliza shughuli hii iliyobaki tunaondoka bila kuchelewa kwani wakati mwingine itatubidi kuondoka mjini hapa kwa haraka.

"Kwa hivi jamani tuwateketeze wapelelezi hawa mapema ndiyo itakuwa raha yetu," Pierre aliwaeleza. Kila mmoja wao waliingiwa na mawazo ya kupanga wapi pa kwenda. Muteba alimfikiria Tete.

"Sijui kama Tete atakuwa tayari kuondoka na mimi, nitaenda kumshawishi nikitoka hapa," Muteba aliwaza.

Jean naye alikuwa na haja ya kwenda kukaa Ufaransa na alikuwa siku zote anaota kwenda kuishi huko. Aliamua kuwa angemchukua Lucie aende naye kwani walikuwa wanapendana sana.

Papa yeye alikuwa anafikiria kwenda Hong Kong, kwa vile alikuwa amejiwekea pesa nyingi sana katika benki za nchi za nje basi alikuwa hana wasiwasi. Alifikiria kuwa kweli muda ulikuwa umefika kwake kustaafu ili akafaidi utajiri aliokuwa amejiwekea.

Pierre yeye alikuwa na mipango ya kwenda Marekani ambako alikuwa na marafiki aliokuwa amefanya nao kazi wakati walipokuwa amepelekwa C.I.A. kufanya kazi kwa muda, ambao sasa amestaafu. 

"Loo mpango mzuri sana. Hii kazi iliyobaki ni kidogo sana naamini tutaimaliza usiku wa leo", Papa alieleza. Kisha walianza kupanga namna watakavyoweka ulinzi wao tayari kwa kuwakabili adui zao.

"Tuna walinzi wapatao thelathini ambao ni wazuri sana sidhani tutapata matatizo yoyote hasa ikiwa sisi wenyewe ndiyo tunawaongoza. Lililobaki ni kutayarisha silaha za kutosha," Pierre alishauri.

Mara kengere ya simu ililia, Pierre aliangalia saa yake ilikuwa saa tisa na nusu, akaondoka kwenda kuijibu. Alisikiliza mara moja akajibu kwa sauti. "Tunakuja", akakata simu. Wenzie wote walimkodolea macho kwani nywele zake zilisimama.

"Vipi?" Muteba aliuliza.

"Vijana wetu wamewaona Kofi na Ozu wanaingia Hoteli Intercontinental hivi wanaomba msaada. Naamini hawatategemea kuwashambulia mchana na mbele za watu, Hivyo twende sisi wenyewe, nafikiri hii ndiyo nafasi nzuri sana," Pierre alishauri.

"Lo, tusiipoteze nafasi hii," alijibu Muteba akasimama tayari kwenda kwenye mapambano. Kundi zima la watu wanne, wakiwa ni majasusi wenye ujuzi wa hali ya juu waliondoka.

ITAENDELEA 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU