MIGUU YA
NYOTA
II
Willy
alipofika kwenye nyumba ya Luteni Biniga taa za ndani zilikuwa zikiwaka. Nyumba
hii ilikuwa imezungushiwa ua kama alivyokuwa ameelezwa na Col. Rwivanga. Badala ya
kubisha hodi langoni aliamua kupita kwenye uchochoro, akapanda ukuta kisha
akatumbukia ndani. Alitambaa chini kwa chini mpaka akaufikia ukuta wa nyumba
hii. Dirisha la nyuma lilikuwa limefungwa, hivyo aliendelea kuambaa na ukuta.
Ndipo aliposikia sauti za watu wakizungumza na kucheka. Alichungulia dirishani
na kuwaona watu watatu. Wanaume wawili na mwanamke mmoja. Mazungumzo yao
yalikuwa kwa lugha ya Kifaransa, ambayo Willy aliielewa vizuri sana, mazungumzo
yao ndiyo yaliyomshitua na kumweka chonjo.
"Kazi
mimi nimeifanya kwa ustadi mkubwa. Hiyo pesa kweli iko kwenye akaunti yangu
Nairobi?", mmoja wa wale vijana alimwuliza yule mwanamke.
"Siyo
wewe tu, nyote kesho pigeni simu kwenye benki zenu. Mambo safi. Nimeelezwa na
wakala wa mlipaji kuwa pesa zimetumwa kwa njia ya 'swift' na tayari ziko kwenye
akaunti zenu", yule mwanamke alijibu.
"Mimi
nilihitaji kulipwa dola laki moja. Ndizo zilizotumwa na kuwekwa kwenye akaunti
yangu?", yule mwanaume wa pili aliuliza.
"Ndio.
Sasa kwenye akaunti yako kuna dola laki tatu. Zimeingia pamoja na zile za
malipo ya kuwatorosha wale makamanda wa Intarahamwe kwenda Zaire", yule
mwanamke alijibu.
"Kama
kesho nikijuwa pesa yangu yote hiyo iko benki, basi mimi nitatoroka kwenda
Kenya. Halafu Afrika Kusini. Sitaki kukaa hapa tena, tusije tukabainika kuwa
tuko kwenye upinzani", mwanaume wa pili alisema.
Hapa Willy
aliamini kuwa wakati wa kukabiliana ana kwa ana na watu hawa ulikuwa umefika
kwani walionekana kana kwamba wanataka kuondoka. Mawazo na akili ya Willy
yalivutika sana kwa yule mwanamke kuliko hata kwa wale wanaume wawili ambao
alihisi ni Luteni Silasi Biniga na Juvinali Mukama. Alipogeuka tu kutaka kwenda
kubisha hodi kwenye mlango wa mbele, alijikuta akiuangalia mtutu wa bunduku
kubwa aina ya 'Sub Machine Gun'.
"Usisogee
hata hatua moja. Hapohapo ulipo weka mikono yako juu, geuka nyuma na utembee
kuelekea mlango wa mbele ya nyumba hii", Willy alimrishwa na yule askari
na kutii amri kama alivyokuwa ameamriwa.
"Nani
huyo tena", Silasi Biniga aliuliza katika hali ya mshangao.
"Nini
Ananie", Juvinali naye aliuliza.
"Inkotanyi",
Ananie alijibu.
"Bibiane
wewe nenda. Sisi ngoja tujuwe huyu mtu ni nani?", Juvenali alimweleza yule
mwanamke huku yeye na Luteni Biniga wakichukuwa bastola zao na kutoka nje
kwenda kumkabiri mtu huyu aliyekuja kuwapeleleza ili kabla hawajamuua wajuwe ni
nani na anajuwa nini kuhusu wao. Wakati Bibiane anatoka ndani alikutana na Willy
pamoja na mtu aliyemkamata, wakiwa wamefika mbele ya nyumba, kwenye mlango wa
mbele.
"Simama
hapo", Ananie alimwamru Willy huku akiwa bado ameweka mikono yake
kichwani. Bibiane alipotoka nje alimwangalia Willy. Willy naye akamtazama.
Kulikuwa na mwanga wa kutosha kuweza kumtambua mtu. Bibiane alimwemweseka kwa
Willy kisha akalekea kwenye lango kubwa la kutokea nje na kutokomea gizani.
"Luteni
Biniga..., lazima mtu huyu ni Inkotanyi, amekuja kupeleleza kuhusu tukio la
leo", Ananie alimwambia Luteni Biniga walipotoka nje pamoja na Juvinali.
Luteni Biniga alimwangalia Willy na kwa sura yake akabaini kuwa mtu huyu hakuwa
Mnyarwanda. Bila kuchelewa Luteni Biniga alimpiga Willy kwa kitako cha bastola
kwenye paji la uso na Willy akaanguka chini. Alipoanguka Juvinali naye alimpiga
teke la tumboni. Willy alipotaka kuinuka alipigwa teke la ubavuni. Ni hapa
ambapo mambo yaligeuka. Baada ya Juvinali kutupa teke kali lililompata Willy
vilivyo ubavuni. Willy akahisi amevunjika mbavu, kama sumaku.
Willy
aliunasa mguu wa Juvinali kabla haujarudi na kuupinda, kisha akauvuta upande
wake, haraka sana akamlalia juu. Hii yote ilitokea kwa haraka mno kiasi cha
kuwatatanisha Luteni Biniga na Ananie wasijuwe wafanye nini kwani wangefyatua
risasi wangemuua Juvinali. Bastola ya Juvinali ilianguka chini karibu yao. Tena
kwa kutumia nguvu zote alizokuwa nazo Willy alimrusha Juvinali kwa Ananie
aliyekuwa kama hatua mbili kutoka pale walipokuwa. Juvinali akamkumba Ananie,
wakaanguka huku bunduki ya Ananie ikitema risasi zilizomwingia Juvinali na
kumwua hapohapo.
Wakati Willy
alipomrusha Juvinali kwa Ananie. Haraka aliirukia ile bastola na kumpiga risasi
kadhaa Luteni Biniga. Kabla hajafyatua bastola yake, risasi zikampata Luteni
Biniga kwenye paja la uso na kumwua pale pale. Ananie naye kwa kutumia nguvu
zake zote. Alijaribu kuitoa maiti ya Juvinali ili aichukuwe tena bunduki yake.
Lakini hakuwahi. Willy alimpiga tena teke la kichwa na kumtoa fahamu. Willy
akaivuta maiti ya Juvinali na kuitoa juu ya Ananie na kuanza kumvuta Ananie ili
aweze kumuuliza maswali. Mara akasikia mlio kama wa king'ola. Akajuwa ama yule
mwanamke ameripoti au ule mlio wa bunduki na bastola umesikika. Hivyo akajuwa
angekutwa pale, kwa hasira aliivunja shingo ya Ananie na kumtupa chini.
Akakimbilia ukutani. Akauparamia ukuta na kuangukia kwenye uchochoro wa mtaa wa
pili; akakimbilia kwa Col. Rwivanga.
Alipoingia
nyumba ya Col. Rwivanga. Ndipo Col. Rwivanga alipojuwa kuwa alipokuwa ameumia
sana. Col. Rwivanga alikuwa ameusikia mlio wa bunduki lakini kwa Kigali halikuwa
jambo la ajabu, ingawa alikuwa na wasiwasi. Lango la ua wake lilipofunguliwa tu
alikuwa nje na ndipo alipomwona Willy akiingia huku akipepesuka. Col. Rwivanga
alimsaidia wakaingia ndani. Willy alikuwa anatoka damu puani, Col. Rwivanga
akajuwa kuwa alikuwa ameumia sana maana alipoonekana kama ana nyuso mbili kwa
vile paji lake lilikuwa limevimba vibaya sana.
"Utadhani
umekanyagwa na trekta", Col. Rwivanga alisema baada ya kumwona Willy.
"Nakwambia
ni zaidi ya trekta. Sijawahi kupigwa teke lenye nguvu kama lile", Willy
alijibu.
Dkt. Daniel
Robinson alikuwa daktari mkuu wa Hospitali ya King Faisal mjini Kigali na
alikuwa rafiki mkubwa wa Col. Rwivanga kabla Dkt. Robinson hajaja Rwanda
alikuwa daktari katika Hospitali ya Mulago mjini Kampala, ambako alikuwa
akiishi karibu na Col. Rwivanga. Na kwa muda wote walipokuwa Kampala walikuwa
marafiki wa karibu sana.
Kwa hivyo
wakati RPF walipoingia tu Kigali, Col. Rwivanga ndiye aliyekuwa kiongozi wa
kikosi cha kwanza kabisa kilichoongoza mapambano dhidi ya majeshi ya serikali.
Na kituo cha kwanza kabisa ni kuwaokoa watu waliokuwa Hospitali ya King Faisal
ambako kuliwa na maelfu ya watu wakiwa pamoja na rafiki yake Dkt. Robinson.
walikuwa wamejisalimisha ndani ya Hospita, lakini baada ya Intalahamwe kuwa wamewaua
watu wengi Hospitali hapo pamoja na wagonjwa.
Baada ya
Col. Rwivanga kuingia na kikosi cha kulinda usalama, watu wengi walipona. Siku
zilizofuata majeruhi na wengineo aliponea katika Hospitali hiyo, hivyo Col.
Rwivanga alimpigia simu Daktari Robinson ambaye ni Mzungu Mwingereza na
kumweleza juu ya Willy kujeruhiwa.
"Niko
njiani!", Dkt. Robinson alimweleza Col. Rwivangga, wakati walipokuwa
wanamsubiri Daktari, Willy alimweleza Col. Rwivanga yote yaliyotokea nyumbani
kwa Luteni Silas Biniga.
"Nini maana
ya Inkontanyi?, maana waliniita hivyo", Willy aliuliza baada ya kumaliza
maelezo yake.
"Inkontanyi
huwa ina maana ya RPF. Maana yake hasa ni mpiganaji mkali na maarufu katika
Kinyarwanda. Lilikuwa ni jina lililopewa kikosi kimoja cha Mfalme wa Bugiri
katika karne ya kumi na tisa hivyo. Walihisi kuwa wewe utakuwa ni mpelelezi wa
RPF", Col. Rwivanga alieleza.
"Kwa
hiyo. Inamaana wao siyo RPF", Willy aliuliza.
"Bila
shaka, kama ulivyosikia na hili limenitia wasiwasi sana kutambua kuwa katika
uongozi wa katikati. Na bila shaka wa juu wa RPF tumeingiliwa na wasalti.
Kinachoonekana wazi ni kuwa hawa waliopambana nawe nao ni watu wanaofanya hivi
vitendo ni wapenda pesa. Sasa mtu au kikundi hatari ni kile kinachotoa pesa
hicho ndicho yafaa tukijuwe na kukiangamiza ili Rwanda iweze kurudi hali yake
ya amani", Col. Rwivanga alijibu.
"Basi
mtafute yule mwanamke niliyesikia wakimwita Bibiane na jibu lako utakuwa
umelipata", Willy alijibu huku akionekana kuwa maumivu yalikuwa yamezidi.
Mara akasikia honi ya gari.
"Daktari
huyo rafiki yangu, ngoja utubiwe usife maana kazi sasa ndiyo imeaanza",
Col. Rwivanga alimtia moyo Willy.
ITANDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment