MANJI AKUTANA NA WCHEZAJI NJE YA MAHAKAMA


WACHEZAJI na baadhi ya viongozi wa Klabu Bingwa ya Soka Tanzania Bara, Yanga na benchi lote la Ufundi, leo wamekutana Mwenyekiti wao wa zamani, Yussuf Manji ili kumjulia hali ambaye awali aliachiwa huru na kutoka katika gereza la Keko Jijini Dar es Salaam wiki iliyopita baada ya kufutiwa mashitaka ya Uhujumu Uchumi yaliyokuwa yanamkabiri. 

Wakati Manji anaachiwa huru, Wachezaji na benchi la ufundi la Yanga walikuwa katika mikoa ya Njombe na Ruvuma kwa ajili ya kushiriki michezo miwili ya ligi kati ya Njombe Mji na Njombe na Majimaji ya Sonea, ambapo Yanga imeambulia pointi nne na magoli mawili baada ya kushinda mchezo dhidi ya Njombe na kutoka sare na Majimaji.

Wachezaji hao wakiongozwa na Kocha Mkuu, Mzambia, George Lwandamina walimfuata Manji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kusutu, Dar es Salaam ambako alikwenda kusikiliza kesi yake nyingine inayomkabiri ya tuhuma za kutumiwa dawa za kulevya.

Pamoja na kusalimiana na kupeana mikono na wachezaji wote, lakini Manji alizungumza na kirefu na Nahodha, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kana inavyoonekana katika picha ya juu. Manji alizungumza na Cannavaro akitoka mahakamani kusikiliza kesi yake, ambayo imeahirishwa tena hadi Septemba 25, mwaka huu.
Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu, Cyprian Mkeha, Wakili wa utetezi, Hajra Mungula alisema  kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kusikilizwa na wako tayari. Alisema mteja wake anahitaji kutoka kwa ajili ya matibabu kwa sababu yuko nje kwa dhamana, hivyo akaiomba Mahakama hiyo iisikilize kesi hiyo kwa siku tatu mfululizo.

Kwa upande wake, Wakili wa Serikali Timon Vitalis alidai kwamba anataka kusafiri mchana na hatoweza kusikiliza kesi hiyo. Hakimu Mkeha alisema kwamba anakwenda kwenye kikao na kuahirisha shauri hilo hadi Septemba 25 litakaposikilizwa kwa siku tatu mfululizo hadi Septemba 27.

Ikumbukwe, Manji anadaiwa kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin kati ya Februari 6 na 9, 2017 katika eneo la Upanga Sea View Ilala alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin. Kesi hiyo ipo katika hatua za usikilizwaji wa mashahidi upande wa utetezi ambapo shahidi wa kwanza katika kesi hiyo,

Hata hivyo Mkugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Prof.Mohamed Janabi aliieleza mahakama kuwa Manji ana Vyuma kwenye moyo. Alhamisi iliyopita Septemba 14, mwaka huu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimuachia huru Manji baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) kumfutia mashtaka baada ya kusota jela kwa miezi miwili.

Mbali na Manji, wengine walioachiwa huru ni Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Quality Group Ltd, Deogratius Kisinda, Mtunza Stoo, Abdallah Sangey na Thobias Fwere. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa wameomba 'remove order' na kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) kwa niaba ya Jamhuri wanaiarifu Mahakama kwamba hakusudii kuendelea kuwashtaki Manji na wenzake katika kesi hiyo.

Hivyo wanaomba kuiondoa kesi hiyo chini ya kifungu cha 91(1) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.
Baada ya kueleza hayo Wakili wa Manji, Hajra Mungula ameeleza kuwa sheria inaruhusu DPP kufanya hivyo na kutokana na hatua hiyo, Hakimu Shaidi amesema kesi hiyo imefutwa na kuanzia sasa washtakiwa wapo huru.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU