KASHESHE
XVII
Col.
Rwivanga, Mpinda na Meja Tom Kabalisa waliwasili mpakani mwa nchi za Rwanda na
Zaire katika sehemu waliyokuwa wamekubaliana na Meja Kasubuga mnamo saa nane na
dakika arobaini usiku.
Hali ya
usalama ilikuwa imeimalishwa katika eneo hili, ambapo vijana wa Meja Kasubuga
walikuwa makini kwa kila jambo, baada ya Helikopta ya jeshi la Rwanda
waliyosafiri hadi mpakani kutua, Col. Rwivanga alikuwa wa
kwanza kushuka akifuatiwa na Mpinda, kasha Meja Kabalisa.
"Mambo
yakoje hapa", Col. Rwivanga alimuuliza Meja kasubuga wakati wakisalimiana
baada ya heshima ya kijeshi.
Meja
Kasubuga alieleza kwa urefu jinsi mapambano yalivyokuwa, kisha akamalizia,
"Huyu Willy atakuwa kauawa kule Kibumba maana kajipeleka mahali ambapo
panatakiwa vikosi vyote husika, huyu Willy ingawaje Afande unamsema ni hatari
lakini hana akili ya tahadhari, angesubiri twende wote, ndipo angeweza kuwa
msaada kwetu maana maiti haina msaada wowote.
"Nakubaliana
na wewe lakini yule ni mtu mwenye maisha mengi, unaweza kumuona kaibuka",
Col. Rwinga alisema wote wakacheka kwa utani huo.
"Kweli,
akiibuka tena atakuwa mtu wa maisha mengi", Meja Tom Kabalisa wa
Banyamulenge alijibu kwani na yeye alijua nguvu za Intarahamwe kule Kibumba na
ndio sababu alikuwa hajathubutu kufanya lolote. Kisha akaendelea. "Col.
Rwivanga, nafikiri sasa tumweleze Meja Kasubuga mipango ikoje ili....",
Kabla Meja Kabalisa hajamaliza kusema sentesi yake, mripuko mkubwa usio kifani
ulisikika mpaka huko walikokuwa.
"Ooh
Willy Gamba, kweli u-hatari", Meja Kasubuga aligwaya.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment