NJAMA
HADITHI YA KUSISIMUA YA UPELELEZI 
SURA YA TATU

"Unajuwa Willy dakika ile mtu anapozaliwa pale pale anapewa huku ya kifo. Nina maana ya kusema

kuwa binadamu hata aishi vipi kufa lazima atakufa. Kule kuishi baada ya kuzaliwa ina maana

kuwa ile hukumu ya kifo inaahirishwa kutekelezwa.Wengine huahirishwa kwa mwezi mmoja. Hivyo

mtoto anazaliwa na baada ya mwezi mmoja anakufa. Hii si ajabu maana hukumu yake ya kifo

imetekelezwa baada ya mwezi mmoja. Wengine huishi hata miaka mia moja. Hii ina maana kuwa

hukumu yake aliyopewa dakika alipozaliwa imetekelezwa baada ya miaka mia.Hivyo kila mtu na

sehemu yake ya kuishi. Kwa hiyo kuogopa kufa ni ujinga."

"Mimi sina wasiwasi, maana kifo cha namna hii, nitakuwa nimekufa kifo cha heshima", alisema

Sherriff.

"Okke, sasa naamini nina watu. Tokea sasa nyinyi si ndugu tena ila ni makomredi", niliwaeleza.

"Kwani komredi ina maana kubwa zaidi ya ndugu?", Veronika aliuliza.

"Hasa, ina maana kali zaidi. Komredi ina maana mwenzi katika harakati".

"Asante komredi Willy, naona tunywe maji haya katika jina la komredi", Veronika aliomba. Wote

tukagonganisha glasi zetu.

"Sasa mimi naonelea itabidi tuanze upelelezi wetu bandarini. Itabidi tukamuone ofisa

aliyehusina ili na sisi tupate habari toka kwake ana kwa ana ingawaje atakuwa amekwisha

sumbuliwa sana na polisi na maafisa usalama kwa maswali. Huenda sisi tukapata jambo ambalo

huenda wao wameliruka. Halafu tukaendelea hivyo hivyo katika ofisi zote zilizohusika kabla

hatujachukua hatua kali zaidi", mnaonaje.

"Sawa", walijibu kwa pamoja.

Tulinyanyuka na kuelekea kwenye gari langu, nikawafungulia milango. Veronika alikaa mbele na

mimi. Sherriff akakaa nyuma. Nilipotaka kuwasha gari moto niliona kijikaratasi chini,

nikakiokota taratibu nikakisoma. Eddy alikuwa ameniandikia namba zote za magari aliyokodi.

Akionesha namba za magari aliyoacha kwenye maegesho ya New Afrika na Kilimanjaro Hoteli kama

nilivyokuwa nimeamru. Nilianza kusikia msisimko wa damu ikionyesha kuwa kazi imeanza. Nilipiga

gari moto tukaelekea bandarini.

MIWSHO WA SURA YA TATU


NJAMA
FUNUNU
SURA YA NNE
"Samahani binti tunaomba kumuona Meneja", nilimwambia mwandishi mahsusi wa Meneja wa Bandari.

"Sijui nyinyi ni akina nani?", aliuliza msichana huyu aliyeonekana amechoka choka.

"Mwambie ni Willy Gamba na wateja wake kutoka gazeti la Afrika".

Meneja wa Bandari tulikuwa tunafahamiana kikazi, hasa kutokana na shughuli zingine tulizokuwa

tunazifanya katika kampuni yetu ya Afrika Internation Agencies.

Yule msichana alizungumza na bosi wake kwa simu, alipomaliza alinyanyuka na kutufungulia

mlango tukaingia ndani. Tulimkuta Issack Mlingi ambaye ndiye Meneja wa Bandari aliyehusika na

tukio hili akionyesha hali ya kuchoka sana. Nafikiri hii ilitokana na bughudha alizopata toka

kwa polisi na watu wengine wanaohusika na upelelezi wa tukio hili. Macho yake yalikuwa mekundu

na yamevimba.

"Karibuni ndani", alisema huku akinyanyuka ili tusalimiane.

"Samahani ndugu Mlingi, naamini una shughuli nyingi sana", nilimuomba radhi.

"Si kitu Gamba, karibuni".

"Hawa ni wateja wangu Sherriff na Veronika kutoka gazeti la Afrika ambalo kampuni yangu ni

wakala wake, na jamani huyu ni Issack Mlingi, Meneja wa Bandari", walipeana mikono kisha wote

tukavuta viti tukakaa.

"Ndugu Mlingi ni imani yangu kuwa umeisha ulizwa maswali mengi juu ya tukio hili lililotokea

hapa bandarini. Lakini naamini hatutakuwa tumekuhangaisha kama tutakuuliza maswali. Kama

nilivyokwisha kwambia hawa waandishi wa gazeti la Afrika na ni waandishi pekee walioruhusiwa

kuingia hapa nchini kuandika juu ya tukio hili, naamini unajua msimamo wa gazeti la Afrika.

Hata hivyo tutakuuliza maswali kidogo tu kusudi tusikuchoshe sana".

"Hebu nipeni vitambulisho vyenu niviangalie", aliomba.

Sherriff na Veronika walimpa vitambulisho, akaviangalia na aliporidhika akavirudisha.

"Haya ulizeni maswali yenu, maana ikiendelea hivi naweza kupata wazimu", alisema huku akitoa

tabasamu la uchovu.

"Tumesoma maelezo yako uliyotoa polisi, ila tumekuja hapa kukuuliza maswali machache juu ya

mambo ambayo hatukuwa tumeyaelewa vizuri", alisema Sherriff.

"Ulieleza kuwa ulipata simu kutoka kwa Jones Mantare ambaye umezoea sana sauti yake, kiasi

kwamba huwezi kuikosea ukiisikia. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba, Mantare anasema hakuwa

amekupigia simu kwani alikuwa na mkutano na Mwenyekiti wa Kamati na Mwenyekiti amethibitisha

kuwa ni kweli walikuwa wote toka saa tisa hadi saa kumi na moja. Baada ya kupata maelezo hayo

bado unaweza kusema kuwa sauti ile ni sawa kabisa na ya Mantare?".

"Kwa sababu wakati ule nilikuwa sina wasiwasi kuwa kuna jambo baya roho yangu iliridhika kuwa

ni Mantare. Lakini sasa kwa sababu Mantare anasema hakupiga simu, ndipo nakumbuka kuwa

nilimwuliza kama ana mafua, maana kwa mbali alikuwa akizungumzia puani, na yeye alijibu kweli

mafua yalikuwa yamemkaba sana. Lakini maelezo mengine, mathalani ambayo huwa tunataniana na

Jonas, yalikuwa yote sawa. Kusema kweli inawezekana kabisa alikuwa mtu mwingine anayemfahamu

sana, lazima niseme sana maana isingekuwa hili jambo la mafua bado ningeendelea kung'ang'ania

alikuwa Jones. Lakini Jones amekuja hapa hana mafua hata kidogo kwa siku nyingi".

"Hebu fikiria tena kidogo juu ya sura na sauti au umbile na tabia ya huyu mtu aliyekuwa

akijiita Meja Paul Liboi, unaweza kuwa na uhakika kabisa kuwa mtu huyu ni mzalendo wa

Tanzania?", Veronika aliuliza.

Ndugu Mlingi alisita kidogo kujibu swali hili na uso wake ukakunjamana kidogo. Baada ya

kufikiri sana akasema.

"Nafikiri anaweza asiwe mzalendo".

Wote tukamwangalia.

"Kwanini unafikiri hivyo?", mimi nilimuuliza.

"Wazo hili lilikuwa halijaingia kichwani mwangu, lakini sasa baada ya kuuliza swali hili

inawezekana mtu huyu asiwe mtanzania maana kwanza kiswahili chake hakikuwa kimenyooka na

alipenda sana kuchanganya na kiingereza. Mimi nilimfikiria kuwa huenda ni Mjaruo, lakini

alikuwa hajang'oa meno. Vile vile alikuwa na haraka haraka na maneno ya mkato mkato. Nikifiri

sana hakuna na ile hali ya kirafiki waliyonayo watanzania wengine wengi. Lakini kwa sababu

nilijuwa ni mwanajeshi nikafikiri ndio sababu aikuwa na tabia ya namna hiyo".

"Una jambo jingine ambalo huenda sasa unafikiri halikuwa lakawaida juu ya tukio lolote baada

ya kujuwa watu hawa walikuwa majahiri?".

"Nafikiri nimeshasema yote, ila tu huenda kitu kimoja, sijui kama kinahusika ama vipi".

"Ehe, kitu gani".

"Baada ya kuzungumza na huyo anayejiita Jones Mantare, simu za jengo hili hazikufanya kazi

tena. Tulipowaeleza Posta kesho yake, walikuja mafundi na kusema waya inayounganisha jengo

hili na waya zinazokwenda Posta ilikuwa imekatika kwa kuangukiwa na mti. Sasa nilianza kuona

picha kidogo ya tukio hili. Nilijua mara moja kuwa watu waliokuwa wameshughulikia tukio hili

ni watu wenye kujua ujasusi wa hali ya juu; kwani walihakikisha kuwa kila hatua wanayoichukua

na nyayo zake wanazifuta ili asiwepo mtu wa kuzifuatiia".

TUjikuta tumeridhishwa sana na safari yetu ya bandarini hivyo tukaona tuondoke.

"Asante sana ndugu Mlingi, kama tukihitaji mambo zaidi tutakuona tena, na kama utakumbuka kitu

cochote kinachoweza kutusaidia nipigie simu. Nafikiri simu yangu unayo?", nilimuuliza.

"Ndio ninayo", alijibu.

"Na tahadhali usizungumze ovyo juu ya tukio hili, maana si tukio zuri", nilimwonya.

"Bila shaka nitajitahidi".

Tuliagana nae, tukaondoka kuelekea mjini.

INAENDELEA...



Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU