KIKOMO

KIDOKEZO

Si kazi yangu kujishughulisha na makosa ya jinai. Nilishangaa kidogo Chifu aliponiamru nifuatilie tatizo la upungufu wa Almasi. Isingekuwa kwa sura aliyoonyesha, nilitaka kumwambia apeleke malalamiko yake kwa Kamishna wa Polisi au anipe uhamisho kwenda huko kama alikuwa hanihitaji katika idara yake. Siku hiyo alivaa sura ya kutisha na sikuwa na la kufanya ila kukubali.

Kulikuwa na ushahidi kwamba Almasi zilizouzwa katika masoko ya nje zilikuwa chache sana kulingana na kiasi kilichokuwa kimechimbwa kwa nini?.

Askari Polisi Joel amegusa chanzo cha uhalifu; akafa katika ajali ya ndege siku chache kabla ya kufunga ndoa na mchumba wake Amanda, na uhalifu ukaendelea.

Chifu alimtuma Jack Mbusile, mpelelezi wa kawaida. Lakini maiti yake iliokotwa ikielea katika Ziwa Victoria na uzito wa jambo zima ukawa umetambuliwa. Ndipo nikatumwa mimi Willy Gamba.

La hasha! Kama ungetumwa wewe nina hakika ungekimbia na kupotea kabisa! Lakini mimi sio wewe. Safari yangu ilinichukua katika miji ya Mwanza, Shinyanga, Maganzo na Songwa; na uvundo niliofichua ulisababisha umwagaji mkubwa wa damu na kuteketeza maisha ya watu wengi.

Yalikuwa mapambano makali na kila mmoja wetu alishangaa kuona ni nani alikuwa anaongoza uhalifu huu.

Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako.

INAANZA RASMI 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU