YANGA, SIMBA NANI JEURI YA MWENZAKE UWANJA WA TAIFA LEO

Na Nyakasagani Masenza

UNAWEZA kusema nani jeuri leo, unapozungumzia mchezo wa leo kati ya mahasimu makubwa wa soka la Tanzania Yanga na Simba, zenye mashabiki wengi, lawama kwa makocha na waamuzi husika, Zinashuka dimbani Taifa leo kila mmoja akikamia kushinda mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mchezo huu unasimamiwa kwa sheria kumi na saba za soka, ambazo pamoja na waamuzi wengi kuzisimamia kwa umakini mkubwa zaidi, lakini minung’uniko hutawala hususan kwa timu zinazopoteza mchezo.

Tanzania kama yalivyo Mataifa mengine duniani, inazo timu za soka zinazoshiriki ligi za madaraja mbalimbali, kuanzia Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na ile ya Zanzibar hadi ligi za madaraja ya chini.

Oktoba 18 leo Alasiri, mahasimu wakubwa wa soka la Tanzania, Yanga Afrika kutoka Jangwani, wakiwa chini ya Mwalimu mhamasishaji Mbrazil Marcio Maximo, watashuka uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuonyeshana umwamba na Simba Sport Klabu ya Msimbazi, chini ya kocha mwenye rekodi nzuri, Mzambia Patrick Phiri kuwania pointi tatu muhimu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Ni vigumu kutabiri mshindi wa mchezo huo, ambao kwa mara ya kwanza utawakutanisha wachezaji wawili waliozusha gumzo kubwa katika usajili, Mbrazil Santos Santana Jaja na Mganda Emanuel Okwi, ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitamba kuonyesha maajabu kuwa watazifungia timu zao mabao muhimu.

Yanga ndio wenye kikosi bora msimu huu, ikiwa imesheheni wachezaji wenye uwezo mkubwa, kama Nahodha Nadir Haroub ‘Canavaro’, Mnyarwanda Haruna Niyonzima, Mrisho Khalfan Ngassa, Mbuyu Twite, Jaja na Hassan Dilunga, Continho na Simon Msuva.

Simba pia inaundwa na kikosi cha wachezaji wenye uwezo na kasi ya kushindana kama Emmanuel Okwi, Amis Tambwe, Ramadhan Singano, Jonas Mkude, Shaaban Kisiga, Joseph Owino na Amri Kiemba. Japokuwa timu hiyo imekuwa haifanyi vizuri msimu huu kwa matokeo ya sare mfululizo, inaweza kufanya maajabu pia.

Ni vigumu kutabiri matokeo ya mchezo wa leo kutokana na rekodi za timu hizo, Yanga ilikuwa na rekodi nzuri wakati wa Abbas Guramali na Mohamed Vilan Babu, wote marehemu, wakiifunga Simba watakavyo, hatmaye mambo yakabadilika Simba nao wakaanza kulipa kisasi.

Simba wanaweza kuwa na nafasi kubwa ya kushinda mchezo wa leo kutokana na hali halisi ya mchezo. Ni rahisi Simba kuwatumia wachezaji wao wa zamani walioko Yanga kupata ushindi, japokuwa ni vigumu kuamini hilo. Ndani ya Yanga kuna wachezaji waliosajiliwa kutoka Simba, Juma Kaseja na Kelvin Yondani.

Kama nilivyowahi kusema siku za nyuma, mchezo wa Yanga na Simba huchezwa kwa mbinu za hapa na pale, lakini Yanga ndio waathirika wakubwa, kwani hucheza uwanjani wakiwa pungufu, huku wenzao Simba wakiwa zaidi. Wakisaidiwa na wenzao ndani ya Yanga.

Kimtazamo Simba hawana ubavu wa kushindana na Yanga, baadhi ya mashabiki wamekuwa wakiangalia matokeo ya awali ya timu hizo, ambapo Yanga wameshinda mara mbili dhidi ya Prison ya Mbeya na JKT Ruvu na kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Mtibwa mkoani Morogoro.

Simba hajapoteza mchezo, lakini imepata sare tatu Uwanja wa Taifa Dar es Saslaam, wakianza kupata mabao ambayo hayadumu dhidi ya Coastal Union ya Tanga 2-2, Polisi Morogoro 1-1 na Stand United ya Shinyanga 1-1. Matokeo ambayo yanaongeza hofu na ushindani katika mchezo wa leo.

Macho na masikio ya mashabiki wa soko yanaelekezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam leo, huku tegemeo la timu hizo ni washambuliaji wawili tegemeo, Jaja kwa upande wa Yanga na Okwi Simba.

Katika mchezo wa mwisho kwa timu hizo zilitoka sare kwa kufungana bao 1-1, Simba wakitangulia kupata bao lililofungwa na ….. Yanga walisawazisha kupitia kwa Simon Msuva.


KIKOSI CHA YANGA KINACHOSHUKA UWANJA WA TAIFA LEO, DAR ES SALAAM LEO KULINDA HESHIMA YA WANA JANGWANI DHIDI YA WENZAO WA MSIMBAZI
 KIUNGO MSHAMBULIAJI TEGEMEO LA YANGA HARUNA NIYONZIMA

KIKOSI CHA SIMBA KINACHOSHUKA DIMBANI LEO KUONYESHANA KAZI NA YANGA

MSHAMBULIAJI MSUMBUFU WA SIMBA EMMANUEL OKWI, ALIYETAMBA KUIFUNGA YANGA LEO
 JAJA WA YANGA AKIONYESHA VITU VYAKE UWANJANI
 AMISI TAMBWA WA SIMBA
 MAKOCHA WA YANGA
MAKOCHA WA SIMBA

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU