Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Bw. Adam Kimbisa, alipotua mjini humo leo asubuhi kwa ajili ya ziara ya siku tisa ya kikazi. Akiwa mkoani Dodoma, Kinana anatarajiwa kukagua na kuhimiza miradi ya wananchi pamoja na kuangalia uhai wa chama.
Katibu Mkuu Kinana
akisalimiana kwa kukumbatiana na Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Luteni Mstaafu Chiku Galawa kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma leo. Kushoto ni
Katibu Mkuu wa CCM wa Mkoa huo, Bw. Albert Mgumba
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Dodoma baada ya timu ya kazi ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana kuwasili Dodoma leo
Katibu Mkuu wa CCM akizungumza na baadhi ya wanachama wa CCM waliofika kwenye Uwanja wa ndege wa mjini Dodoma leo kwa ajili ya kumpokea.
Comments
Post a Comment