SURA YA TANO
Nyumba hii iliyobomolewa kwa bomu ilikuwa katika mtaa wa Manda Magomeni Mikumi. Ilikuwa nyumba ambayo kwa muda mrefu haikutumiwa kutokana na kutokamilika kwake tu. Joram alikuwa ameichagua nyumba hii kwa ajili ya kujificha baada ya kuitazama mara kwa mara kila alipopita katika mtaa huu na kuona ilivyokaa vizuri kwa siri. Ilikuwa imezungukwa na kichaka cha miti ambayo awali ilikusudiwa kuwa bustani. Haikuwa rahisi kwa mtu wa nyumba jirani kufahamu yanayotokea katika nyumba hii kwa jinsi zilivyotengana.
Zaidi, ilikuwa na njia nyingine ya uwani ambayo ilipitia katika uchochoro hadi mitaa ya nje kabisa. Kuhamia hapa ilikuwa siri yake binafsi ingawa Inspekta Kombara alimsihi sana amfahamishe wapi amejificha, Alikuwa amehamia hapa usiku wa manane baada ya kujipitishapitisha ili kuhakikisha kuwa hafuatwi au kuonekana na mtu. Mzigo wake pekee ulikuwa ni Suitcase yake ambayo ilichukuwa vifaa vyake muhimu ikiwa pamoja na silaha ndogo,
Usiku huo wa kwanza alilala vyema. Alfajiri aliamka na kujiandaa kwa kuvua ujana na kuvaa uzee. Baada ya kukamilisha taratibu za uzee alilificha vizuri begi lake na kutoka hadi polisi ambako alikamilisha mipango yake na kurejea mafichoni akisubiri muda alioupanga ili aanze harakati zake.
Joram alikuwa na hakika kuwa kazi hii isingemchukua muda kuimaliza. Jambo lililomtia matumaini ni kule kujua kuwa adui zake walikuwa wakisubiri kifo chake ili waanze shughuli zao. Kadharika, mmoja kati ya adui hawa hakuwa mgeni kwake. Alichungulia alipokuwa akitoa amri kwa marehemu Waridi na kuipata picha yake. Insingemchukua muda mrefu kumfahamu kikailifu.
Kitu kimoja Joram hakujua. Hakujua kuwa makazi haya ya siri aiyohamia hayakuwa yake binafsi. Yalikuwa malazi ya Luta Magambe, mmoja kati ya mamia ya vijana wazurulao katika Jiji la Dar es Salaam. Luta alikuwa ameingia Jijini miaka zaidi ya kumi iliyopita, akitokea kwao kijijini katika moja wapo ya Wilaya za mkoa wa Kagera. Alikuja Dar es Salaam kwa nia njema ya kutafuta kazi baada ya elimu yake ya msingi. Jiji likamlaki kijeuri kama linavyowalaki wote. Kazi haikupatikana kwani hakuwa na mtu wa kumfanyia "mpango" wala pesa za "motisha".
Akaambulia kuangukia katika vibarua vya kutwa. Pesa alizopata zikawa ndogo mno kulingana na mahitaji ya Jiji. Kila siku akawa mtu wa "Kuchacha". Hilo likamtuma kutumia muda wake wa ziada kuwachomolea wasafiri wa Uda na Daladala. Tabia hiyo haikuchelewa kumfikisha Keko akiwa na majeraha mengi usoni. Alipotoka Keko hakuwa luta mwenye nia njema tena, bali mtu ambaye yuko tayari kufanya lolote mradi apate chochote.
Msimamo huo mpya ulimanya apoteze chumba na kukosa marafiki wa haja. Rafiki zake pekee walikuwa wahuni wenzake na walikutania "kazini". Baada ya "kazi' kila mmoja alijua lake.
Siku alizopata, alistarehe kwa kulewa, kujipatia wasichana wazuri na kulala vizuri katika majumba ya wageni ama kwenye nyumba za wasichana hao. Alipokosa alijutia na kujisahaurisha kwa kuvuta bhandi na kujilaza katika jumba hilo bovu.
Hivyo kwenye alfajiri hiyo aliona kama mwujiza kuona 'mzee' huyu mwenye dalili ya pesa na sura ya Kialhaji akitokea ndani ya moja ya vyumba vya jumba hili akiitumia njia yake ya siri! Mara moja wazo likamjia Luta?. Kwamba mzee huyu alikuja katika ghofu hili kwa sababu maalumu. Sababu ambayo Luta aliamini kuwa haikuwa nyingine zadi ya kuficha pesa au vitu vya thamani, Wazo hilo likamtuma kuanza upekuzi akitafuta chochote ambacho mzee huyo alikificha. Hakupata kitu. Hata hivyo alikuwa bado akiendelea na upekuzi wake 'mzee' aliporejea. Hima akajipenyeza katika chumba cha pili ambamo alijificha vizuri. Joram hakumuona. Darubini ya adui yake Joram kutoka nyumba ya pili pia haikuweza kumuona. Alitulia akimchungulia Joram ambaye aliketi akifanya mambo yake.
Kisha Bagambe alimuona mtu mwigine akinyatia nyumba hii mkononi kashika vitu ambavyo alivificha kwa hadhari chini ya mlango, Baada ya mtu huyo kushika hapa na pale aliondoka eneo hilo kwa hadhari na ukimya ule ule.
Kitu gani kitatokea?, Bagambe alijiuliza, Hakika moja alikuwa nayo. kuwa hii ilikuwa nafasi yake pekee ya 'kuukata'. Kwamba leo lazima ungekuwa mwisho wake wa maisha ya kubahatisha na mwanzo wa maisha mapya. Ingekuwaje vngine na eti bahati zinamfuata hadi huku badala ya yeye kuzifuata kwenye vituo vya basi? Hakuona sababu ya kuendelea kusubiri.
Kwa hadhari mfano wa paka anayemnyemelea panya, aliiendea sehemu hiyo aliyoona kitu kikifichwa. alipofika alipekua taratibu. Kisha aligusa waya fulani ambao hakutarajia kuuona hapo. Aliutazama waya huo kwa mshangao. Mshangao ambao ulikatizwa na mlipuko mkali uliomfanya apae juu na kutua chini akiwa tayari ametawanyika vipande mfano wa nyama za kopo, zinazoandaliwa kwa ajili ya kusindikwa.
Mlipiko huo ulimkuta Joram Kiango akiwa amesimama wima, fimbo mkononi. Aliduwaa alipoona ghafla mtu akizuka mbele yake na kupaa angani ambako alitawanyika vipande vipande. Lakini hakupata muda wa kuendelea kuduwaa, kwani wakati huo huo kila kitu kilikuwa kikipaa na kutua huku na huko kwa kishindo cha kutisha.
Kila kitu pamoja na Joram mwenyewe. Alijikuta angani kisha akajibwaga chini akifuatwa na lundo kubwa la vitu vizito ambavyo vilimfunika juu.
Joram hakuwa na muda wa kusikia maumivu pia. Alihisi kama mtu aliyepoteza kichwa au ubongo. Fahamu zikamtoka na nafsi yake kuchukuliwa na kiza kinachotisha.
Kifo cha kusikitisha! Joram aliwaza hivyo, karibu kila mtu kati ya umati mkubwa uliosimama kando kuizingira nyumba hiyo. Macho yenye hofu na huzuni yalikuwa yakiwatazama askari ambao walikuwa wakiviokota viungo vya marehemu kimoja baada ya kingine na kuvitia katika sanduku. Ni watu wachache sana walioweza kutazama tukio hili kwa muda mrefu. Wengi walitupa jicho kwa sekunde kadhaa na kisha kugeuza nyuso zao upande mwingine huku wakiguna na kufuta machozi. Mama mmoja alisikika akilia kwa sauti.
Ilikuwa mara ya kwanza kwa wengi wao kushuhudia tukio la mtu aliyepoteza maisha kwa njia hii ya kutisha.
Miongoni mwa walioshuhudia tukio hilo alikuwwepo Jodor Proper. Alikuwa mmoja wa watu waliofika mapema katika eneo hilo. Lakini alimkuta mtu wake aliyetega bomu hilo akijifuta vumbi baada ya ule mweleka alioupata kutokana na tofali lililomponda kichwani. Yeye alikuwa mmoja kati ya 'wapita njia' wanne waliojeruhiwa katika ajali hii. Proper alimsaidia mtu huyu kama asiyemfahamu. Walipopata mwanya walinong'onezana: "Kazi nzuri sana, Sasa nenda zako..."
Mtu huyo alipoondoka. Proper aliendelea kutazama 'ajali' huku akijitia kunung'unika. Lakini ndani ya moyo wake alikuwa akisherehekea na kushangilia sana tukio hilo. 'Kifo kinachomstahili kabisa' Aliwaza kwa furaha. "Mnofu mmoja mmoja! Na ajiunge basi tuuone huo ushujaa wake".
Wazo la kwamba huenda huyu akawa si adui yake mkubwa Joram Kiango halikumjia akilini. Ingawa haikuwa njia rahisi ya kuthibitisha mabaki hayo ya marehemu, lakini katika uchunguzi wake Proper alifanikiwa kuiona ile fimbo ya Joram na madevu yake ya bandia ambayo yaliokotwa na askari mmoja na kumwonyesha Inspekta wao ambaye alibabaika kama mtu aliyeguswa na simba. Kitendo hicho kilimfanya Proper ajisikie kucheka huku akijituliza. Wangetangaza nini tena wakati dunia nzima imefahamishwa zamani kuwa Joram Kiago amefariki dunia?.
Proper alipotoka katika eneo hilo kwa tabasamu, alikuwa na wazo moja tu la kuendelea na mipango yao bila kuwa na hofu yoyote. Kikwazo pekee alichoogopa yaani Joram Kiango kilikuwa tayari kimeingia kuzimu, kikiwasalimia babu zake huko.
Mmoja wa maofisa wa polisi alipendekeza wafanye uchunguzi wa kina ili kuhakiki kama eneo hili lilikuwa na maiti ama mareruhi wengine zaidi waliokandamizwa na kifusi. Lakini majirani wa eneo hilo waliwahakikishia polisi kuwa nyumba hiyo haikuwa na watu. Wakaondoka haraka haraka kwani kazi ya kufukua vifudi ilikuwa nzito, ambayo hakika ingewatoa jasho. Wakaondoka na mwili wa marehemu wakiuacha umati wa watu ukiendelea kufika katika eneo hilo kutazama kilichotokea.
Usiku ulipoingia, giza liliwaondoa watu katika eneo hilo likabaki katika hali yake ya kawaida.
ITAENDELEA 0784296253
Nyumba hii iliyobomolewa kwa bomu ilikuwa katika mtaa wa Manda Magomeni Mikumi. Ilikuwa nyumba ambayo kwa muda mrefu haikutumiwa kutokana na kutokamilika kwake tu. Joram alikuwa ameichagua nyumba hii kwa ajili ya kujificha baada ya kuitazama mara kwa mara kila alipopita katika mtaa huu na kuona ilivyokaa vizuri kwa siri. Ilikuwa imezungukwa na kichaka cha miti ambayo awali ilikusudiwa kuwa bustani. Haikuwa rahisi kwa mtu wa nyumba jirani kufahamu yanayotokea katika nyumba hii kwa jinsi zilivyotengana.
Zaidi, ilikuwa na njia nyingine ya uwani ambayo ilipitia katika uchochoro hadi mitaa ya nje kabisa. Kuhamia hapa ilikuwa siri yake binafsi ingawa Inspekta Kombara alimsihi sana amfahamishe wapi amejificha, Alikuwa amehamia hapa usiku wa manane baada ya kujipitishapitisha ili kuhakikisha kuwa hafuatwi au kuonekana na mtu. Mzigo wake pekee ulikuwa ni Suitcase yake ambayo ilichukuwa vifaa vyake muhimu ikiwa pamoja na silaha ndogo,
Usiku huo wa kwanza alilala vyema. Alfajiri aliamka na kujiandaa kwa kuvua ujana na kuvaa uzee. Baada ya kukamilisha taratibu za uzee alilificha vizuri begi lake na kutoka hadi polisi ambako alikamilisha mipango yake na kurejea mafichoni akisubiri muda alioupanga ili aanze harakati zake.
Joram alikuwa na hakika kuwa kazi hii isingemchukua muda kuimaliza. Jambo lililomtia matumaini ni kule kujua kuwa adui zake walikuwa wakisubiri kifo chake ili waanze shughuli zao. Kadharika, mmoja kati ya adui hawa hakuwa mgeni kwake. Alichungulia alipokuwa akitoa amri kwa marehemu Waridi na kuipata picha yake. Insingemchukua muda mrefu kumfahamu kikailifu.
Kitu kimoja Joram hakujua. Hakujua kuwa makazi haya ya siri aiyohamia hayakuwa yake binafsi. Yalikuwa malazi ya Luta Magambe, mmoja kati ya mamia ya vijana wazurulao katika Jiji la Dar es Salaam. Luta alikuwa ameingia Jijini miaka zaidi ya kumi iliyopita, akitokea kwao kijijini katika moja wapo ya Wilaya za mkoa wa Kagera. Alikuja Dar es Salaam kwa nia njema ya kutafuta kazi baada ya elimu yake ya msingi. Jiji likamlaki kijeuri kama linavyowalaki wote. Kazi haikupatikana kwani hakuwa na mtu wa kumfanyia "mpango" wala pesa za "motisha".
Akaambulia kuangukia katika vibarua vya kutwa. Pesa alizopata zikawa ndogo mno kulingana na mahitaji ya Jiji. Kila siku akawa mtu wa "Kuchacha". Hilo likamtuma kutumia muda wake wa ziada kuwachomolea wasafiri wa Uda na Daladala. Tabia hiyo haikuchelewa kumfikisha Keko akiwa na majeraha mengi usoni. Alipotoka Keko hakuwa luta mwenye nia njema tena, bali mtu ambaye yuko tayari kufanya lolote mradi apate chochote.
Msimamo huo mpya ulimanya apoteze chumba na kukosa marafiki wa haja. Rafiki zake pekee walikuwa wahuni wenzake na walikutania "kazini". Baada ya "kazi' kila mmoja alijua lake.
Siku alizopata, alistarehe kwa kulewa, kujipatia wasichana wazuri na kulala vizuri katika majumba ya wageni ama kwenye nyumba za wasichana hao. Alipokosa alijutia na kujisahaurisha kwa kuvuta bhandi na kujilaza katika jumba hilo bovu.
Hivyo kwenye alfajiri hiyo aliona kama mwujiza kuona 'mzee' huyu mwenye dalili ya pesa na sura ya Kialhaji akitokea ndani ya moja ya vyumba vya jumba hili akiitumia njia yake ya siri! Mara moja wazo likamjia Luta?. Kwamba mzee huyu alikuja katika ghofu hili kwa sababu maalumu. Sababu ambayo Luta aliamini kuwa haikuwa nyingine zadi ya kuficha pesa au vitu vya thamani, Wazo hilo likamtuma kuanza upekuzi akitafuta chochote ambacho mzee huyo alikificha. Hakupata kitu. Hata hivyo alikuwa bado akiendelea na upekuzi wake 'mzee' aliporejea. Hima akajipenyeza katika chumba cha pili ambamo alijificha vizuri. Joram hakumuona. Darubini ya adui yake Joram kutoka nyumba ya pili pia haikuweza kumuona. Alitulia akimchungulia Joram ambaye aliketi akifanya mambo yake.
Kisha Bagambe alimuona mtu mwigine akinyatia nyumba hii mkononi kashika vitu ambavyo alivificha kwa hadhari chini ya mlango, Baada ya mtu huyo kushika hapa na pale aliondoka eneo hilo kwa hadhari na ukimya ule ule.
Kitu gani kitatokea?, Bagambe alijiuliza, Hakika moja alikuwa nayo. kuwa hii ilikuwa nafasi yake pekee ya 'kuukata'. Kwamba leo lazima ungekuwa mwisho wake wa maisha ya kubahatisha na mwanzo wa maisha mapya. Ingekuwaje vngine na eti bahati zinamfuata hadi huku badala ya yeye kuzifuata kwenye vituo vya basi? Hakuona sababu ya kuendelea kusubiri.
Kwa hadhari mfano wa paka anayemnyemelea panya, aliiendea sehemu hiyo aliyoona kitu kikifichwa. alipofika alipekua taratibu. Kisha aligusa waya fulani ambao hakutarajia kuuona hapo. Aliutazama waya huo kwa mshangao. Mshangao ambao ulikatizwa na mlipuko mkali uliomfanya apae juu na kutua chini akiwa tayari ametawanyika vipande mfano wa nyama za kopo, zinazoandaliwa kwa ajili ya kusindikwa.
****************************
Mlipiko huo ulimkuta Joram Kiango akiwa amesimama wima, fimbo mkononi. Aliduwaa alipoona ghafla mtu akizuka mbele yake na kupaa angani ambako alitawanyika vipande vipande. Lakini hakupata muda wa kuendelea kuduwaa, kwani wakati huo huo kila kitu kilikuwa kikipaa na kutua huku na huko kwa kishindo cha kutisha.
Kila kitu pamoja na Joram mwenyewe. Alijikuta angani kisha akajibwaga chini akifuatwa na lundo kubwa la vitu vizito ambavyo vilimfunika juu.
Joram hakuwa na muda wa kusikia maumivu pia. Alihisi kama mtu aliyepoteza kichwa au ubongo. Fahamu zikamtoka na nafsi yake kuchukuliwa na kiza kinachotisha.
******************************
Kifo cha kusikitisha! Joram aliwaza hivyo, karibu kila mtu kati ya umati mkubwa uliosimama kando kuizingira nyumba hiyo. Macho yenye hofu na huzuni yalikuwa yakiwatazama askari ambao walikuwa wakiviokota viungo vya marehemu kimoja baada ya kingine na kuvitia katika sanduku. Ni watu wachache sana walioweza kutazama tukio hili kwa muda mrefu. Wengi walitupa jicho kwa sekunde kadhaa na kisha kugeuza nyuso zao upande mwingine huku wakiguna na kufuta machozi. Mama mmoja alisikika akilia kwa sauti.
Ilikuwa mara ya kwanza kwa wengi wao kushuhudia tukio la mtu aliyepoteza maisha kwa njia hii ya kutisha.
Miongoni mwa walioshuhudia tukio hilo alikuwwepo Jodor Proper. Alikuwa mmoja wa watu waliofika mapema katika eneo hilo. Lakini alimkuta mtu wake aliyetega bomu hilo akijifuta vumbi baada ya ule mweleka alioupata kutokana na tofali lililomponda kichwani. Yeye alikuwa mmoja kati ya 'wapita njia' wanne waliojeruhiwa katika ajali hii. Proper alimsaidia mtu huyu kama asiyemfahamu. Walipopata mwanya walinong'onezana: "Kazi nzuri sana, Sasa nenda zako..."
Mtu huyo alipoondoka. Proper aliendelea kutazama 'ajali' huku akijitia kunung'unika. Lakini ndani ya moyo wake alikuwa akisherehekea na kushangilia sana tukio hilo. 'Kifo kinachomstahili kabisa' Aliwaza kwa furaha. "Mnofu mmoja mmoja! Na ajiunge basi tuuone huo ushujaa wake".
Wazo la kwamba huenda huyu akawa si adui yake mkubwa Joram Kiango halikumjia akilini. Ingawa haikuwa njia rahisi ya kuthibitisha mabaki hayo ya marehemu, lakini katika uchunguzi wake Proper alifanikiwa kuiona ile fimbo ya Joram na madevu yake ya bandia ambayo yaliokotwa na askari mmoja na kumwonyesha Inspekta wao ambaye alibabaika kama mtu aliyeguswa na simba. Kitendo hicho kilimfanya Proper ajisikie kucheka huku akijituliza. Wangetangaza nini tena wakati dunia nzima imefahamishwa zamani kuwa Joram Kiago amefariki dunia?.
Proper alipotoka katika eneo hilo kwa tabasamu, alikuwa na wazo moja tu la kuendelea na mipango yao bila kuwa na hofu yoyote. Kikwazo pekee alichoogopa yaani Joram Kiango kilikuwa tayari kimeingia kuzimu, kikiwasalimia babu zake huko.
Mmoja wa maofisa wa polisi alipendekeza wafanye uchunguzi wa kina ili kuhakiki kama eneo hili lilikuwa na maiti ama mareruhi wengine zaidi waliokandamizwa na kifusi. Lakini majirani wa eneo hilo waliwahakikishia polisi kuwa nyumba hiyo haikuwa na watu. Wakaondoka haraka haraka kwani kazi ya kufukua vifudi ilikuwa nzito, ambayo hakika ingewatoa jasho. Wakaondoka na mwili wa marehemu wakiuacha umati wa watu ukiendelea kufika katika eneo hilo kutazama kilichotokea.
Usiku ulipoingia, giza liliwaondoa watu katika eneo hilo likabaki katika hali yake ya kawaida.
ITAENDELEA 0784296253
Comments
Post a Comment