Mwakilishi wa Mauzo ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kanda
ya Temeke, Alen Mwebuga (kushoto), akimkabidhi Mganga Mkuu wa Kituo cha
Afya cha Mbagala Round Table Maternity Home, Dkt. Baturi Luhanda, mfano wa
Hundi ya Milioni 20, za kuchimba kisima cha maji.
Wengine ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu (wa pili
kulia), Mhandisi wa Maji, Onesmo Zakaria na Rais wa Rotary Klab, Agnes
Batenga.
HEKAYA ZA ABUNUWASI
HEKAYA ZA ABUNUWASI ni kitabu cha hadithi za kusisimua, zinazofurahisha sana kutokana na umahili wa watunzi wa vitabu vya kale. Kutokana na utamu wa hadithi za ABUNUWASI, Blog ya MPIGANAJI itawaletea hadithi hizo ili kuwachangamsha akili............... KISA CHA ABUNUWASI NA MFALME SIKU moja alfajiri, wakati wananchi wa mji wenye wakazi wengi walipokwenda kuchota maji mtoni, walishangazwa kuuona mkono wa mtu ukiwa katikati ya mto. Mkono huo wa ajabu ulikuwa umenyoosha vidole viwili juu, kuonyesha alama ya mbili. Wananchi walistushwa sana na kitendo hicho, wakaogopa hata kuchota maji mtoni, kwani hawakuwahi kuona tukio la kuogopesha kama lile. Wengine waliamini kuwa huo ulikuwa mwili wa mtu aliyetupwa mtoni. Lakini ishara iliyoonyeshwa na mkono huo iliwafanya wananchi waamini kuwa huo ulikuwa mkono wa ajabu. Katika kiza kinene kilichozunguka ndani ya vichwa vya wananchi, habari zikamfikia Mfalme wao, naye akafika haraka eneo la tukio. Mfalme wa nchi hiyo baada ya kujiridhisha k
Comments
Post a Comment