UCHU

GISENYI

IX

Meja Kasubuga baada ya kuachana na Willy Gamba, alimtafuta Col. Rwivanga akitumia simu ya Satellite na kumweleza kuwa Willy alikuwa amefika salama na kwamba Willy na Bibiane walipanga kuelekea Kibumba usiku uleule.

Col. Rwivanga alifurahi kupata simu ya Meja Kasubuga lakini akakataa Willy na mwenzake wasiondoke, "Hapana mwambie Willy na mwenzake wasiondoke mpaka kesho, kuna mabadiliko ya mipango ya kazi huku, waambie wapumzike tu hakuna tatizo. Meja Tom Kabalisa atakuja kumuona Willy kesho asubuhi, nami nitafika huko kesho asubuhi. Hivyo, mambo yote tutapanga kesho baada ya sisi kufika huko".

"Nimekusoma, nitamweleza kuhusu taarifa hii afande".

Kasubuga aliona si vyema kumweleza Willy wakati ule, bali amwache mpaka baadaye ili apumzike kidogo, lakini muda si mrefu alikuja askari mmoja na kusema kuwa wale wageni wa Msalaba Mwekundu walikuwa wakihitaji chakula. Meja Kasubuka akaona huo ulikuwa muda mwafaka vilevile kuwaeleza kuhusu maagizo kutoka kwa Col. Rwivanga. Hivyo, akaamua yeye mwenyewe ndiye awapelekee chakula kitakapokuwa tayari ili awaeleza kama alivyoagizwa.

"Chakula kilipokuwa tayari Meja Kasubuga aliwapelekea yeye mwenyewe na kuwaeleza kuhusu maagizo aliyopewa kutoka kwa Col. Rwivanga.

"Sawa tumekusikia", Willy alijibu bila kuonyesha kama alikuwa na maana gani au alipanga kufanya nini usiku ule.


ITAENDELEA 0784296253

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU