MAXIMO ALIWASAIDIA SIMBA KUPATA SARE NA YANGA





 Kocha wa Yanga, Marcio Maximo


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, siku chache baada ya mchezo wa mahasimu wa Soka la Tanzania, Yanga na Simba, mashabiki wa Klabu ya Yanga wamemwaga shutuma nzito kwa Kocha wao Marcio Maximo, kuwa alichangia kwa kiasi kikubwa timu yao kutoa sare ya bila kufungana na Simba.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati mchezo ukiendelea na baada ya mchezo huo, Yanga wenye kikosi bora kuliko wapinzani wao Simba, walitegemea kupta matokeo mazuri, lakini badala yake timu hizo zikatoka sare tasa.

Salmu Rupia kutoka Zanzibar, alikuwa wa kwanza kulaani matokeo hayo, akisema yamechagizwa na ubishi wa Kocha wao Maximo, aliyewachezesha wachezaji anaowataka yeye, Santana Jaja na Andre Continho, ambao walionyesha kiwango kidogo tofauti na wenzao Simba.

Samwel Kitundu wa Yombo yeye alisema, Simba wana kila sababu ya kushangilia matokeo ya sare, kwani mashabiki wao hawakuwa na matumaini ya kushinda, lakini wakaonyesha kiwango kizuri, kutokana na sehemu ya kiungo ya Yanga kuzidiwa kwa sababu wachezaji hao hawakuwa na msaada.

“Maximo alipaswa kuwaanzisha wachezaji wenye kasi kama Jerrison Tegete anayewajuwa Simba ndani nje na winga mwenye kasi ya ajabu Simon Msuva, ambaye aliingia dakika 20 za mwosho”, alisema Kitundu na kuongeza kuwa lawama zmuendee Maximo kwa ubishi wake.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU