NJAMA

SURA YA SITA

CHIMALAMO

IV

Ofisi za SANP zilikuwa barabara ya Umoja wa Mataifa baada ya kuvuka barabara inayoingia Hospitali ya Muhimbili. Hivyo niliendesha moja kwa moja na kuingia barabara ya Morogoro kutokea mtaa wa Makunganya. Tulipofika kwenye taa za usalama barabara za Jangwani, nilikata kulia na kuingia barabara ya Umoja wa Mataifa. Nilisimamisha gari karibu na mlango wa ofisi kwani kwa upande mwingine wa barabara kuna gereji na magari yalikuwa yamejaa kibao.

Tuliingia mapokezi na kumkuta binti mmoja anajipaka poda usoni. Alipotuona akaweka mkebe wa poda kando, alijifuta vizuri usoni halafu akatutolea tabasamu.

"Karibuni".

"Asante. Hujambo Binti?".

"Mimi sijambo, sijui niwasaidie nini?".

"Tunaomba kuonana na Ndugu Sikazwe.

"Mna miadi naye?".

"Hapana".

"Basi hawezi kuwaona, ana kazi nyingi sana. Huenda mnaweza kumwona ndugu Amos Shumka ambaye naye ni ofisa katika ofisi hii".

"Wewe ni Mtanzania?".

"Ndio".

"Basi dada sisi hatutaki kumwona mtu mwingine ila ndugu Sikazwe".

"Basi kaka yangu, ndio huwezi kumwona leo. Amesema hawezi kumwona mtu yeyote hata awe nani kama hana miadi naye. Mimi ninatii amri ya wakubwa wangu kwa hiyo siwezi kufanya vinginevyo".

"Jaribu kumpigia simu umwambie sisi tunataka kumwona tunatoka gazeti la Afrika, mwache yeye aamue".

"Hata kama mnatoka katika gazeti la dunia, siwezi", alichukua rangi ya midomo na kuanza kujipaka.

"Naona tumenoa", alisema Veronika.

"Basi, tutajipeleka wenyewe, twendeni", niliwaambia wenzangu.

Yule msichana alisimama na kututangulia haraka haraka na kuelekea kwenye ofisi moja huku uso wake umejaa hasira. Na sisi tukamfuata mbio mbio nyuma. Alipofungua mlango wa ofisi hiyo tu na sisi tukaingia.

Hawa watu nimewakatalia kumwona mzee lakini wamekuja kwa mabavu", alimweleza msichana mwingine aliyekuwa anapiga taipu. Kabla yule msichana hajajibu mimi nilipita mbele na kufungua mlango wa ofisi ya ndugu Sikazwe kwani bila huyu msichana kujua alikuwa ametuelekeza mwenyewe. Wasichana wote wawili walibaki wameshikwa na butwaa na kushika midomo yao. Mimi nilifungua mlango na wote watatu tukaingia ndani. Tulimkuta Ndugu Sikazwe anazungumza kwenye simu, na alipotuona tunaingia mara moja alikata simu na sura yake ikawa na hasira. 

"Nani amewaruhusu kuingia ofisini mwangu kwa kikuku namna hii?".

"Samahani ndugu Sikazwe. Sisi tunatoka kwenye ofisi za gazeti la Afrika na tumekuja kukuona kwa jambo la maana sana kuhusu wewe na Afrika nzima. Sasa tulipofika hapa ofisini kwako mzee, msichana wa mapokezi akatukatalia tusikuone. Kwa sababu sisi tuna uhakika kuwa ungeturuhusu tuonane nawe, tumeona hatuna budi kufanya jambo lililo la busara, ambalo ni kujileta sisi wenyewe tukiwa na imani kubwa kuwa utatuona. Naamini umeelewa kwa nini tumechukua hatua hii, na ukiwa kiongozi mmojawapo mwenye busara kati ya viongozi wa vyama vya wapigania uhuru wa Afrika Kusini tuna imani utatupokea kwa mikono miwili. Jambo lililotuleta si jambo la kitoto", nilimweleza kwa utaratibu sana.

Ghafla uso wake ukabadilika. Tabasamu kubwa likaonekana usoni mwake naye akasimama.

"Samahani sana ndugu zangu katika jina la Afrika huru. naamini mtawasamehe hao wasichana pamoja na mimi, kwani ilibidi kutoa amri hiyo kwa sababu sasa hivi nashughulikia tukio ambalo limetokea hivi karibuni ambalo limevuruga vichwa vyetu. Msiwe na wasiwasi jioneni kama halikutokea jambo la kuwaudhi. Karibuni tuendelee na shughuli zilizowaleta".

Baada ya maelezo haya tulipeana mikono tukajulishana kisha tukaketi chini tayari kwa mazungumzo.

"Nafikiri ndugu Gamba tumewahi kuonana?", aliuliza.

"Ndio tumewahi kuonana kwenye tafrija nyingi".

"Umesema kampuni yako ndio wakala wa gazeti la Afrika hapa Tanzania?".

"Ndio".

"Aisee, haya mimi niko tayari tuendelee na mazungumzo yaliyowaleta".

Veronika alikohoa kuliweka koo lake vizuri kabla hajaanza kusema. Alipokuwa tayari alichukua uwanja.

"Gazeti la Afrika ni gazeti ambalo limekuwa na litazidi kutetea mapambano ya Kusini mwa Afrika. Hivi majuzi tumesikia tukio lililotokea hapa mjini, ambalo sisi tumelichukua kama pigo kubwa sana kwenye harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Ndio sababu tuko hapa ili tuweze kuzungumza na viongozi wa Serikali ya Tanzania na Maraisi wa vyama vya wapigania Uhuru walioko hapa nchini hivyo tuweze kupata mwanga wa jambo hili. Kumekuwa na uvumi wa kutatanisha ulimwengu mzima juu ya tukio hili.

"Kuna mambo mawili yanazungumziwa. Jambo la kwanza ni kwamba tukio hili limetokana na njama za mabeberu za kutaka kuzima harakati za ukomboni Afrika Kusini na ndiyo sababu silaha hizi zimeibiwa. Wengine wanalaumu serikali ya Tanzania kuwa ndiyo iliyofanya njama hizi kwani silaha zilizokuwa zimekuja. Serikali yoyote hata iwe ya kimapinduzi namna gani ingeweza kupata kishawishi cha kuchukua silaha hizi kwa manufaa yake. Sijui wewe una mawazo gani juu ya jambo hili", Veronika aliuliza baada ya kutoa maelezo haya marefu.

"Kusema kweli mimi bado nimechanganyikiwa juu ya tukio hili. Mambo yote haya mawili nimeyasikia lakini bado mimi sijasikia uamuzi jambo lipi ni sawa. Kama mlivyonikuta hata mimi najaribu kuzungumza na maofisa mbali mbali wa serikali ya Tanzania na Ofisi ya ukombozi ya OAU ili na mimi nipate msimamo wangu. Tukio hili si la kukimbilia kuamua".

"Kwa hiyo tuseme una wasiwasi kuwa huenda ikawa kweli Serikali ya Tanzania ikawa inahusika?", aliuliza Veronika huku macho yake yakimwuliza Sikazwe.

"Sikazwe alisita kidogo akajaribu kukwepa macho ya Veronika.

"Sina wasiwasi na Serikali ya Tanzania kuhusika na tukio hili, lakini ili niwe na uhakika vile vile ni lazima nichunguze upande huo vile vile. Msinielewe vibaya, mimi ni mtu ambaye mara kwa mara hupenda kuchunguza mambo na nipatapo ukweli nang'ang'ania kwenye ukweli. Sijui mumenielewa?".

"Mimi nimekuelewa kuwa utakuwa na uhakika tu kuwa Tanzania haijahusika utakapopata ukweli wa jambo lilivyo", Veronika alijibu.

Sikazwe alisita tena.

"Kitu kama hicho. Mnajua sisi wapigania Uhuru tuko katika hali ya kutatanisha sana. Kwa sababu serikali za nchi huru za Kiafrika unakuta moja inapendelea chama hiki nyingine chama kile maana sisi tuko vyama vingi. Hivyo ili kuamua jambo hili ni lazima uangalie mambo mengi", alijibu.

"Kama nimekuelewa vizuri unatupa tena hali ya tatu kuwa huenda si Tanzania wala mabeberu waliohusika katika njama hizi ila inaweza kuwa nchi mojawapo katika nchi huru za Kiafrika", nilisema.

"Nafikiri sasa umenipata".

Sisi tuliangaliana kwa mshangao kwani fikra hii ilikuwa haijaingia vichwani mwetu.

"Vizuri tumejua msimamo wako", nilijibu.

"Kwa hiyo ili niweze kuwapa msimamo wangu kamili mnipe muda ili niweze kutuliza mawazo yangu baada ya kuzungumza na watu fulani".

"Unamjua kijana mmmoja aitwae George Kiki", Sherriff aliuliza.

Sura ya Sikazwe ilionyesha mshituko ambao ni mtu kama mimi tu ambaye angeweza kuona.

"Ndio ninamkumbuka aliwahi kuja hapa ofisini kwangu akiwa mkimbizi kutoka Afrika Kusini baada ya matatizo ya Soweto. Na sisi huwa ni wajibu wetu kama chama cha wapigania uhuru kuwasaidia. Tokea siku hiyo mpaka leo sijapata kumwona tena. Je ana nini?".

"Amekutwa ameuawa nyumbani kwake", Sherriff alimjibu.

Sikazwe alionyesha hali ya mshangao.

"Nimesikitishwa sana; alionekana kijana mzuri".

Simu ililia Sikazwe akaichukua.

"Sikazwe hapa".

Akaisikiliza kwa muda halafu akajibu. "Sawa, nakuja sasa hivi".

Akakata simu.

"Sijui mna maswali zaidi maana nahitajiwa ofisi za Ubalozi wa Botswana kwani kesho kutwa nina safari ya kwenda huko kuonana na wanachama na wanajeshi wangu walioko huko".

Tulitazamana tukaona hakuna zaidi.

"Nafikiri inatosha, tukikuhitaji naamini utakuwa tayari kutuona kabla hujaondoka".

"Bila shaka".

Tulisimama, tukapeana mikono na tukaagana. Tulitoka na kuingia ndani ya ofisi ya mwandishi wake.

"Hujambo mrembo, maana hatukusalimiana wakati tunaingia kwani tulikuwa katika haraka", nilimsalimu.

"Mimi sijambo", alijibu huku bado anatuangalia kwa macho ya kushangaa.

Tulimwacha ashangae tukatoka nje ya ofisi na kuelekea mapokezi. Hapo tulimkuta yule msichana.

"Siku nyingine ukitukatalia utafukuzwa kazi. Angalia vizuri sana sura hizi maana sidhani utapata kazi mahali pengine wanakochukua muda kujirembua wakati wa kazi. Hivyo chunga kazi yako", nilimshauri.

"Si nikikosa kazi kwa sababu yako nitakutafuta".

"Nani atataka msichana wa kujirembua huku chungu jikoni kinaungua nyumbani kwake?".

Msichana yule alivimba, tukaona tuondoke kabla hajapasuka. Tulipotoka nje tulielekea moja kwa moja kwenye gari letu tayari kwa safari ya mjini. Ghafla nikasikia sauti.

"Bosi, rukeni ua".

Kama umeme tuliruka na kuanguka chini upande mwingine wa ua wakati ambapo risasi zilimiminika pale pale tulipokuwa tumesimama.

"Nenda ofisini", tulisikia sauti ya Eddy ikiamru.

Kama umeme tuliruka na kuangukia mapokezi wakati tuliposikia mlipuko mkubwa wa bomu uliotingisha hata ofisi za SANP.

Baada ya dakika-mbili hivi Eddy alisimamisha gari lake mbele ya mlango na kuamru twende. Kama risasi tuliingia ndani ya gari na kuondoka kasi na kuacha gari langu likiwa limesambazwa vipande vipande.

ITAENDEEEEEEEEEEENJAMA
CHIMALAMO
IV

Ofisi za SANP zilikuwa barabara ya Umoja wa Mataifa baada ya kuvuka barabara inayoingia hospitali ya Muhimbili. Hivyo niliendesha moja kwa moja na kuingia barabara ya Morogoro kutokea mtaa wa Makunganya. Tulipofika kwenye taa za usalama barabara ya Jangwani, nilikata kulia na kuingia barabara ya Umoja wa Mataifa. Nilisimamisha gari karibu na mlango wa ofisi kwani kwa upande mwingine wa barabara kuna gereji na magari yalikuwa yamejaa kibao.

Tuliingia mapokezi na kumkuta binti mmoja anajipaka poda usoni. Alipotuona akaweka mkebe wa poda kando, alijifuta vizuri usoni halafu akatutolea tabasamu.

"Karibuni".

"Asante. Hujambo Binti?".

"Mimi sijambo, sijui niwasaidie nini?".

"Tunaomba kuonana na Ndugu Sikazwe.

"Mna miadi naye?".

"Hapana".

"Basi hawezi kuwaona, ana kazi nyingi sana. Huenda mnaweza kumwona ndugu Amos Shumka ambaye naye ni ofisa katika ofisi hii".

"Wewe ni Mtanzania?".

"Ndio".

"Basi dada sisi hatutaki kumwona mtu mwingine ila ndugu Sikazwe".

"Basi kaka yangu, ndio huwezi kumwona leo. Amesema hawezi kumwona mtu yeyote hata awe nani kama hana miadi naye. Mimi ninatii amri ya wakubwa wangu kwa hiyo siwezi kufanya vinginevyo".

"Jaribu kumpigia simu umwambie sisi tunataka kumwona tunatoka gazeti la Afrika, mwache yeye aamue".

"Hata kama mnatoka katika gazeti la dunia, siwezi", alichukua rangi ya midomo na kuanza kujipaka.

"Naona tumenoa", alisema Veronika.

"Basi, tutajipeleka wenyewe, twendeni", niliwaambia wenzangu.

Yule msichana alisimama na kututangulia haraka haraka na kuelekea kwenye ofisi moja huku uso wake umejaa hasira. Na sisi tukamfuata mbio mbio nyuma. Alipofungua mlango wa ofisi hiyo tu na sisi tukaingia.

Hawa watu nimewakatalia kumwona mzee lakini wamekuja kwa mabavu", alimweleza msichana mwingine aliyekuwa anapiga taipu. Kabla yule msichana hajajibu mimi nilipita mbele na kufungua mlango wa ofisi ya ndugu Sikazwe kwani bila huyu msichana kujua alikuwa ametuelekeza mwenyewe. Wasichana wote wawili walibaki wameshikwa na butwaa na kushika midomo yao. Mimi nilifungua mlango na wote watatu tukaingia ndani. Tulimkuta Ndugu Sikazwe anazungumza kwenye simu, na alipotuona tunaingia mara moja alikata simu na sura yake ikawa na hasira. 

"Nani amewaruhusu kuingia ofisini mwangu kwa kikuku namna hii?".

"Samahani ndugu Sikazwe. Sisi tunatoka kwenye ofisi za gazeti la Afrika na tumekuja kukuona kwa jambo la maana sana kuhusu wewe na Afrika nzima. Sasa tulipofika hapa ofisini kwako mzee, msichana wa mapokezi akatukatalia tusikuone. Kwa sababu sisi tuna uhakika kuwa ungeturuhusu tuonane nawe, tumeona hatuna budi kufanya jambo lililo la busara, ambalo ni kujileta sisi wenyewe tukiwa na imani kubwa kuwa utatuona. Naamini umeelewa kwa nini tumechukua hatua hii, na ukiwa kiongozi mmojawapo mwenye busara kati ya viongozi wa vyama vya wapigania uhuru wa Afrika Kusini tuna imani utatupokea kwa mikono miwili. Jambo lililotuleta si jambo la kitoto", nilimweleza kwa utaratibu sana.

Ghafla uso wake ukabadilika. Tabasamu kubwa likaonekana usoni mwake naye akasimama.

"Samahani sana ndugu zangu katika jina la Afrika huru. naamini mtawasamehe hao wasichana pamoja na mimi, kwani ilibidi kutoa amri hiyo kwa sababu sasa hivi nashughulikia tukio ambalo limetokea hivi karibuni ambalo limevuruga vichwa vyetu. Msiwe na wasiwasi jioneni kama halikutokea jambo la kuwaudhi. Karibuni tuendelee na shughuli zilizowaleta".

Baada ya maelezo haya tulipeana mikono tukajulishana kisha tukaketi chini tayari kwa mazungumzo.

"Nafikiri ndugu Gamba tumewahi kuonana?", aliuliza.

"Ndio tumewahi kuonana kwenye tafrija nyingi".

"Umesema kampuni yako ndio wakala wa gazeti la Afrika hapa Tanzania?".

"Ndio".

"Aisee, haya mimi niko tayari tuendelee na mazungumzo yaliyowaleta".

Veronika alikohoa kuliweka koo lake vizuri kabla hajaanza kusema. Alipokuwa tayari alichukua uwanja.

"Gazeti la Afrika ni gazeti ambalo limekuwa na litazidi kutetea mapambano ya Kusini mwa Afrika. Hivi majuzi tumesikia tukio lililotokea hapa mjini, ambalo sisi tumelichukua kama pigo kubwa sana kwenye harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Ndio sababu tuko hapa ili tuweze kuzungumza na viongozi wa Serikali ya Tanzania na Maraisi wa vyama vya wapigania Uhuru walioko hapa nchini hivyo tuweze kupata mwanga wa jambo hili. Kumekuwa na uvumi wa kutatanisha ulimwengu mzima juu ya tukio hili.

"Kuna mambo mawili yanazungumziwa. Jambo la kwanza ni kwamba tukio hili limetokana na njama za mabeberu za kutaka kuzima harakati za ukomboni Afrika Kusini na ndiyo sababu silaha hizi zimeibiwa. Wengine wanalaumu serikali ya Tanzania kuwa ndiyo iliyofanya njama hizi kwani silaha zilizokuwa zimekuja. Serikali yoyote hata iwe ya kimapinduzi namna gani ingeweza kupata kishawishi cha kuchukua silaha hizi kwa manufaa yake. Sijui wewe una mawazo gani juu ya jambo hili", Veronika aliuliza baada ya kutoa maelezo haya marefu.

"Kusema kweli mimi bado nimechanganyikiwa juu ya tukio hili. Mambo yote haya mawili nimeyasikia lakini bado mimi sijasikia uamuzi jambo lipi ni sawa. Kama mlivyonikuta hata mimi najaribu kuzungumza na maofisa mbali mbali wa serikali ya Tanzania na Ofisi ya ukombozi ya OAU ili na mimi nipate msimamo wangu. Tukio hili si la kukimbilia kuamua".

"Kwa hiyo tuseme una wasiwasi kuwa huenda ikawa kweli Serikali ya Tanzania ikawa inahusika?", aliuliza Veronika huku macho yake yakimwuliza Sikazwe.

"Sikazwe alisita kidogo akajaribu kukwepa macho ya Veronika.

"Sina wasiwasi na Serikali ya Tanzania kuhusika na tukio hili, lakini ili niwe na uhakika vile vile ni lazima nichunguze upande huo vile vile. Msinielewe vibaya, mimi ni mtu ambaye mara kwa mara hupenda kuchunguza mambo na nipatapo ukweli nang'ang'ania kwenye ukweli. Sijui mumenielewa?".

"Mimi nimekuelewa kuwa utakuwa na uhakika tu kuwa Tanzania haijahusika utakapopata ukweli wa jambo lilivyo", Veronika alijibu.

Sikazwe alisita tena.

"Kitu kama hicho. Mnajua sisi wapigania Uhuru tuko katika hali ya kutatanisha sana. Kwa sababu serikali za nchi huru za Kiafrika unakuta moja inapendelea chama hiki nyingine chama kile maana sisi tuko vyama vingi. Hivyo ili kuamua jambo hili ni lazima uangalie mambo mengi", alijibu.

"Kama nimekuelewa vizuri unatupa tena hali ya tatu kuwa huenda si Tanzania wala mabeberu waliohusika katika njama hizi ila inaweza kuwa nchi mojawapo katika nchi huru za Kiafrika", nilisema.

"Nafikiri sasa umenipata".

Sisi tuliangaliana kwa mshangao kwani fikra hii ilikuwa haijaingia vichwani mwetu.

"Vizuri tumejua msimamo wako", nilijibu.

"Kwa hiyo ili niweze kuwapa msimamo wangu kamili mnipe muda ili niweze kutuliza mawazo yangu baada ya kuzungumza na watu fulani".

"Unamjua kijana mmmoja aitwae George Kiki", Sherriff aliuliza.

Sura ya Sikazwe ilionyesha mshituko ambao ni mtu kama mimi tu ambaye angeweza kuona.

"Ndio ninamkumbuka aliwahi kuja hapa ofisini kwangu akiwa mkimbizi kutoka Afrika Kusini baada ya matatizo ya Soweto. Na sisi huwa ni wajibu wetu kama chama cha wapigania uhuru kuwasaidia. Tokea siku hiyo mpaka leo sijapata kumwona tena. Je ana nini?".

"Amekutwa ameuawa nyumbani kwake", Sherriff alimjibu.

Sikazwe alionyesha hali ya mshangao.

"Nimesikitishwa sana; alionekana kijana mzuri".

Simu ililia Sikazwe akaichukua.

"Sikazwe hapa".

Akaisikiliza kwa muda halafu akajibu. "Sawa, nakuja sasa hivi".

Akakata simu.

"Sijui mna maswali zaidi maana nahitajiwa ofisi za Ubalozi wa Botswana kwani kesho kutwa nina safari ya kwenda huko kuonana na wanachama na wanajeshi wangu walioko huko".

Tulitazamana tukaona hakuna zaidi.

"Nafikiri inatosha, tukikuhitaji naamini utakuwa tayari kutuona kabla hujaondoka".

"Bila shaka".

Tulisimama, tukapeana mikono na tukaagana. Tulitoka na kuingia ndani ya ofisi ya mwandishi wake.

"Hujambo mrembo, maana hatukusalimiana wakati tunaingia kwani tulikuwa katika haraka", nilimsalimu.

"Mimi sijambo", alijibu huku bado anatuangalia kwa macho ya kushangaa.

Tulimwacha ashangae tukatoka nje ya ofisi na kuelekea mapokezi. Hapo tulimkuta yule msichana.

"Siku nyingine ukitukatalia utafukuzwa kazi. Angalia vizuri sana sura hizi maana sidhani utapata kazi mahali pengine wanakochukua muda kujirembua wakati wa kazi. Hivyo chunga kazi yako", nilimshauri.

"Si nikikosa kazi kwa sababu yako nitakutafuta".

"Nani atataka msichana wa kujirembua huku chungu jikoni kinaungua nyumbani kwake?".

Msichana yule alivimba, tukaona tuondoke kabla hajapasuka. Tulipotoka nje tulielekea moja kwa moja kwenye gari letu tayari kwa safari ya mjini. Ghafla nikasikia sauti.

"Bosi, rukeni ua".

Kama umeme tuliruka na kuanguka chini upande mwingine wa ua wakati ambapo risasi zilimiminika pale pale tulipokuwa tumesimama.

"Nenda ofisini", tulisikia sauti ya Eddy ikiamru.

Kama umeme tuliruka na kuangukia mapokezi wakati tuliposikia mlipuko mkubwa wa bomu uliotingisha hata ofisi za SANP.

Baada ya dakika-mbili hivi Eddy alisimamisha gari lake mbele ya mlango na kuamru twende. Kama risasi tuliingia ndani ya gari na kuondoka kasi na kuacha gari langu likiwa limesambazwa vipande vipande.   
 
ITAENDELEA

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU