SURA YA TATU IV
"Anakuja!
Na atakufa!" Proper alimwambia Waridi.
"Ondoa
hiyo mikunjo ya hofu usoni uvae suruali yako nzuri kama ilivyo. Akifika mpe
tabasamu, mpe mapenzi, kisha mkaribibishe pombe. Usisahau chupa hilo hapo ni
kwa ajii yake, akionja tu yamekwisha, asipoinywa mpake hii kwa hila".
Walikuwa
katika chumba fulani, ghorofa fulani, katika jumba hili la light ambalo liko
katika mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam. Proper alikodi chumba hiki kwa
ajili ya kazi hii tangu jana alipomtoa Waridi kule hospitali. Usiku mzima
aliutmia kumtisha Waridi kwa kila namna pale alipojaribu kuleta ubishi. Kisha
alikuwa amemlazimisha kufanya naye mapenzi kwa njia zake za kinyama. Ilipofika
alfajiri ndipo wakaanza kupanga mikakati ya mauaji.
Waridi
alivishwa vazi jeupe la hariri, vazi hili lilifichua kila kitu kilichofaa
kifichwa katika mwili wake. Kila jicho liliweza kuona mwili mzuri wa msichana
huyo, ulikuwa ukimelelemeta kwa wekundu ndani ya mavazi hayo. Uso wake pia
ulikuwa "kioo" kwa uzuri wake wa asili ulioshinikizwa kwa vipodozi
murua vilivyotumiwa kistaarabu. Nywele zake zilitengenezwa kwa ile mitindo ya
kisasa. Kwa kila hali, msichana huyu alionekana mtu tofauti kabisa na yule
binti ambaye usiku wa jana tu alilala chini pale baa akiwa nusu uchi, akilia.
Huyu alikuwa katika hali ambayo ilikusudiwa na ilitosha kuushinda ukaidi wa
Joram Kiango dhidi ya wasichana warembo.
"Uwe
msichana hodari. Ni kazi ndogo tu. Baada ya hapo utakuwa huru. Nitakulipa pesa
za kutosha ukanisubiri Nairobi. Kutoka hapo tutakwenda zetu London au New York,
tukatumie. Unasemaje?".
Waridi
hakujibu.
"Mbona
husemi neno?" Proper alimwuliza Waridi. "Hofu ya nini? Hii ni kazi
ndogo mno kuliko ile uliyoifanya kwa Bomba. Na bado itakulipa pesa nyingi zaidi
ya ule uchafu uliochukua. Jitie furaha na ucheke kidogo".
Kikcheko
kilikuwa mbali na Waridi. Aliendelea kuduaa kama mzoga akisubiri lolote
aliloelekezwa kulifanya. Hilo likamchukiza sana Proper.
Akasema.
"Sikia wewe, endapo utavuruga tena mpango huu, sitasita kukuua papa hapa.
Sasa hivi bado dakika ishirini Joram ataingia hapa. Nitakuwa chumba cha pili nikiangalia
kila kitu. Ukishindwa au kuvuruga mpango huu nitakuua wewe na huyo Joram papa
hapa. Nitakuua wewe kwanza na kisha Joram kwa hili hapa", akatoa bastola
ndogo kutoka kwenye mfuko wa koti lake.
"Sipendi
kukuua", Proper aliongeza. "Lakini ukinilazimisha nitaitumia
kuwaua". Akaitazama tena saa yake. "JOram anaweza kuwa anakuja sasa.
Natoka. Kumbuka kuwa niko karibu na tayari kukuua endapo utavuruga mpango huu.
Sawa? Proper alitoka na kumwacha Waridi ameduwaa kama alivyokuwa.
Baada ya
dakika kadhaa mlango wa chumba hiki uligogwa, kisha ukafunguliwa. Joram Kiango
alichungulia ndani na kisha kuingia polepole macho yake yakiwa yamepumbazwa na
uzuri wa Waridi. Hakutegemea.
"Sisiter...
mimi ni mgeni wako nadhani. Naitwa Joram Kiango", alieleza Joram huku akiandaa
tabasamu ambalo alijua linamfaa binti mzuri kama huyu.
Ndipo Waridi
alipogeuka kumtazama.
ITAENDELEA
0784296253
Comments
Post a Comment