Dar es
Salaam Jumanne November 21, 2017; Kama
ilivyo ada, katika msimu huu wa sikukuu, Multichoice Tanzania imetangaza neema
kwa watanzania kwa kutoa ofa kabambe kwa wateja wake ambapo kuanzia leo mteja
mpya wa DStv ataweza kuunganishwa kwa shilingi 79,000 tu kwa vifaa
vyote pamoja na kifurushi cha DStv Bomba cha mwezi mzima.
Akizungumzia
ofa hiyo, kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania Hilda Nakajumo,
amesema kuwa Multichoice imekuwa na utamaduni wa miaka nenda rudi wa kuwapa
zawadi wateja na watanzania kwa ujumla na kwamba kila ufikapo msimu kama huu
DStv huwatunuku wateja wake ili kuwawezesha kufurahia zaidi msimu wa
sikukuu.
"Tunafahamu
kuwa msimu huu wa sikukuu familia nyingi zinaungana katika kusherehekea, hivyo
DStv imeamua kuwaongezea burudani kwa kutoa ofa hii kabambe". Amesema badala ya
mteja mpya kulipa shilingi 98,000 kwa ajili ya kuunganishwa pamoja na kifurushi
cha mwezi, sasa wateja wapya watalipa shilingi 79,000 tu na kuunganishwa na DStv pamoja na
kifurushi cha Bomba cha mwezi mzima.
“Tunapokuwa
nyumbani na familia zetu, watoto wanataka waangalie katuni, sisi kinamama
tunapenda kuangalia vipindi kama vile vya mapishi, urembo, na tamthilia,
kinababa nao hupenda sana kutazama michezo mbalimbali kama kandanda na
kadhalika. Ni kwa msingi huu tumeamua kuwarahisishia burunani hii inayopatikana
kutoka DStv” alisema Hilda na kuongeza kuwa wataendelea kutoa ofa kwa wateja
wao kila inapihitajika. Ofa hii ni
kwa nchi nzima na itaendelea kwa miezi miwili hadi Januari 15, 2018
Hilda amesema Ofa hii
kwa wateja wapya inakuja siku chache tu baada ya DStv kuanza kutoa zawadi kwa
wateja wake kwa kuwaongezea chaneli za SuperSport kwenye vifurushi vyao punde
walipiapo akaunti zao kabla hazijakatika. Katika ofa
hii ya kuongezewa chanel, wateja wa kifurushi cha Compact na Compact Plus watapata
chaneli zote za SuperSport zinazopatikana katika kifurushi cha DStv Premium kwa
kipindi cha siku saba (7) mfululizo bureeee!
Hali
kadhalika, watumiaji wa kifurushi DStv Bomba na DStv Family nao watapata chanel zote za Supersport
zinazopatikana kwenye Kifurushi DStv Compact na hivyo kuweza
kushuhudia mechi zote za Ligi ya Uingereza (PL) na mashindano mengine makubwa
kwa siku saba (7) mfululizo bureee! Multichoice
Tanzania imekuwa ikitoa huduma za DStv hapa nchini kwa Zaidi ya miaka 20 sasa
na imeendelea kuwa kinara katika kuwapatia watanzania habari, elimu na Zaidi ya
yote burudani kabambe.
Comments
Post a Comment