KASHESHE
XV
Meja
Kasubuga alipigana vikali na jeshi la Luteni Nyamboma na kufanikiwa kuwazidi
nguvu na hivyo askari wa jeshi hilo walilazimika kukimbilia mpakani. Luteni
Nyamboma alikuwa amepoteza askari wengi sana, walipfika mpakani wakitegemea
kumkuta Nkubana ili awaongezee nguvu ya askari warudi kuendeza mapambano,
lakini hakumkuta Nkubana. Hivyo, Luteni Nyamboma akaamua kuelekea Kibumba na
masalia ya askari wa kikosi chake waliobaki. Luteni Nyamboma alipoangalia saa
yake ilikuwa saa nane usiku. Walitumia magari waliyoyakuta pale mpakani, Luteni
Nyambona na askari wake waliondoka kuelekea Kibumba.
Hata hivyo,
Luteni Nyamboma alilazimika kuwaacha askari wa jeshi la Zaire pale mpakani kwa
ajili ya ulinzi ili baada ya kazi ya Gisenyi Luteni Nyamboma awafuiate Kibumba.
Meja
Kasubuga alipofika mpakani aliyaona magari yanaondoka kasi eneo la mpakani.
Meja Kasubuga akagundua kuwa magari yale yalikuwa yakielekea Kibumba.
Asingekuwa ameamriwa na Col. Rwivanga awasubiri pale mpakani hakika Meja
Kasubuga angeyafuata magari yaliyoondoka na kikosi kile. Baada ya kufika
mpakani, jeshi la Meja Kasubuga lilifanikiwa kukitwaa kikosi cha jeshi la Zaire
kilichokuwa kikiwasaida wanajeshi la Intarahamwe na hii ikawa ngome ya jeshi
lake kwa muda.
Kikosi hiki
kilichokuwa mpakani mwa Zaire na Rwanda kilikuwa kimejijenga vizuri kivita,
kikiwasaidia wanajeshi wa Intarahamwe na kundi la Akazu lililokuwa likifanya
jitihada ya kuivamia serikali ya RPF ili kutwaa madaraka ya kuiongoza Rwanda
kijeshi.
Baada ya
kuhakikisha usalama wa eneo hili, Meja Kasubuga alielekea sehemu iliyoandaliwa,
ambayo Col. Rwivanga alimweleza kuwa angetua hapo kwa Helikopta akiwa na
kiongozi wa kikundi cha Banyamulenge na kiongozi wa vikosi vya vyama
vinavyoipinga serikali ya Zaire. Meja Kasubuga alipoangalia saa yake ilikuwa
saa nane na dakika kumi. Muda ambao Col. Rwivanga aliahidi kuwa atafika
Gisenyi. Hivyo, Meja Kasubuga na kikosi chake wakaamua kusubiri.
Col.
Rwivanga alikuwa na matumaini makubwa na kikosi cha Meja Kasubuga, hivyo baada
ya kuondoka Kigali kwa Helikopta ya jeshi, walisafiri moja kwa moja usiku huo
kuelekea Gisenyi. Col. Rwivanga hakuwa na papala wakati wote alikuwa
akitafakari jambo kabla ya kulifanyia kazi. Alikuwa mmoja wa maofisa wa jeshi
walioheshimiwa na kutegemewa sana na serikali ya Rwanda. Alikuwa mtu mwadilifu
asiyependa kuisalti nchi yake, kutokana na msimamo wake dhabiti aliogopwa sana
na vibaraka hususan wanaotaka kuigawa Afrika.
Alikuwa
akijitosheleza kiulinzi, kutokana na hali hiyo nyumba yake haikuwekewa ulinzi
kutoka jeshini, kama ilivyo kwa maofisa wengine wa ngazi za juu kama yeye.
Alikuwa mmoja wa makomandoo wa jeshi waliofuzu vizuri mafunzo yake, lakini
kutokana na cheo chake jeshini alibaki kuwa ofisa wa jeshi aliyeheshimiwa sana.
Alikuwa mpole asiyependa makuu, alikuwa na subira, hata ukimchoma kidole
machoni hatakufanya kitu. Lakini akilazimika kuchukuzwa na upuuzi alifanya kitu
ambacho hakuna awezaye kuamini, hakuwa na mchezo tena. Huyo ndiye Col. Thomas
Rwivanga, Afisa wa jeshi mwandamizi.
ITAENDELEA 0784296253
Comments
Post a Comment