HOFU

ARUSHA
II

Saa tatu juu ya alama Bon Sipele alibisha hodi kwenye chumba cha Willy, huko New Arusha Hotel, kama walivyokuwa wamepanga jana yake.

"Hakllo vipi", Bon alimsalimia. Rocky alikuwa amejilaza kitandani.

"Wewe ni mchawi nini?, ulipotelea wapi?", Willy aliuliza.

"Wewe mwenyewe unajuwa kwamba kujibadilisha kama kinyonga na kuwapotea watu ndio mchezo wangu", Bon alijibu kwa mzaha.

"Hivi ulipita pale pale? Sidhani. Hata mimi nisikutambue?", Willy aliuliza kwa mshangao.

"Mimi nilikuona umejibanza kwenye nguzo. Nikakurushia busu la uzima halafu nikawahi kwenda kulala ili leo niamke safi", Bon alijibu.

"Si kitu. SItaki kujua ulitoka vipi", Willy alisema. "Inatosha kukuona mzima kwani tulikuwa na wasiwasi huenda umetekwa nyara. Huo ukinyonga wako uweke iwe siri yako, kwani huenda utakufaa baadaye. Maana kusema kweli ulitupotea kishenzi. Hapo hata mimi nimevua kofia".

"Eh, vipi, mbona kama kwamba nyinyi nyote mmelala humu maana naliona sanduku la Rocky Equator Hoteli ilijaa", Bon aliuliza.

"Ilijaa?", Rocky alidakia, "Hebu Willy mpashe kabla hajauliza mengi".

"Sisi bado hatujalala kama wewe. Mpaka sasa lazima ujuwe kwamba majasusi wameshaingia hapa. Zaidi ya hayo, jana usiku tumepambana nao!", Willy alianza kumweleza yote yaliyotokea usiku ule.

Bon alisikiliza kwa mshangao mkubwa.

ITAENDELEA

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU