TIMU YA SOKA YA WAANDISHI WA HABARI WA MWANANCHI COMMUNICATION WALIOTINGA HATUA YA PILI BAADA YA KUWAFUNGA RADIO MARIA TCC KWA MIKWAJU YA PENATI 4-2 KWENYE VIWANJA VYA TCC CHANG'OMBE.
............................................................................................................................................
NAHODHA NA MSHAMBULIAJI WA MWANANCHI COMMUNICATION JULIUS KIHAMPA (KULIA) AKIUTAMANI MPIRA ULIODAKWA NA KIPA WA RADIO MARIA, YONA MNG'ONG'O
MLINZI WA RADIO MARIA FRED WANGAO (KUSHOTO) AKIMLINDA JULIUS KIHAMPA WA MWANANCHI ILI ASIMFIKIE KIPA WAKE. MWANANCHI WALISHINDA KWA PENATI 4-2.
JULIUS KIHAMPA WA MWANANCHI COMMUNICATION AKITAFUTA MBINU ZA KUMTOKA MLINZI WA RADIO MARIA FRED WANGAO, TI,U HIZO ZILIPOCHUANA JANA.
MLINZI KISIKI WA MWANANCHI COMMUNICATION, SALUM JABA (KULIA), AKIMCHUNGA VILIVYO MSHAMBULIAJI WA RADIO MARIA MUSSA JUMA.
WACHEZAJI WA RADIO MARIA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MWAMUZI WA MCHEZO HUO PAMOJA NA NAHODHA WA MWANANCHI MAJUTO OMARI BAADA YA WACHAZAJI WA TIMU HIYO KUTILIWA SHAKA KUWA SI WAANDISHI WA HABARI
MLINZI WA MWANANCHI HATIMU NAHEKA (KUSHOTO) AKIJARIBU KUWAHI MPIRA MBELE YA MSHAMBULIAJI HAMIS NGUMBE WA RADIO MARIA.
KATIBU MKUU WA ZAMANI WA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA (TFF), ANGETILE OSIAH (KULIA) AKIUCHEZEA MPIRA HUKU GERALD MOSES WA RADIO MARIA AKIWA MAKINI
ANGETILE AKITAFUTA MBINU ZA KUMTOKA GERALD MOSES WA
............................................................................................................................................
Na Mwandishi
Wetu
Mashindano
ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa Vyombo vya habari ya ‘NSSF
Media Cup 2015’ yameendelea kuonyesha msisimko na ushindani wa aina yake baada
ya timu vigogo kupata ushindi na zingine kuondolewa katika michezo ya awali.
Mashindano
hayo yanafanyika wakati wa wiki ya Huduma Kwa wateja wa NSSF ambao watapata
fursa ya kupata elimu kuhusu huduma zinazotolewa na shirika hilo, ambapo
wanachana watapata taarifa za michango yao na wengine wataandikishwa uanachama
wa hiari.
Mashindano
hayo yanayoendeshwa kwa mtindo wa mtoano, yalianza Machi 14, mwaka huu baada ya kuzinduliwa na Naibu Waziri wa Kazi na
Ajira, Makongoro Mahanga kwenye viwanja vya TCC Chang’ombe, Dar es Salaam.
Katika
mchezo wa ufunguzi, TBC ilifanikiwa kuitupa nje Free Media kwa bao 1-0
lililofungwa na Ahamed Salim, nao IPP wakaifungasha virago TSN kwa bao 1-0
lililofungwa na Urio, huku Mwananchi Communition wakatinga hatua ya pili kwa
mikwaju ya penati 4-2 dhidi ya Radio Maria, baada ya timu hizo kutoshana nguvu
kwa bao 1-1.
Katika
mchezo mwingine uliochezwa kwenye viwanja vya TCC, timu ya Azam Tv iliyokuwa
chini ya Kocha wao mwamuzi mkongwe Othman Kazi walikubali kipigo kitakatifu cha
mabao 5-0 kutoka kwa Clouds Media.
Kwenye
viwanja vya Bandari, New Habari walifanikiwa kuwafungisha virago wakongwe wa
michuano hiyo, Business Times kwa mikwaju ya penaali, nao Habari Zanzibar wakafanikiwa
kuwashinda Radio Heri 3-0.
Hadi
tunakwenda mitamboni timu za NSSF na Jambo Leo zilikuwa zikichuana vikali
kwenye viwanja vya TCC kuwania nafasi ya kusonga mbele, wakati Uhuru
Communication nao wakionyesha umwamba na Sahara Media.
Kupitia
mashindano hayo, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Salim Kimaro amewataka
wanachama wa shirika hilo waishio Dar es Salaam kufika kwa wingi kwenye viwanja
vya TCC kujua maendeleo mafao yao.
NAHODHA NA MSHAMBULIAJI WA MWANANCHI COMMUNICATION JULIUS KIHAMPA (KULIA) AKIUTAMANI MPIRA ULIODAKWA NA KIPA WA RADIO MARIA, YONA MNG'ONG'O
MLINZI WA RADIO MARIA FRED WANGAO (KUSHOTO) AKIMLINDA JULIUS KIHAMPA WA MWANANCHI ILI ASIMFIKIE KIPA WAKE. MWANANCHI WALISHINDA KWA PENATI 4-2.
JULIUS KIHAMPA WA MWANANCHI COMMUNICATION AKITAFUTA MBINU ZA KUMTOKA MLINZI WA RADIO MARIA FRED WANGAO, TI,U HIZO ZILIPOCHUANA JANA.
MLINZI KISIKI WA MWANANCHI COMMUNICATION, SALUM JABA (KULIA), AKIMCHUNGA VILIVYO MSHAMBULIAJI WA RADIO MARIA MUSSA JUMA.
WACHEZAJI WA RADIO MARIA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MWAMUZI WA MCHEZO HUO PAMOJA NA NAHODHA WA MWANANCHI MAJUTO OMARI BAADA YA WACHAZAJI WA TIMU HIYO KUTILIWA SHAKA KUWA SI WAANDISHI WA HABARI
MLINZI WA MWANANCHI HATIMU NAHEKA (KUSHOTO) AKIJARIBU KUWAHI MPIRA MBELE YA MSHAMBULIAJI HAMIS NGUMBE WA RADIO MARIA.
KATIBU MKUU WA ZAMANI WA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA (TFF), ANGETILE OSIAH (KULIA) AKIUCHEZEA MPIRA HUKU GERALD MOSES WA RADIO MARIA AKIWA MAKINI
ANGETILE AKITAFUTA MBINU ZA KUMTOKA GERALD MOSES WA
Comments
Post a Comment