MAXIMO AWATUMIE AKINA TEGETE KUPATA USHINDI


 
KATIKA moja ya Makala zangu kupitia MPIGANAJI, niliwahi kuandika kuwa Kocha wa Yanga, Mbrazil Marcio Maximo, ameisaidia Simba kupata sare dhidi ya Yanga, kwa kulazimisha kuwachezesha wabrazil wenzake, Santos Jaja na Andy Continho.

Ukweli huo ulidhihirika Jumamosi iliyopipa, Ynga ilipocheza na Stand United ya Shinyanga, na kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0, mawili yakifungwa na mshambuliaji nguli wa Yanga, Jerrison Tegete, aliyeingia kabla ya dakika 19, akichukua nafasi ya Jaja.

Hakuna ubishi kuwa Maximo ni Kocha mzuri, lakini kulazimisha kuwatumia wachezaji hao kila mchezo kunaifanya timu kuzidiwa kutokana na aina ya uchezaji wao kwani hawakabi adui, isipokuwa wanasubiri kuletewa mipira ili wafunge.

Wakati umefika kama Kocha Maximo anataka kuwafurahisha wapenzi na mashabiki wa Yanga, awatumie Tegete, Hussen Javu na Nizar Khalfan, ambao kutokana na umakini wao uwanjani, wanaweza kuisaidia timu kushinda mchezo wowote.

Tegete ni aina ya mshambuliaji anayetakiwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Yanga, kwani msimu uliopita pamoja na kucheza mechi sita tu, tena akitokea benchi, aliweza kufunga mabao 6, tofauti na wenzake Didie Kavumbangu aliyehamia Azam, alifunga mabao 7 pamoja na kucheza mechi karibu zote 23.

Kwa mahesabu ya haraka, kama Kocha Maximo ataacha upendeleo kwa Jaja na Continho, awatumie japo kipindi cha akina Tegete, Nizar Khalfan na Hussen Javu, watawafunika kabisa wabrazil hao.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU